Maandiko Matakatifu
Ukurasa wa Jina wa Kitabu cha Mormoni


Kitabu cha Mormoni

Historia Iliyoandikwa kwa
Mkono wa Mormoni
kwenye Mabamba
Yaliyochukuliwa kutoka katika Mabamba ya Nefi

Kwa hivyo, huu ni ufupisho wa maandishi ya watu wa Nefi, na pia ya Walamani—Ulioandikiwa Walamani, ambao ni baki la nyumba ya Israeli; na pia kwa Myahudi na kwa Myunani—Uliandikwa kutokana na amri, na pia kwa roho ya unabii na ufunuo—Uliandikwa na kufungwa, na kufichwa katika Bwana, ili usiharibiwe—Upate kutolewa kwa karama na uwezo wa Mungu na hata utafsiri wake—Ulifungwa kwa mkono wa Moroni, na kufichwa katika Bwana, ili uje utolewe wakati wa kufaa kupitia Myunani—Na kutafsiriwa kwa karama ya Mungu.

Na pia ufupisho kutoka kitabu cha Etheri, ambao ni maandishi kuhusu watu wa Yaredi, ambao walitawanyishwa wakati Bwana alipochanganya lugha za watu, walipokuwa wakijenga mnara ili wafike mbinguni—Ambao ni kuonyesha baki la nyumba ya Israeli vitu vikubwa ambavyo Bwana aliwatendea baba zao; na ili wajue maagano ya Bwana, kuwa hawakutupiliwa mbali milele—Na pia kuwathibitishia Myahudi na Myunani kwamba Yesu ndiye Kristo, Mungu wa Milele, anayejidhihirisha kwa mataifa yote—Na sasa, kama kuna makosa ni mapungufu ya wanadamu; kwa hivyo, usilaumu vitu vya Mungu, ili usipatikane na doa kwenye kiti cha hukumu cha Kristo.

Tafsiri asili ya Kiingereza kutoka kwENYE MAbamba
na Joseph Smith, Mdogo