2022
Shiriki Nuru
Februari 2022


NJIA YANGU YA AGANO

Shiriki Nuru

Acha tuwe majasiri katika kushiriki injili kwa familia zetu.

Kuwa jasiri! Ni mara nyingi kiasi gani tunasoma maneno haya kwenye maandiko yakihusiana na kushuhudia injili, kuchagua mema, kusimamia kweli, kufanya matendo ya ukarimu na kuwatumikia wengine? Je, tu majasiri katika kushiriki nuru? Je, tunasita kuishiriki na familia zetu kwa hofu ya kukataliwa?

Unakumbuka ono la Lehi la mti wa uzima? “Na nilipokula tunda lile lilijaza nafsi yangu na shangwe tele; kwa hivyo, nikaanza kutaka jamii yangu na wao pia wale; kwani nilijua kwamba lilikuwa tunda la kupendeza zaidi ya yote.”1 Pale tu alipogundua jinsi mpango wa wokovu ulivyokuwa wa thamani, mara moja alitaka kuushiriki—na hakuogopa kuwa jasiri. Alijua Lamani na Lemweli mara zote hawakuwa wapokeaji lakini kwa sababu ya upendo wake mkuu kwao, aliamua tu kushiriki.

Kama mwanafunzi kijana wa chuo, miaka hamsini iliyopita, rafiki yangu muumini alikuwa jasiri. Aliniuliza moja kwa moja ‘swali la dhahabu’: “Unafahamu nini kuhusu Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho? Je, ungependa kufahamu zaidi?” Nilipojifunza, kuelewa na kupata ushuhuda wa injili, nilitaka kuushiriki na familia yangu—ingawa nilijua kwamba wengi wao wasingekuwa wapokeaji. Na hakika, hawakupokea! Lakini hamu yangu ya kuwa jasiri inabaki kuwa imara. Mara zote ninafikiria jinsi ninavyoweza kwa ujasiri lakini kwa upole kuwaalika waje kwa Kristo.

Pengine tunaweza kuzingatia mapendekezo haya:

Maneno na matendo yetu huakisi vile tulivyo. “Kuwa mpole na mwenye upendo katika matendo na mawazo; Kwani haya ndiyo mambo Yesu aliyofundisha.”2

Onesha upendo, usaidizi na ujasiri kwa kila mwanafamilia wakati wanapopitia shangwe na changamoto. Kwa upole onesha upendo wa Bwana pale tunapouona na tuwasaidie wautambue.

Kuwa mfano mzuri katika sala na kujifunza maandiko. Shiriki mawazo mazuri na misukumo tuliyonayo kadiri inapohusu uhusiano na uzoefu katika familia zetu.

Watumikie kwa upendo na shangwe. Na wakati wanapotuuliza, “Kwa nini unakuwa muelewa sana na mwenye kusaidia sana?” Tunaweza kusema kwa dhati, “Tunajitahidi kuwa zaidi kama Kristo na kufuata mfano Wake.”

Na swali la injili linapokuja, hebu tusiogope kushiriki kanuni hizo na kuwaalika waje kwa Kristo.

Hebu tufuate mfano wa Lehi: kwa shukrani, upendo na shangwe hebu sote “Tuwe majasiri!” Kuna fursa nyingi kila siku za kushiriki nuru. Hebu tusikose hata moja ya hizo!

Muhtasari

  1. 1 Nefi 8:12.

  2. “Ninajaribu Kuwa kama Yesu” 1980, Janic Kapp Perry.