2010–2019
Shukrani katika Hali Yoyote.
Aprili 2014


Shukrani katika Hali Yoyote.

Je! Sisi hatuna sababu ya kujawa na shukrani, bila kujali hali ambazo sisi tunajipata ndani yake?

Kwa maika mingi, nimepata kuwa na fursa takatifu kukutana na watu wengi ambao huzuni wao unaonekana umewaathiri kwa kina roho zao. Katika nyakati hizi, nimewasikiliza wapendwa ndugu na dada zangu na nimehuzunika pamoja nao kuhusu mizigo yao. Nimetafakari nini cha kusema kwao, na nimejitahidi sana kujua jinsi ya kuwafariji na kuwasaidia katika majaribio yao.

Mara nyingi huzuni wao unasababishwa na kile kinachoonekana kwao kama ni mwisho. Wengine wanapata uzoefu wa mwisho wa uhusiano uliotunzwa, kama kifo cha mpendwa wao au utengano kutoka kwa mwana familia. Wengine wanahisi wanakabiliana na mwisho wa matumaini---matumaini ya kuoa na kuolewa au kuzaa watoto au kushinda ugonjwa. Wengine wanaweza kukabiliana na mwisho wa imani yao, wakati ushawishi unaochanganya na kupingana katika ulimwengu unawajaribu kuwa na shaka, hata kutelekeza, kile ambacho hapo mwanzo walijua kuwa ni kweli.

Hapana budi, naamii kwamba sisi sote tuna uzoefu wa muda ambapo inaonekana kwamba kila kitu kinakwenda visivyo katika maisha yetu, na kutuacha tukijihisi wapweke, tuliokatishwa tamaa na tusiokanyika.

Inaweza kumtokea yeyote. Hakuna aliye na kinga.

Tunaweza kuwa Wenye Shukrani

Hali ya kila mtu ni tofauti, na utondoti wa kila maisha ni wa kipekee. Hata hivyo, mimi nimejifunza kwamba kuna kitu ambacho kingeweza kuondoa uchungu ambao unaweza kuja katika maisha yetu. Kuna kitu kimoja tunaweza kufanya maisha ya matamu zaidi, yawe na shangwe zaidi, hata matukufu.

Tunaweza kuwa wenye shukrani!

Inaweza kuonekana kinyume kwa busara za ulimwengu kupendekeza kwamba mtu aliyelemewa na huzuni angetoa shukrani kwa Mungu. Lakini wale wanaoweka kando chupa ya machungu na kuinua glasi ya shukrani wanaweza kupata kinywaji cha utakaso cha uponyaji, amani, na uelewa.

Kama wafuasi wa Kristo, tunaamriwa ”kumshukuru Bwana [wetu] Mungu katika vitu vyote,”1 “Kuimba kwa Bwana kwa shukrani,”2 na “kuruhusu moyo [wetu] ujae shukrani kwa Mungu.”3

Kwa nini Mungu anatuamuru sisi tuwe na shukrani?

Amri zake zote zimetolewa kufanya baraka zipatikane kwetu. Amri ni fursa ya kutumia wakala wetu wa kuchagua na kupokea baraka. Baba yetu wa Mbinguni mwenye upendo anajua kwamba kuchagua kuendeleza roho ya shukrani kutatuletea shangwe ya kweli na furaha tele.

Kuwa na Shukrani kwa ajili ya Vitu

Lakini baadhi wanaweza kusema, “Ni kwa kitu gani nimekuwa na shukrani kwacho wakati ulimwengu wangu unasambaratikana?

Labda kuzingatia kile tunachokuwa na shukrani nacho ni mtizamo usio sahihi. Ni vigumu kukuza roho ya shukrani ikiwa kiwango chetu cha shukrani kinategemea ni kiasi gani cha baraka tulizonazo. Kweli, ni muhimu kwa kawaida “ kuhesabu baraka zetu”---na yeyote ambae amejaribu hivi anajua ni nyingi---lakini mimi siamini Bwana anatarajia sisi tuwe wenye shukrani kidogo katika wakati wa majaribio kuliko kwenye wakati tunapokuwa na wingi wa vitu na maisha yetu ni rahisi. Kwa kweli, nyingi za kumbukumbu za kimaandiko hazizungumzii juu ya shukrani kwa vitu lakini kwa kiasi zinapendekeza roho jumla au mtizamo wa shukrani.

Ni rahisi kuwa na shukrani kwa vitu wakati maisha yetu yanaonekana yakienda vizuri. Lakini vipi kuhusu nyakati ambapo kile tunachotamani kinaonekana kuwa mbali sana na uwezo wetu?

Napendekeza kwamba tuone shukrani kuwa mwelekeo wa asili, njia ya maisha ambayo haitegemei na hali yetu ya sasa? Kwa maneno mengine, napendekeza kwamba badala ya kuwa na “shukranikwa ajili ya vitu,” tuzingatie kuwa na “shukrani wakati tupo katika hali zetu”---kwa hali yeyote itakavyokuwa.

Kuna hadithi ya zamani ya mhudumu aliyemwuliza mteja kama amefaidi mlo. Mgeni alijibu kwamba kila kitu kilikuwa sawa, lakini ingekuwa vizuri zaidi kama mhudumu angeongeza mkate zaidi. Siku iliyofuata, wakati yule mtu aliporudi, mhudumu aliongeza mara dufu kiasi cha mkate, akampa slesi nne badala ya mbili, lakini bado yule mtu hakufurahi. Siku iliyofuata, mhudumu akaongeza tena mkate mara dufu, bila mafanikio.

Siku ya nne, mhudumu alikuwa hasa amedhamiria kumfanya yule mtu afurahi, kwa hiyo alichukua mkate wenye urefu wa futi-tisa (3-m) akaukata nusu mbili na kwa tabasamu, akamhudumia mteja. Mhudumu alikuwa na shauku kuona furaha ya mtu yule.

Baada ya mlo, yule mtu alitazama juu na kusema, “Ni vizuri kama kawaida. Lakini naona umerudia tena kutoa slesi mbili tu za mkate.

Kuwa wenye shukrani katika hali zetu

Ndugu na akina Dada wapendwa, uchaguzi ni wetu.Tunaweza kuchagua kuweka kikomo cha shukrani zetu, kutegemea baraka tunazohisi tumekosa. Au tunaweza kuchagua kuwa kama Nefi, ambaye moyo wake wa shukrani kamwe haukusita. Wakati kaka zake walipomfunga kwenye meli---ambayo alikuwa ameijenga kuwachukua kuwapeleka nchi ya ahadi---visigino vyake na vifundo vya mikono vilikuwa na vidonda kiasi kwamba “vilikuwa vimevimba” sana na dhoruba kali ilitishia kumzamisha katika kilindi cha bahari. “Hata hivyo” Nefi alisema, “Nilimtazama Mungu wangu, na nilimsifu siku yote nzima; na sikumlalamikia Bwana kwa sababu ya masumbuko yangu.”4

Tunaweza kuchagua kuwa kama Ayubu, aliyeonekana kuwa na kila kitu lakini kisha akapoteza vyote. Bado Ayubu alijibu kwa kusema,” Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena …. : Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.”5

Tunaweza kuchagua kuwa kama watangulizi Wamormoni, ambao walidumisha roho ya shukrani wakati wa safari yao ya polepole na maumivu kuelekea Great Salt Lake, hata kuimba na kucheza na hata kushangilia kwa sababu ya wema wa Mungu.6 Wengi wetu tungehisi dhamira halisi ya kujitoa, kulalamika, na kusikitishwa na ugumu wa safari.

Tunaweza kuchagua kuwa kama Nabii Joseph Smith, ambaye wakati ni mfungwa katika hali zenye taabu katika Jela la Liberty, aliandika maneno ya kuvutia: “Kwa hiyo, ndugu wapendwa, kwa furaha na tufanye mambo yote yaliyo katika uwezo wetu; na ndipo tusimame imara, kwa uhakika mkubwa, kuuona wokovu wa Mungu, na kwa mkono wake kufunuliwa.”7

Tunaweza kuchagua kuwa wenye shukrani, haidhuru vipi.

Aina hii ya shukrani inaweza kuwepo bila kujali nini kinachotendeka karibu nasi. Ni kubwa zaidi ya masikitiko, kuvunjika moyo, na kukata tamaa. Huchanuka kwa urembo kama vile katika mandhari ya barafu ya msimu wa baridi jinsi inavyokuwa katika joto zuri la msimu wa joto.

Wakati tunapokuwa na shukrani kwa Mungu katika hali zetu, tunaweza kuwa na uzoefu wa amani ya upole wakati tuko katikati ya majaribio. Wakati tunahisi huzuni, tunaweza bado kuinua mioyo yetu katika sifa. Wakati tunahisi maumivu tunaweza kushangilia kwa sababu ya Upatanisho wa Kristo. Katika ubaridi wa huzuni mkali tunaweza kupata uzoefu wa ukaribu na joto la kumbatio la mbinguni.

Wakati mwingine tunafikiri kwamba kuwa na shukrani ni kile tunachofanya baada ya matatizo yetu kutatuliwa, lakini huo ni mtizamo finyu jinsi gani. Ni kiasi gani cha maisha tunachokosa kwa kungojea kuona upinde kabla ya kumshukuru Mungu kwamba kutakuwa na mvua?

Kuwa wenye shukrani katika wakati wa dhiki si kumaanisha kwamba tunafurahishwa na hali zetu. Inamaanisha kwamba kupitia kwa macho ya imani tunatazama mbele zaidi ya changamoto za siku yetu ya leo.

Hii sio tu shukrani ya midomo bali ni ya nafsi. Ni shukrani ambayo huponya moyo na kupanua akili.

Shukrani kama Kitendo cha Imani

Kuwa na shukrani katika hali zetu ni kitendo cha imani katika Mungu. Inahitaji kwamba tumtegemee Mungu na kutegemea vitu tusivyoweza kuviona lakini ambavyo ni vya kweli.8 Kwa kuwa wenye shukrani, tunafuata mfano wa Mwokozi wetu mpendwa, ambaye alisema,”Sio mapenzi yangu, bali yako, yatimizwe.”9

Shukrani ya kweli ni onyesho la matumaini na ushuhuda. Inakuja kutokana na kutambua kwamba wakati wote hatuelewi majaribio ya maisha lakini kwa kuamini kwamba siku moja tutaelewa.

Kwa hali yoyote ile, hisi zetu za shukrani zitanawirishwa na wingi wa kweli takatifu tusizojua: kwamba Baba yetu amewapa watoto Wake mpango mkubwa wa furaha; kwamba kupitia kwa Upatanisho wa Mwanae,Yesu Kristo, tunaweza kuishi milele na wapendwa wetu; kwamba mwishowe, tutakuwa na miili ya utukufu, kamili, na isiyo kufa, isiyolemewa na ugonjwa au ulemavu; na kwamba machozi yetu ya huzuni na upotevu yatabadilishwa na wingi wa shangwe na furaha, “kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa---sukwa hata kumwagika.”10

Ni sharti ingekuwa aina hii ya ushuhuda ambao uliwabadilisha Mitume wa Mwokozi kutoka kuwa waoga, wanaume wenye shaka na kuwa wasio na hofu, wawakilishi wa Bwana wenye furaha. Katika masaa kufuatia Kusulibiwa Kwake, walijawa na hofu na huzuni, kutokuelewa nini hasa kilichotokea. Lakini tukio moja lilibadilisha vyote hivyo. Bwana wao aliwatokea na kutangaza,”Tazameni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe.”11

Wakati Mitume walipomtambua Kristo aliyefufuka---walipopata uzoefu wa utukufu wa Ufufuo wa Mwokozi mpendwa wao---walikuwa watu tofauti. Hakuna kingewazuia kutimiza ujumbe wao. Walikubali kwa ujasiri na ushupavu mateso, kudhalilishwa, hata kifo ambacho kingekuja kwao kwa sababu ya ushuhuda wao.12 Hawakuzuiliwa kumsifia na kumtumikia Bwana wao. Walibadilisha maisha ya watu kila sehemu. Walibadilisha Ulimwengu.

Huhitaji kumwona Mwokozi, kama walivyofanya Mitume kupata uzoefu wa mbadiliko sawa na huo. Ushuhuda wako wa Kristo, unaokuja toka kwa Roho Mtakatifu unaweza kukusaidia kuangalia nyuma miisho ya kusikitisha katika maisha ya umauti na kuona mategemeo ambayo Mkombozi wa Ulimwengu ameyatayarisha.

Hatukutengenezwa kwa Miisho

Kwa kufikiria kile tunachojua kuhusu kudra yetu ya milele, si ajabu kwamba tunapokabiliwa na miisho ya maisha, inaonekana kuwa haikubaliki kwetu? Inaonekana kuwa kuna kitu ndani yetu kinazuia miisho.

Kwa nini hivi? Kwa sababu tumetegenezwa kwa nyenzo za milele. Sisi ni viumbe vya milele, watoto wa Mwenyezi Mungu ambaye jina lake ni Asiye na Mwisho13 na ambaye huahidi baraka za milele zisizo na mwisho. Miisho sio kudra yetu.

Tunapozidi kujifunza injili ya Yesu Kristo, ndiyo zaidi tunaelewa kwamba miisho hapa katika umauti sio miisho kabisa. Ni mikatizo tuu---ya mapumziko ya muda ambayo siku moja itaonekana midogo ikifananishwa na furaha ya milele ambayo watapewa watu ambao ni waaminifu.

Nina shukrani jinsi gani kwa Baba yangu wa Mbinguni kwamba katika mpango wake hakuna miisho halisi ila mianzo ya milele.

Wale Wenye Shukrani Watafanywa kuwa Watakatifu.

Ndugu na akina dada, je, hatuna sababu ya kujawa na shukrani, bila kujali hali tunazojipata ndani yake?

Hatuhitaji sababu yeyote kubwa kujazwa mioyoni mwetu “kwa kina na shukrani kwa Mungu”?14

“Je, hatuna sababu kubwa ya kushangilia?”15

Tutabarikiwa sana jinsi gani kama tunatambua kazi ya mikono ya Mungu katika ufumaji wa ajabu wa maisha. Shukrani kwa Baba yetu wa Mbinguni hupanua utambuzi wetu na husafisha kuona kwetu. Inavutia unyenyekevu na inajenga hisia za huruma kuelekea binadamu wenzetu na viumbe vyote vya Mungu. Shukrani ni kichocheo cha sifa zote za Kikristo! Moyo wenye shukrani ni mzazi wa wema wote.16

Bwana ametupa ahadi Yake kwamba “yule apokeaye vitu kwa shukrani atatukuzwa; na vitu vya dunia hii ataongezewa, hata mara mia, ndio, zaidi.”17

Na acha sisi “tuishi katika kutoa shukrani kila siku”18—hasusani wakati unaoonekana kuwa wa miisho isiyoelezeka ambayo ni sehemu ya maisha ya muda. Na acha sisi turuhusu nafsi zetu, zipanuke kwa shukrani, kuelekea kwa Baba yetu wa Mbinguni mwenye rehema. Na acha sisi daima na kila mara tupaze sauti zetu na kuonyesha kwa maneno na vitendo shukrani zetu kwa Baba yetu aliye Mbinguni na kwa Mwanawe Mpendwa, Yesu Kristo. Kwa hayo ninaomba, na kuwaachia ushuhuda na baraka, katika jina la Bwana wetu, Yesu Kristo, amina.