2010
Mafundisho ya Wakati Wetu
Novemba 2010


Mafundisho ya Wakati Wetu

Mafundisho ya jumapili ya nne ya Ukuhani wa Melkizedeki na Muungano wa Usaidizi wa kina Mama yatatengwa kwa “Mafundisho ya Wakati Wetu.” Kila fundisho linaweza kutayarishwa kutoka kwa hotuba moja au zaidi za Mkutano Mkuu wa hivi karibuni. Marais wa Vigingi na wilaya wanaweza kuchagua hotuba zitakazotumiwa, au wanaweza kuwapa majukumu maaskofu na marais wa matawi. Viongozi wanafaa kusisitiza umuhimu wa ndugu za Ukuhani wa Melkizediki na akina dada wa Muungano wa Usaidizi wa Kina Mama kusoma hotuba hizo katika jumapili hizo.

Wale wanaohudhuria mafundisho ya jumapili ya nne wanahimizwa kusoma na kuleta mafundishoni nakala za majarida ya Mkutano Mkuu.

Mapendekezo ya Kutayarisha funzo

Omba kwamba Roho Mtakatifu awe nawe unaposoma na kufundisha hotuba hizi Unaweza kushawishiwa kutayarisha mafundisho kwa kutumia vifaa vingine, lakini hotuba za mkutano mkuu ni mafundisho yaliyoidhinishwa. Jukumu lako ni kuwasaidia wengine kujifunza na kuishi kulingana na injili kama ilivyofundhishwa katika Mkutano Mkuu wa hivi karibuni.

Tafakari upya hotuba hizi, ukitafuta kanuni na mafundisho yanayolingana na mahitaji ya washiriki wa darasa. Pia, tafuta hadithi, marejeleo ya maandiko, na matamko kutoka kwa hotuba yatakayokusaidia kufundisha kweli hizi.

Tayarisha vidokezo vya jinsi ya kufundisha kanuni na mafundisho. Vidokezo vyako lazima vijumhishe maswali yatakayowasaidia washiriki wa darasa:

  • Tafuta kanuni na mafundisho katika hotuba.

  • Tafakari maana yake.

  • Shiriki mawazo, tajiriba, kuelewa na ushuhuda.

  • Tumia kanuni na mafundisho haya katika maisha yao.

Miezi

Vifaa vya Mafundisho ya Jumapili ya Nne

Novemba 2010—Aprili 2011

Hotuba zilichapishwa November 2010 Liahona*

Mei 2011—Oktoba 2011

Hotuba ilichapishwa Mei 2011 Liahona*