2010–2019
Uwezo, Furaha, na Upendo wa Kuweka Maagano
Oktoba 2013


Nguvu, Furaha, na Upendo wa Kuweka Agano

Nawaalika kila mmoja wetu kutathimini ni upendo kiasi gani tunavyompenda Mwokozi, tukitumia kama kipimo cha jinsi tunavyoweka maagano yetu kwa furaha.

Ningependa kuanza kwa kushiriki hadithi ambayo inagusa moyo wangu.

Jioni moja mtu aliita kondoo wake watano kuingia zizini kwa ajili ya usiku. Familia yake ilitazama kwa makini sana alipoita kwa urahisi, “Njoo,” na mara moja vichwa vyote vitano vikainuka na kugeuka kuelekea kwake. Kondoo wanne wakaanza kukimbia kuelekea kwake. Kwa upendo mkarimu aliwapapasa kwa upole kila moja ya wale wanne kwenye kichwa. Kondoo walijua sauti yake na kumpenda.

Lakini kondoo wa tano hakuja mbio. Alikuwa kondoo mkubwa wa kike ambaye wiki chache zilizopita alikuwa amepeanwa na mmiliki wake, ambaye aliripoti kwamba alikuwa mkali, mkaidi na kila mara aliwapotosha kondoo wengine. Mmiliki mpya alikubali kondoo na kumfungia katika shamba lake kwa siku chache ili ajifunze kutulia. Kwa subira alimfundisha kumpenda na kondoo wengine mpaka hatimaye alipokuwa na kamba fupi shingo mwake lakini kujifungia chini tena.

Jioni hiyo familia yake ikitazama, huyu mtu alimkaribia kondoo jike, aliyesimama ukingoni mwa shamba, na tena alisema kwa upole, “Njoo. Hujafungwa chini tena. Yuko huru.” Kisha kwa upendo alimfikia, akaweka mkono wake kichwani mwake, na kurudi pamoja naye na kondoo wengine kuelekea zizini.1

Kwa hisia ya hadithi hiyo, naomba kwamba Roho Mtakatifu atatusaidia kujifunza pamoja usiku wa leo juu ya kuweka agano. Kufanya na kuweka maagano kunamaanisha kuchagua kujifunga wenyewe kwa Baba yetu wa Mbinguni na Yesu Kristo. Ni kujitolea kufuata Mwokozi. Ni kumwamini Yeye na kutamani kuonyesha shukrani zetu kwa thamana Aliyolipa ili kutuweka huru kupitia kwa zawadi ya milele ya Upatanisho.

Mzee Jeffrey  R. Holland alieleza kwamba “agano ni mkataba wa kufunganisha, ahadi tukufu kwa Mungu Baba yetu kwamba tutaishi na kufikiri na kutenda kwa njia fulani- njia ya Mwanawe, Bwana Yesu Kristo. Badala yake, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu wanatuahidi fahari kamili ya uzima wa milele.”2 Katika mkataba huo wa kufunganisha, Bwana anaweka masharti na tunakubali kuyaweka. Kuweka na kushika maagano yetu ni onyesho la dhamira yetu wa kuwa kama Mwokozi.3 Kinachofaa ni kujitahidi kuwa na mtazamo ulioonyeshwa vyema katika vishazi vichache vya wimbo upendwayo: “Mimi nitaenda kule wewe unataka mimi niende. … Mimi nitasema kile wewe unataka mimi niseme…. Mimi nitakuwa kile wewe unataka mimi niwe.”4

Kwa nini Tuweke na Tushike Maagano ?

1. Kuweka maagano huimarisha, huwezesha, na kulinda.

Nefi aliona katika ono baraka kubwa Bwana Aliweka juu ya waweka agano. “Na ikawa kwamba mimi, Nefi, niliona nguvu za Mwanakondoo wa Mungu, kwamba ziliwashukia…watu wa agano wa Bwana, …na walikuwa wamejikinga kwa utakatifu na kwa nguvu za Mungu katika utukufu mkuu.”5

Hivi juzi nilikutana na rafiki mpendwa mpya. Yeye ni alishuhudia kwamba baada ya kupokea endaumenti yake ya hekalu, alihisi kuimarishwa kwa nguvu ya kupinga majaribu aliyopambana nayo awali.

Tunaposhika maagano yetu, tunapokea pia ujasiri na nguvu wa kutusaidia kubeba mizigo ya mmoja na ya mwingine. Dada aliyevunjika moyo alikuwa na mwana aliyekuwa akikabiliwa na changamoto ngumu za kimaisha. Kwa sababu ya imani yake kwa kina Dada wa Muungano wa Usaidizi wa kina Mama kama waweka agano, kwa ujasiri aliwaalika kufunga na kuomba kwa ajili ya mwanawe. Dada mwingine alieleza jinsi alitamani angeulizia sala kama hio kutoka kwa kina dada zake. Miaka iliyopita, mtoto wake alikuwa akiteseka. Yeye alitamani angewaalika ili kusaidia familia yake kubeba mzigo huu. Mwokozi alisema, “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”6

Ee, dada, sote tuna mizigo ya kubeba na kushiriki. Mwaliko wa kubeba mizigo ya mmoja kwa mwingine ni mwaliko wa kuweka maagano yetu. Shauri la Lucy Mack Smith kwa kina dada wa kwanza wa Muungano wa Usaidizi wa kina Mama ni muhimu zaidi leo kuliko hapo mbeleni: “Ni lazima tuthaminiane, tulindane, tufarijiane na kupata maelekezo, ili tuweze kukaa chini pamoja mbinguni.”7 Hii ndio njia bora ya kushika agano na mafundisho ya matembezi!

Kitabu cha Mormoni kinatukumbusha kwamba ilimbidi hata nabii Alma kubeba mzigo wa kuwa na mwana muasi. Lakini Alma alifanikiwa kubarikiwa na kina ndugu na dada waweka agano katika injili ambao waliongoka kwa dhati kwa Bwana na walikuwa wamejifunza kilichomaanisha kubeba mizigo ya kila mmoja. Tunafahamu mstari katika Mosia inayozungumza kuhusu imani kuu ya maombi ya Alma kwa niaba ya mwanawe. Lakini rekodi inaelezea kwamba “Bwana...alisikia sala za watu wake, na pia sala za mtumishi wake, Alma.”8

Tunajua kwamba Bwana siku zote Anafurahi “katika nafsi ambayo hutubu,”9 lakini tunatamani juu ya yote kuwezesha watoto wetu kufuata ushauri wa Rais Henry  B. Eyring wa “kuanza mapema na kuwa thabiti” katika kuweka na kushika maagano.10 Si muda mrefu uliopita, swali la kusisimua mawazo liliulizwa katika baraza la viongozi wa ukuhani na wasaidizi: “Je, kwa kweli tunatarajia watoto wa miaka minane kuweka ahadi zao” Tuliposhaurina pamoja, ilipendekezwa kuwa njia moja ya kuandaa watoto kufanya na kuweka maagano takatifu ya ubatizo ni kuwasaidia kufanya na kuweka ahadi rahisi.

Wazazi waaminifu wana haki ya kujua jinsi ya kufundisha bora na kukidhi mahitaji ya watoto wao. Wazazi wanapotafuta na kutenda kwa ufunuo wa kibinafsi, kushauri kwa pamoja, na kuhudumu na kufundisha kanuni rahisi za injili, watakuwa na uwezo wa kuimarisha na kulinda familia zao. Wanafamilia wengine wanaweza pia kusaidia. Babu yangu mwema alitufundisha umuhimu wa kuweka ahadi kupitia kwa wimbo rahisi. Ambao uliimbwa hivi: “Kabla ya kufanya ahadi, fikiria vizuri umuhimu wake. Kisha inapofanywa, iandike moyoni mwako. iandike moyoni mwako.” Wimbo huo mfupi ulifundishwa kwa upendo, imani, na nguvu kwa sababu Babu aliziandika ahadi zake mwenyewe moyoni mwake.

Mama mwenye busara hujumuisha watoto wake kwa makusudi katika juhudi zake za kuweka maagano yake. Yeye kwa furaha hubeba mizigo ya majirani, marafiki, na washiriki wa kata— na hufariji wale wanaohitaji faraja. Haikushangaza wakati binti yake mdogo alipokuja hivi majuzi akiuulizia usaidizi wa kujua jinsi ya kufariji vyema rafiki yake ambaye baba yake alikuwa amefariki. Hiyo ilikuwa fursa nzuri ya kufundisha kwamba hamu yake ya kumfariji rafiki yake ilikuwa njia moja ya kuweka ahadi yake ya ubatizo. Jinsi gani tunaweza kutarajia watoto kufanya na kuweka maagano ya hekalu ikiwa hatuwatarajii kuweka agano lao la kwanza —agano lao la ubatizo?

Mzee Richard  G. Scott aliona, “Mojawapo wa baraka kubwa tunazoweza kutoa kwa ulimwengu ni uwezo wa nyumba unaomtegemea Kristo ambapo injili inafundishwa, maagano yanawekwa, na upendo kudumu.”11 Ni kwa njia gani tunaweza kujenga nyumba kama hiyo ili kuandaa watoto wetu kufanya na kuweka maagano ya hekalu?

  • Tunaweza kugundua pamoja maana ya kuwa mstahiki wa sifu ya hekalu.

  • Tunaweza kugundua pamoja jinsi ya kusikiliza Roho Mtakatifu. Kwa sababu endaumenti ya hekalu inapokelewa kwa ufunuo, tunahitaji kujifunza ujuzi huo muhimu.

  • Tunaweza kugundua pamoja jinsi ya kujifunza kupitia kwa matumizi ya ishara, kuanzia kwa ishara takatifu za ubatizo na sakramenti.

  • Tunaweza kugundua pamoja kwa nini mwili ni takatifu, kwa nini wakati mwingine hujulikana kama hekalu, na jinsi mavazi ya heshima na mapambo yanahusiana na asili takatifu ya mavazi ya hekalu.

  • Tunaweza kugundua mpango wa furaha katika maandiko. Jinsi tunavyofahamu zaidi mpango wa Baba wa Mbinguni na Upatanisho katika maandiko, ndivyo ibada ya hekalu itakavyokuwa na maana zaidi.

  • Tunaweza kujifunza hadithi za mababu zetu pamoja, kutafiti historia ya familia, fahirisi, na kufanya kazi kwa niaba kwa wapendwa waliokufa.

  • Tunaweza kugundua pamoja maana ya maneno kama vile endaumenti, agizo, kuunganisha, ukuhani, funguo, na maneno mengine yanayohusiana na ibada ya hekaluni.

  • Tunaweza kufundisha kwamba tunaenda hekaluni kufanya maagano na Baba wa Mbinguni--- tunarudi nyumbani kuyaweka! 12

Acha tukumbuke dhana ya “nzuri, bora, na bora zaidi” tunapofundisha.13 Ni vizuri kufundisha watoto wetu juu ya Hekalu. Ni bora kuwaandaa na kuwatarajia kufanya na kuweka maagano. Ni bora kuwaonyesha kwa mfano kwamba tunashika kwa furaha maagano yetu ya ubatizo na hekalu! Kina dada, je, tunatambua wajibu wetu muhimu katika kazi ya wokovu tunapolea, kufundisha, na kuandaa watoto kuendelea katika njia ya agano? Uwezo wa kufanya hivyo utakuja tunapoheshimu na kuweka maagano yetu.

2. Kuweka maagano ni muhimu kwa furaha ya kweli.

Rais Thomas  S. Monson alifundisha, “Maagano Takatifu yanapaswa kuheshimiwa na sisi, na uaminifu kwao ni sharti kwa furaha.”14 Katika  2  Nefi inaeleza kwa urahisi, “Na ikawa kwamba tuliishi kwa furaha.”15 Mapema katika sura hii tunajifunza kwamba Nefi na watu wake walikuwa wamejenga hekalu. Hakika walikuwa waweka agano wenye furaha! Na katika Alma tunasoma, “Lakini tazama hakujakuwa wakati wa furaha miongoni mwa watu wa Nefi, tangu siku ya Nefi, kuliko siku za Moroni.”16Kwa nini? Tena tunajifunza katika mstari uliopita kwamba walikuwa “waaminifu kwa kutii amri za Bwana.”17 Waweka agano ni waweka amri!

Nalipenda andiko lisemalo: “Na sasa wakati watu waliposikia haya maneno[kumaanisha maneno yanayoelezea agano la ubatizo] walipiga makofi kwa shangwe, na wakasema kwa nguvu: Hili ndilo pendo la mioyo yetu.”18 napenda pendo la mioyo yao. Walipenda kwa furaha kufanya na kuweka ahadi zao!

Jumapili moja msichana alisema kwa furaha, “Nitaweza kushiriki sakramenti leo!” Ni lini mara ya mwisho tulipofurahi kwa fursa hiyo? Na tunaidhihirisha kwa njia gani? Tunafanya hivyo kwa kumkumbuka Mwokozi daima na daima kuweka amri Zake, ambayo ni pamoja na kuweka siku Yake ya Sabato takatifu. Tunafanya hivyo kwa kumkumbuka daima tunapokuwa na sala zetu za binafsi na za familia daima masomo ya maandiko ya kila siku, na jioni ya familia nyumbani ya kila wiki. Na tunaposahau au kulegea kwa mambo haya muhimu, tunatubu na kuanza tena.

Kufanya na kuweka maagano yetu kwa furaha hutoa uhalali na maisha kwa maagizo muhimu takatifu na ya kuokoa tunayopaswa kupokea ili kupata “yote Baba aliyonayo.”19 Maagizo na maagano ndiyo “hatua muhimu za kiroho” ambazo Rais Henry  B. Eyring alirejea wakati alipofundisha: Watakatifu wa siku za mwisho ni watu wa agano. Tangu siku ya ubatizo kupitia kwa hatua muhimu za kiroho za maisha yetu, tunafanya ahadi na Mungu na Yeye anafanya ahadi na sisi. Kila mara Yeye daima hutimiza ahadi zake zinazotolewa kupitia kwa watumishi Wake wenye mamlaka, lakini ni mtihani muhimu wa maisha yetu kuona kama sisi tutafanya na kuweka maagano yetu na Yeye.”20

3. Kuweka maagano yetu inaonyesha upendo wetu kwa Mwokozi wetu na Baba yetu wa Mbinguni.

Kati ya sababu zote zinazotubidii kuwa watendaji zaidi katika kuweka maagano kwetu, sababu hii inalazimisha zaidi ya yote---upendo. Mstari katika Agano la Kale ni moja ambao unagusa moyo wangu tunapofikiria kanuni ya upendo. Ni nani wa kwetu asiyeguswa na hadithi ya biblia ya Yakobo na Raheli ya upendo tunaposoma, “Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli; ikawa machoni pake kama siku tu, kwa vile alivyompenda”?21 Kina dada, je, sisi hushika maagano yetu kwa aina hiyo ya upendo wa kina na wa dhati?

Kwa nini Mwokozi alikuwa tayari kuweka ahadi yake na Baba na kutimiza utume Wake wa kiuungu ili kulipia dhambi za ulimwengu? Ilikuwa ni upendo wake kwa Baba Yake na upendo wake kwa ajili yetu. Kwa nini Baba alikuwa tayari kuruhusu Mwanawe wa pekee na mkamilifu kuteseka maumivu makali yasiyoelezeka ili kubeba dhambi, machungu, magonjwa, na udhaifu wa dunia na vyote visivyofaa katika maisha haya? Tunapata jibu katika maneno haya: “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee.”22

“Kama tutakubali kikamilifu baraka nyingi ambazo ni zetu kupitia kwa ukombozi uliotolewa kwa ajili yetu, hakuna chochote ambacho Bwana angeuliza kutoka kwetu tusichoweza kufanya bila wasiwasi na kwa hiari.”23 Kulingana na kauli hii ya Rais Joseph Fielding Smith, kushika agano ni njia mojawapo ya kuonyesha upendo wetu kwa Upatanisho usioeleweka na usio na mwisho wa Mwokozi na Mkombozi wetu na upendo kamili wa Baba yetu wa Mbinguni.

Mzee Holland kwamba alipendekeza kwa upendo, “Sina hakika jinsi hali yetu itakavyokuwa Siku ya Hukumu, lakini nitashangaa sana kama wakati fulani katika mazungumzo hayo, Mungu hatatuuliza hasa kile Kristo alimuuliza Petro: ‘Je, unanipenda?’ ”24 Usiku wa leo ninaalika kila mmoja wetu kutathmini ni kiasi gani tunampenda Mwokozi, kwa kutumia kama kipimo jinsi tunavyoweka kwa furaha maagano yetu. Mwokozi alisema, “Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”25 Jinsi gani tunavyohitaji udhihirisho wa kila mara wa Mwokozi katika maisha yetu ya kila siku!

Acha tukumbuke kwamba hata wale ambao wameasi hapo nyuma au ambao kwa sasa wanajitahidi waweze kuhisi mguso wa mkono wa Mchungaji Mwema juu ya vichwa vyao na kusikia sauti yake ikisema : “Njoo. Hujafungwa chini tena. Uko huru.” Mwokozi alisema, “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.”26 Anaweza kusema hivyo kwa sababu Aliweka maagano yake kwa upendo. Swali basi ni, tutaweza? Acha tuenende kwa imani, mioyo yenye furaha, na hamu kubwa ya kuwa watunza agano. Hivi ndivyo tunavyoonyesha upendo wetu kwa Baba yetu wa Mbinguni na Mwokozi wetu, wote ambao juu yao mimi nashuhudia kwa upendo mkubwa, katika jina la Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. Ona D. Todd Christofferson, “You Are Free,” Ensign, Mar. 2013, 38, 40; au Liahona, Mar. 2013, 16, 18.

  2. Jeffrey R. Holland, “Keeping Covenants: A Message for Those Who Will Serve a Mission,” New Era, Jan. 2012, 3; au Liahona, Jan. 2012, 49.

  3. Ona “Understanding Our Covenants with God,” Ensign, July 2012, 25; au Liahona, July 2012, 23.

  4. “I’ll Go Where You Want Me to Go,” Hymns, no. 270; mkazo umeongezewa.

  5. 1 Nefi 14:14.

  6. Yohana 13:35.

  7. Lucy Mack Smith, katika Daughters in My Kingdom: The History and Work of Relief Society (2011), 25.

  8. Mosia 27:14; mkazo umeongezewa.

  9. Mafundisho na Maagano 18:13.

  10. Ona Henry B. Eyring, “Spiritual Preparedness: Start Early and Be Steady,” Ensign au Liahona, Nov. 2005, 37–40.

  11. Richard G. Scott, “For Peace at Home,” Ensign au Liahona, May 2013, 30.

  12. Ona D. Todd Christofferson, “The Gospel Answers Life’s Problems and Challenges” (mkutano wa uongozi wa duniani kote, Feb. 2012); lds.org/broadcasts.

  13. Ona Dallin H. Oaks, “Good, Better, Best,” Ensign au Liahona, Nov. 2007, 104.

  14. Thomas S. Monson, “Happiness—the Universal Quest,” Ensign, Oct. 1993, 4; au Liahona, Mar. 1996, 5.

  15. 2 Nefi 5:27.

  16. Alma 50:23.

  17. Alma 50:22.

  18. Mosia 18:11.

  19. Mafundisho na Maagano 84:38.

  20. Henry B. Eyring, “Witnesses for God,” Ensign, Nov. 1996, 30; mkazo umeongezewa.

  21. Mwanzo 29:20.

  22. Yohana 3:16.

  23. Joseph Fielding Smith, “Importance of the Sacrament Meeting,” Relief Society Magazine, Oct. 1943, 592.

  24. Jeffrey R. Holland, “The First Great Commandment,” Ensign au Liahona, Nov. 2012, 84.

  25. Yohana 14:21.

  26. Yohana 10:11.