2010–2019
Matamanio ya Roho ya Dhati
Oktoba 2016


Matamanio ya Roho ya Dhati

Kila wakati wa sala ya thamani unaweza kuwa muda mtakatifu tukiwa pamoja na Baba, katika jina la Yesu Kristo, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Katika mapambano ya maisha ya duniani, kamwe hatuko peke yetu kukamilisha kazi zetu, kupigana vita vyetu, kukabiliana na dhiki au maswali ambayo hayajajibiwa. Yesu Kristo alifundisha kwa fumbo “kwamba watu wanatakiwa siku zote kusali, na bila kuchoka.”1 Alizungumza kuhusu hakimu ambaye hakumcha Mungu, na wala hakujali mtu. Kila siku, mjane alikuja mbele yake, akisihi alipiziwe kisasi dhidi ya adui yake. Kwa wakati, hakimu hakutoa usaidizi wowote. Lakini kama matokeo ya uaminifu na msimamo wa kusihi, hakimu hatimaye alifikiri, “kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampa haki yake, asije kunichosha kwa kunijia daima.”

Kisha Yesu alielezea:

“Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu … ?

“Nawaambia, atawapatia haki upesi.”

Na kisha Bwana anauliza swali hili: “Walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?”1

Maombi ni muhimu katika kujenga imani. Wakati Bwana atakapokuja tena atawapata watu wanaojua kuomba kwa imani na walio tayari kupokea wokovu? “Kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokoka.”2 Sisi ni watoto wa Baba wa Mbinguni mwenye upendo, na tunaweza kufurahia mawasiliano ya kibinafsi pamoja Naye wakati tunasali “kwa moyo wa kweli, na kusudi halisi, tukiwa na imani katika Kristo”3 na kisha kutenda kufuatana na majibu tunayopokea kwa hisia za Roho Mtakatifu. Kwa imani tunasali, tunasikiliza, na tunatii ili tujifunze na kuwa kitu kimoja na Baba na Mwana.4

Sala ya imani hufungua njia ya kupokea baraka tukufu kutoka mbinguni. Mwokozi alifundisha:

“Ombeni, nanyi mtapewa tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa:

“Kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.”5

Kama tunategemea kupokea, ni lazima tuombe, tutafute na kubisha. Katika upekuzi wake wa ukweli, Joseph Smith alisoma kutoka katika maandiko “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.”6 Kama jibu la maombi yake ya imani, mbingu zilifunguka. Mungu Baba na Mwanawe, Yesu Kristo,walishuka katika utukufu na wakazungumza na Joseph, wakianzisha kipindi cha utimilifu wa Nyakati. Kwetu, uponyaji wa kimiujiza, ulinzi wa nguvu, uelewa wa milele, msamaha unaoweka huru, na amani ya thamani ni kati ya majibu yanayotujia tunapotoa “matamanio ya kweli ya roho zetu”7 kwa imani.

Tunasali kwa Baba yetu, katika jina la Yesu Kristo, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, hivyo kuwashirikisha washiriki wote wa Uungu katika matamshi yetu.

Tunasali kwa Baba yetu wa Mbinguni na kwake Yeye pekee kwa sababu Yeye ni “Mungu aliye Mbinguni, na asiye na mwisho na ni wa milele, kutoka milele hata milele …  , aliyezifanya mbingu na dunia, na vitu vyote vilivyomo ndani yake.” Kama Muumbaji wetu, Alitoa amri kwamba “inatupasa kumpenda na kumtumikia Yeye, pekee aliye hai na Mungu wa kweli, na kwamba yapasa awe pekee tunayepaswa kumwabudu.”8

Unapoomba kwa Baba wa Mbinguni kwa imani, “atakufariji katika mateso yako … [na unaweza] kusherehekea upendo wake.”9 Rais Henry  B. Eyring alishiriki kwamba sala za baba yake wakati alipokuwa akipoteza vita dhidi ya saratani zilimfundisha uhusiano binafsi wa kina kati ya Mungu na watoto Wake:

“Wakati maumivu yalipokuwa makali sana, tulimkuta asubuhi amepiga magoti pembeni mwa kitanda chake. Alikuwa amekuwa dhaifu mno kurudi kitandani mwake. Alituambia amekuwa akisali akimwuliza Baba yake wa Mbinguni, kwa nini alibidi ateseke kiasi kile na hali amejaribu siku zote kuwa mwema. Alisema jibu la huruma lilikuja: ‘Mungu anawataka wana hodari.’

“Kwa hiyo alisonga mbele kwa ujasiri mpaka mwisho, akiamini kwamba Mungu alimpenda, alimsikiliza na angemwinua juu. Alibarikiwa kujua mapema na kamwe kutosahau kwamba Mungu mwenye upendo yu karibu kama sala.”10

Tunasali katika jina la Yesu Kristo kwa sababu wokovu wetu ni katika Kristo, na “hapana jina lingine lolote chini ya mbingu walilopewa wanadamu, litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”11 Sisi tunakuja kwa Baba katika jina takatifu la Yesu Kristo12 kwa sababu Yeye ni wakili wetu kwa Baba na Anatetea kesi yetu.13 Aliteseka, alitokwa damu, na alikufa kumtukuza Baba yake, na ombi Lake la huruma kwa niaba yetu linafungua njia kwa kila mmoja wetu kupata amani katika maisha haya na maisha ya milele katika ulimwengu ujao Hataki sisi tuteseke kwa muda mrefu au kuvumilia majaribu zaidi ya inavyohitajika. Tunamgeukia Yesu Kristo na kumruhusu kuufanya mwepesi mzigo wetu, kuponya mioyo yetu, na kusafisha roho zetu kupitia kwa uwezo Wake wa kutakasa. Kamwe hatutaki kulitaja jina Lake bure kwa kukariri na maneno ya kurudia rudia Sala za kweli zikitolewa katika jina takatifu la Yesu Kristo ni sura maalumu ya upendo wetu, shukrani zetu za milele, na matumaini yetu thabiti kusali kama alivyosali, kufanya kama alivyofanya, na kuwa kama alivyo.

Tunasali kwa nguvu ya Roho Mtakatifu kwa sababu “yule ambaye anaomba katika Roho anaomba kufuatana na mapenzi ya Mungu.”14 Tunapoomba kwa imani, Roho Mtakatifu anaweza kuongoza mawazo yetu ili kwamba maneno yetu yapatane na mapenzi ya Mungu. “Msiulize, ili mle kwa tamaa yenu, lakini ulizeni kwa udhabiti usiotingishika, kwamba msilegee kwa majaribu yoyote, lakini kwamba mheshimu Mungu wa kweli na aishie.”15

“Sio tu muhimu kwamba tunajua jinsi ya kusali, lakini vilevile ni muhimu kwamba hatuna budi kujua jinsi ya kupokea jibu kwa sala zetu, kuweza kutambua, kuwa tayari, kuweza kiona kwa maono ya wazi na kuelewa kwa uwazi nia ya mapenzi na madhumuni ya Mungu kutuhusu sisi.”16

Rais Eyring alisema: “Nimekuwa na sala zilizojibiwa. Majibu hayo yalikuwa wazi kabisa wakati kile nilichokitaka kilinyamazishwa na mahitaji yaliyoshinda kujua nini Mungu alitaka. Ni wakati huo kwamba jibu kutoka kwa Baba wa Mbinguni mwenye upendo linaweza kusemwa kwenye akili na sauti ya dhamira na inaweza kuandikwa kwenye moyo.”17

Picha
Kristo akiwa na Mitume
Picha
Kristo katika Gethsemane

Wakati Mwokozi alipoingia Bustani ya Gethsemane, roho Yake ilikuwa na huzuni mwingi hata kufikia kifo. Katika maumivu, mtu pekee angeweza kumgeukia alikuwa Baba Yake. Alimsihi, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke.” Lakini aliongezea, “Lakini aliongeza, “Walakini sio kama nitakavyo mimi, bali kama utavyo wewe.”18 Ingawa hakuwa na dhambi, Mwokozi aliagizwa “[kuteseka] maumivu na mateso na majaribu ya kila aina,” ikijumuisha magonjwa na udhaifu wa watu Wake. “[Yeye] aliteseka katika mwili ili achukue dhambi za watu wake, kwamba aondoe uvunjaji wao wa sheria kulingana na nguvu za ukombozi wake.”19 Mara tatu Yeye aliomba, “Baba, mapenzi yako yatimizwe.”20 Kikombe hakikuondolewa. Katika sala unyenyekevu na imani Yeye aliimarishwa kwenda mbele na kukamilisha utumishi Wake mtakatifu kutayarisha ukombozi wa wanadamu wote, ili wote waweze kutubu, kuamini, na kutii waweze kupata baraka za milele.

Picha
Kristo aliomba katika Gethsemane

Majibu tunayopokea katika sala yanaweza yasiwe kile ambacho tungetamani. Lakini katika muda wa matatizo, sala zetu zinakuwa tegemeo kuu la upendo na huruma ororo. Katika kusihi kwetu, tunaweza kuimarishwa kwenda mbele na kutimiza yale yote tuliyotawazwa kufanya. Kwa Watakatifu wake wanaoishi katika wakati wa hatari, Bwana anasema , “Kwa hiyo, mioyo yenu na ifarijike … ; kwa kuwa wenye mwili wote tulieni na jueni kuwa Mimi ni Mungu.”21

Kama sala zetu zitolewa kibinafsi, katika familia, kanisani, au katika hekalu; kama tunasali na moyo uliovunjika na roho iliyopondeka kutafuta hekima ya mbinguni au nguvu ya kuvumilia, tunasali daima na mioyo iliyojaa, iliyovutwa kwa Mungu wakati wote kwa ajili ya ustawi wetu na ustawi wa wale wanatuzunguka. Tamaa za kweli zilizotolewa katika roho ya shukrani kwa baraka nyingi na shukrani kwa masomo ya maisha hutia mioyo mwetu imani thabiti, “tumaini angavu, upendo wa Mungu na wa watu wote.”22

Ni karama kutoka kwa Mungu. Hatuhitaji kamwe kuhisi tupo peke yetu. Mimi nashuhudia kwamba kila wakati wa sala ya thamani unaweza kuwa muda mtakatifu tukiwa pamoja na Baba, katika jina la Yesu Kristo, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Katika jina takatifu la Yesu Kristo, amina.