2010
Jaribio langu la Imani
Aprili 2010


ujana

Jaribio langu la Imani

Wakati nilikuwa na umri wa 13, nilianza kusoma Kitabu cha Mormoni kila siku, na nimebarikiwa kila siku tangu wakati huo.

Darasa letu la shule ya Jumapili la wenye umri wa 13 halikujulikana kwa utulivu. Ingawaje, tulikuwa na mwalimu mwema aliyejaribu awezavyo kutufundisha kila somo kwa Roho. Mojawapo wa somo kama hilo ilikuwa ni kusoma maandiko.

Mwishoni wa somo alitupatia changamoto. Ilikusudiwa kwa sisi sote, lakini kwa sababu nyengine alinitazama mimi alivyosema, “Nakupa changamoto kusoma kutoka kwa Kitabu cha Mormoni kila siku!” Nilifikiria mwenyewe, “Nitakuonyesha. Nitafanya hivyo!”

Nilianza 1 Nefi mlango wa 1 usiku huo huo na nikaendelea kusoma kila siku. Pengine sikuwa na mtazamo sahihi nilipoanza, lakini baada ya muda nilianza kupenda jinsi kusoma Kitabu cha Mormoni kulinifanya kuhisi. Kusoma kila usiku kukawa tabia ya kufurahisha.

Miezi baadaye nilifikia kwa Alma 32 na nilivutiwa na wazo la jaribio la imani. Shuleni tulikuwa tumesoma kuhusu kufanya majaribio ya kisayansi, basi nilipiga magoti chini na kumwambia Baba wa Mbinguni kwamba nilikuwa naanza jaribio. Niliuliza kwamba ningekuja kujua ikiwa Kitabu cha Mormoni kilikuwa cha kweli.

Kwa utambuzi, Najua kwamba Baba wa Mbinguni alijibu maombi yangu mara nyingi. Kusoma kila siku kutoka kwa Kitabu cha Mormoni kulinipatia uwezo mwingi wa kushinda uovu. Nilihisi kuwa karibu na Baba yangu wa Mbinguni. Nilihisi kuimarishwa na nguvu ya Roho Mtakatifu ili kushinda vizuizi. Kile Alma alichosema kuhusu kufanya jaribio na neno la Mungu ni kweli: “Linaanza kukua ndani ya nafsi yangu; ndio, linaanza kuangaza kuelewa kwangu, ndio, linaanza kunipendeza mimi” (Alma 32:28).