2012
Maombi na Amani
Oktoba 2012


Vijana

Maombi na Amani

Jioni moja nilibishana na mama yangu na nikahisi vibaya sana. Kwa hivyo niliamua niombe. Ingawa nilikuwa katika nilijisikia vibaya na sikutaka kusikia “kiroho.” Nilijua kuomba kungenisaidia mimi kusikia furaha na kutokuwa na ubishi tena. Baada ya mama yangu kutoka chumbani, nilianza maombi yangu. “Baba wa Mbinguni mpendwa, naja mbele Zako jioni hii kwa sababu …” Hapana. Nikafungua macho yangu na kukujua mikono yangu, hivyo vilisikika kuwa vigumu. Nikajaribu tena. “Baba wa Mbinguni, nahitaji …” Hivyo pia kukasikika kuwa kigeni. Nilihisi Shetani akinishwawishi niache maombi yangu ya kumuomba Baba wa Mbinguni usaidizi.

Ghafula nikapata msukumo wa kutoa shukrani! Kwa hivyo nikafanya hivyo, na mawazo yakaanza kutiririka kutoka akilini mwangu mambo yote ambayo ningeweza kumshukuru Baba aliye Mbinguni. Nilipomaliza kunshukuru, nilizungumza juu ya shida iliyokuwepo.

Baadaye nilihisi amani ya ajabu ndani yangu, hisia ororo ya kiroho kwamba najua Baba yetu wa Mbinguni na wazazi wangu wananipenda na kwamba mimi ni mtoto wa Mungu. Niliweza kumuomba mama yangu radhi na nikakubali kuomba radhi kwake.