2015
Badiliko Langu la Moyo
Februari 2015


Vijana

Badiliko Langu la Moyo

Mwandishi anaishi Fortaleza, Brazil.

Nilipojifunza kwa mara ya kwanza kuhusu injili rejesho ya Yesu Kristo, nilihisi Roho akishuhudia ukweli wake. Kupitia maombi, ushuhuda wangu ulikuwa thabiti zaidi, na niliamua kubatizwa.

Punde baada ya ubatizo wangu, watu katika kata yangu walianza kuniuliza jinsi gani nilihisi kuhusu kuhudumu misheni. Kwa kweli, sikujua hakika kile cha kusema. Wazo la kuacha familia yangu na shule ili kuhudumu misheni lilionekana upuuzi.

Kisha siku moja nilianza kufikiria kuhusu uongofu wangu. Niliwakumbuka wamisionari ambao walikuwa wamenifundisha, ambao kwa uvumilivu walikuwa wamejibu maswali yangu na kunisaidia kuelewa injili. Nilitambua kwamba bila usaidizi wao, singaliwahi kugundua Kanisa la kweli. Punde nilipobainisha hayo, nia ya kuhudumu ilikuwa katika moyo yangu. Ningemsikia Roho akiniambia kwamba nilipaswa nihudumu katika misheni ya muda.

Ninajua kwamba kazi ya umisionari ni kazi ya Baba yetu wa Mbinguni na kwamba tunaweza kusaidia kuleta watu katika ufahamu mzuri wa injili rejesho.