2010–2019
Makini dhidi ya Kawaida
Mkutano Mkuu wa Aprili 2019


Makini dhidi ya Kawaida

Wakati ushawishi wa ulimwengu unazidi sana kukumbatia uovu, lazima tujitahidi kwa bidii yote kubaki imara kwenye njia inayotuongoza salama kwa Mwokozi.

Niliwahi kuona alama ndani ya duka ambayo ilisema: “Furaha, Dola 15.00.” Nilikuwa mdadisi kujua kiasi gani cha furaha ningeweza kununua kwa Dola 15.00 hivyo niliingia ndani kuona. Nilichopata ilikuwa ni vipambo na hedaya za bei ndogo—hakuna hata kimoja nilichoona kingeweza kunipa aina ya furaha ambayo alama ilidokeza! Kwa miaka mingi, nimewaza mara nyingi kuhusu alama ile na jinsi inavyoweza kuwa rahisi kutafuta furaha katika vitu ambavyo ni vya bei ndogo au vya muda. Kama waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, tumebarikiwa kujua ni kwa jinsi gani na wapi furaha ya kweli hupatikana. Inapatikana katika kuishi injili kwa makini iliyoasisiwa na Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo, na katika kujitahidi kuwa zaidi kama Yeye.

Tuna rafiki mpendwa ambaye alikuwa mhandisi wa garimoshi. Siku moja wakati akiendesha garimoshi katika njia yake, aliona gari limesimama juu ya reli mbele yake. Haraka alitambua kwamba gari lilikuwa limekwama na halikuweza kuvuka reli. Kwa haraka aliliweka garimoshi katika hali ya tahadhari, ambayo ilihusisha breki kwenye kila kisanduku ambazo zilienea maili 3/4 nyuma ya injini, iliyobeba mzigo wa tani 6500 (tani mita 5,900). Hakukuwa na nafasi kwamba garimoshi lingeweza kusimama kabla ya kuligonga gari, na ililigonga. Bahati nzuri kwa waliokuwa ndani ya gari, walisikia onyo la king’ora cha garimoshi na walitoka kwenye gari kabla ya dhara. Wakati mhandisi alipozungumza na afisa mpelelezi wa polisi, mwanamke mwenye hasira aliwasogelea. Alifoka kwamba alikuwa ameona tukio zima na kushuhudia kwamba mhandisi hakujaribu hata kuchepuka nje ya njia ili kulikwepa gari!

Kwa kawaida, kama rafiki yetu mhandisi angeweza kuchepuka na kuacha reli ili kuepuka ajali, yeye na garimoshi lake lote wangepotea katika kuanguka na kusonga mbele kwa garimoshi kungefikia ukomo wa ghafla. Bahati nzuri kwake, vyuma vya reli ambapo garimoshi yake ilipita vilifanya magurudumu ya garimoshi kusogea kuelekea mwisho wa safari yake licha ya kikwazo katika njia yake. Bahati nzuri kwetu, sisi pia tuko kwenye reli, njia ya agano tuliyojiweka wakati tulipobatizwa kama waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Ijapokuwa tutakumbana na vikwazo mara kwa mara kwenye njia, njia hii itatusogeza mbele kuelekea tuzo yetu ya ukomo wa milele kama tutabaki imara kwayo.

Picha
Ono la Lehi la mti wa uzima

Ono la mti wa uzima linatuonyesha jinsi matokeo ya kuwa wa kawaida yanavyoweza kutuongoza mbali kutoka kwenye njia ya agano. Kumbuka kwamba fimbo ya chuma na njia nyembamba iliyosonga, au njia ya agano, iliongoza moja kwa moja kwenye mti wa uzima, ambapo baraka zote zinazotolewa na Mwokozi wetu na Upatanisho Wake zinapatikana kwa waaminifu. Pia ulioonekana katika ono ulikuwa ni mto wa maji ukiwakilisha uchafu wa ulimwengu. Maandiko yanaeleza kwamba mto huu “ulitiririka kando” ya njia na bado ulipita tu “kando ya mti, siyo kwenye mti. Ulimwengu umejaa fadhaa ambazo zinaweza kuwahadaa hata wateule, zikiwafanya kuwa wa kawaida katika kuishi maagano yao—hivyo zikiwaongoza karibu na mti, na siyo kwenye mti. Kama hatuko makini katika kuishi maagano yetu kwa usahihi, juhudi zetu za kawaida zinaweza hatimaye kutuongoza kwenye njia zilizokataliwa au kujiunga na wale ambao tayari wameingia jengo kubwa na pana. Pasipo umakini, tunaweza hata kuzama katika vilindi vya mto wa maji machafu.1

Kuna njia makini na njia ya kawaida ya kufanya kila jambo, ikijumuisha kuishi injili. Tunapotafakari kujitolea kwetu kwa Mwokozi, je tuko makini au kawaida? Kwa sababu ya asili yetu ya kufa, je wakati mwingine hatuhalalishi matendo yetu, wakati mwingine kurejelea matendo yetu kama ni kuwa uzeeni, au kuchanganya mema na jambo ambalo si jema sana? Wakati wowote tunaposema, “hata hivyo,” “isipokuwa,” au “lakini” pale inapohusiana na kufuata ushauri wa viongozi wetu manabii au kuishi injili kwa makini, kwa kweli tunasema, “Ushauri huo hauhusiki kwangu.” Tunaweza kuhalalisha vyovyote tunavyotaka, lakini ukweli ni kwamba, hakuna njia sahihi ya kufanya jambo baya!

Dhamira ya vijana kwa 2019 imechukuliwa kutoka Yohana 14:15, ambapo Bwana anaelekeza: “Mkinipenda, mtazishika amri zangu.” Kama tunampenda jinsi tunavyosema, je, tunaweza kuonesha upendo huo kwa kuwa kidogo zaidi makini katika kuishi amri Zake?

Kuwa makini katika kuishi injili siyo lazima imaanishe kuwa rasmi au kununa sana. Kile inachomaanisha ni kuwa sahihi katika mawazo na tabia kama wafuasi wa Yesu Kristo. Tunapotafakari tofauti kati ya makini na kawaida katika kuishi kwetu injili, haya ni baadhi ya mawazo ya kuzingatia:

Je tuko makini katika kuabudu kwetu siku ya Sabato na katika maandalizi yetu ya kupokea sakramenti kila wiki?

Je tungeweza kuwa makini zaidi katika sala zetu na usomaji wa maandiko au kujihusisha zaidi katika Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia?

Je tuko makini katika kuabudu kwetu hekaluni, na je kwa umakini na kwa kudhamiria tunaishi maagano tuliyofanya kwenye ubatizo na hekaluni? Je tuko makini katika muonekano wetu na nadhifu katika kuvaa kwetu, hasa mahali na katika mambo matakatifu? Je tuko makini jinsi tunavyovaa mavazi matakatifu ya hekaluni? Au mitindo ya ulimwengu inaamuru mtazamo wa kawaida zaidi?

Je tuko makini kwenye jinsi tunavyowahudumia wengine na kwenye jinsi tunavyotimiza miito yetu Kanisani, au je ni wasiojali au wa kawaida katika wito wetu wa kutumikia?

Je tuko makini au kawaida kwenye kile tunachosoma na kile tunachotazama kwenye TV na kwenye simu zetu? Je tuko makini kwenye lugha yetu? Au kwa kawaida tunakumbatia ukatili na ukosefu wa adabu?

Kijitabu cha Kwa Nguvu ya Vijana kina viwango ambavyo, vikifuatwa kwa makini, vitaleta baraka tele na kutusaidia kubaki kwenye njia ya agano. Japokuwa kiliandikwa kwa manufaa ya vijana, viwango vyake haviishi muda wa matumizi pale tunapoacha programu za Wavulana na Wasichana. Vinahusika kwa kila mmoja wetu, wakati wote. Kurejea viwango hivi kunaweza kuchochea njia zingine za tunavyoweza kuwa makini zaidi katika kuishi injili.

Hatushushi viwango vyetu ili tufae au kumfanya mtu mwingine ahisi vizuri. Sisi ni wafuasi wa Yesu Kristo, na hivyo tunawaweka juu wengine, tukiwainua mahali pa juu, patakatifu ambapo wao pia wanaweza kuvuna baraka kuu.

Ninawaalika kila mmoja wetu kutafuta mwongozo wa Roho Mtakatifu ili kujua marekebisho yapi tunahitaji kufanya katika maisha yetu ili tuwe kwa umakini tumeunganishwa na maagano yetu. Pia ninawasihi msiwe wakosoaji kwa wengine wanaofanya safari kama hii. “Hukumu ni yangu, asema Bwana.”2 Sote tupo kwenye mchakato wa kukua na kubadilika.

Hadithi iliyosimuliwa katika Kitabu cha Mormoni kuhusu waamlisi walioasi kwangu ni ya kuvutia. Kama njia ya kuwakumbusha wengine kwamba hawakuwa tena na muunganiko na Yesu Kristo na Kanisa Lake, waliweka alama ya wazi nyekundu kwenye paji za nyuso zao kwa ajili ya wote kuona.3 Katika njia tofauti, na kama wafuasi wa Yesu Kristo, je tunajiwekea alama gani? Je wengine wanaweza kuona kwa urahisi taswira Yake katika nyuso zetu na kujua nani tunamwakilisha kwa jinsi kwa umakini tunavyoishi maisha yetu?

Kama watu wa agano, hatupaswi kuwa kama walimwengu wengine. Tumepewa jina la “mzao mteule”4—sifa kuu iliyoje! Wakati ushawishi wa ulimwengu unazidi sana kukumbatia uovu, lazima tujitahidi kwa bidii yote kubaki imara kwenye njia inayotuongoza salama kwa Mwokozi, tukiongeza umbali kati ya kuishi kwetu maagano na ushawishi wa ulimwengu.

Ninapotafakari juu ya kupata furaha ya kudumu, ninagundua kwamba wakati mwingine tunajikuta uzeeni. Ukungu wa giza hauzuiliki tunaposafiri kwenye njia ya agano. Majaribu na ukawaida vinaweza kutufanya kuacha njia bila kutambua kuelekea kwenye giza la ulimwengu na mbali na njia ya agano. Kwa wakati ambapo hili linaweza kutokea, nabii wetu mpendwa, Rais Russell M. Nelson, ametusihi kurudi kwenye njia ya agano, na kufanya hivyo haraka. Nina shukrani kubwa kwa ajili ya zawadi ya toba na kwa nguvu ya Upatanisho wa Mwokozi wetu.

Haiwezekani kuishi maisha makamilifu. Ni mtu mmoja tu aliyeweza kuishi kikamilifu wakati akiishi katika sayari hii ya telestia. Huyo alikuwa ni Yesu Kristo. Ijapokuwa tunaweza tusiwe wakamilifu, akina kaka na akina dada, tunaweza kuwa wastahili: wastahili kupokea sakramenti, wastahili wa baraka za hekaluni, na wastahili kupokea ufunuo binafsi.

Mfalme Benyamini alishuhudia juu ya baraka na furaha ambayo huja kwa wale ambao kwa makini humfuata Mwokozi: “Na zaidi, ningetamani mtafakari juu ya hali ya baraka na yenye furaha ya wale wanaotii amri za Mungu. Kwani tazama, wanabarikiwa katika vitu vyote, vya muda na vya kiroho; na kama watavumilia kwa uaminifu hadi mwisho watapokewa mbinguni, kwamba hapo waishi na Mungu katika hali ya furaha isiyo na mwisho.”5

Je furaha inaweza kununuliwa kwa Dola 15? Hapana, haiwezi. Furaha ya kudumu na ya kina huja kwa kudhamiria na kwa umakini kuishi injili ya Yesu Kristo. Katika Jina la Yesu Kristo, amina.