2010–2019
Je, Mimi ni Mzuri vya Kutosha? Nitaweza Kweli?
Oktoba 2016


Je, Mimi ni Mzuri vya Kutosha? Nitaweza Kweli?

Kama utajaribu hasa sana na hautarazini au hutaasi—ukitubu kila mara na kuomba neema—hakika utakuwa “mzuri vya kutosha.”

Wapendwa kina dada na kaka, ni baraka kiasi gani kwetu kukusanyika ili kufundishwa na watumishi wa Bwana. Je, ni vizuri jinsi gani kwa njia nyingi Baba yetu wa Mbinguni anavyotuongoza na kutubariki sisi? Hakika Yeye anatutaka tuje nyumbani.

Kupitia mfululizo wa rehema mwororo kama daktari kijana nipohitimu shule ya udaktari, nilikubaliwa kwenye mafunzo ya udaktari wa watoto mpango wa nguvu sana, unaoshindaniwa sana. Nilipokutana na madaktari wakufunzi wengine, nilihisi kama mwenye akili kidogo na ambaye sikujiandaa kati ya hawa wote. Nilifikiri hapakuwa na njia ya kuweza kufikia kiwango cha wana kikundi.

Mwanzoni mwa mwaka wetu wa tatu, nilikuwa nimekaa kwenye eneo la nesi hospitali usiku mmoja, nikiwa natafakari mwenyewe na kusinzia nikiwa najaribu kuandika kadi ya mvulana mdogo aliyekuwa na kichomi. Sikuwa nimewahi kukatishwa tamaa kiasi hicho maishani mwangu. Sikuwa na uelewa wowote jinsi ya kutibu kichomi kwa mtoto wa miaka 10. Nilianza kujiuliza kile nilichokuwa nikifanya pale.

Mara moja wakati ule, mmoja wa wasimamizi aliweka mkono wake kwenye mabega yangu. Aliniuliza nilikuwa nafanya nini, na nikamwambia kuchanganyikiwa kwangu na hofu. Jibu lake lilibadilisha maisha yangu. Aliniambia jinsi yeye na wafanyakazi wengine walivyokuwa wanajivunia kwa ajili yangu na walihisi kama nitakuja kuwa daktari mahiri. Kwa kifupi, aliniamini wakati ambao sikuweza hata kujiamini mimi mwenyewe.

Kama uzoefu wangu mwenyewe, mara nyingi waumini wetu wanauliza “Je, mimi ni tu mzuri vya kutosha?” au “Je, kweli nitaweza kufika kwenye ufalme wa selestia?” Bila shaka, hakuna kitu kama vile “kuwa mzuri vya kutosha.” Hakuna kati yetu ambaye angeweza “kupata” au “kustahili” wokovu wetu, lakini ni kawaida kushangaa kama tunakubalika mbele za Bwana, hivi ndivyo ninavyoelewa maswali haya.

Wakati mwingine tunapohudhuria kanisani, tunakatishwa tamaa hata kwa mwaliko wa kujirekebisha. Tunafikiria kimya kimya, “Siwezi kufanya vitu hivi vyote” au “Siwezi kuwa mzuri kama watu hawa wote.” Huenda tunajisikia hivyo hivyo kama nilivyojisikia hospitalini siku ile.

Tafadhali, wapendwa kaka na dada zangu, lazima tuache kujilinganisha na wengine. Tunajitesa wenyewe bila haja kwa kushindana na kujifananisha. Kimakosa tunauhukumu wema wetu kwa vitu tunavyovifanya au tusivyo kuwa navyo na kwa maoni ya wengine. Kama ni lazima kujilinganisha, acheni tujilinganishe tulivyokuwa awali dhidi ya leo—na jinsi tunavyotaka kuwa hapo baadaye. Mawazo yetu pekee yenye umuhimu ni vile Baba yetu wa Mbinguni anavyofikiria kutuhusu sisi. Tafadhali muuliza Yeye kwa dhati kile Yeye anafikiria kukuhusu wewe. Atatupenda na atatusahihisha lakini kamwe hawezi kutuvunja moyo, huo ni ujanja wa Shetani.

Acha mimi niwe mkweli na muwazi. Majibu ya maswali “Mimi ni Mzuri vya Kutosha?” na “Nitaweza Kweli?” ni “Ndiyo! Wewe utakuwa mzuri wa kutosha” na “Ndiyo, utaweza iwapo tu utaendelea kutubu na usirazini au kuasi. Mungu wa mbinguni siyo refa hasiye na huruma akitafuta kosa lolote la kutuondoa toka kwenye mchezo. Yeye ni Baba yetu mkamilifu mwenye upendo, anayesikiliza zaidi kuliko kitu chochote ili kuwafanya watoto Wake warudi nyumbani na kuishi Naye kama familia milele. Hakika alimtoa Mwanae wa Pekee ili tusiangamie bali kuwa na uzima wa milele!1 Tafadhali amini, na tafadhali kuwa na matumaini na ufariji kutoka kwa, huu ukweli wa milele. Baba yetu wa Mbinguni anatarajia sisi kufanya hivyo! Hiyo ndiyo kazi Yake na utukufu Wake.2

Ninapenda jinsi Rais Gordon B. Hinckley alivyokuwa akifundisha kanuni hii. Nilimsikia akisema katika nyakati kadhaa, “Akina kaka na dada, anayoyatarajia Bwana kutoka kwetu ni kujaribu, lakini unatakiwa kujaribu kweli!”3

“Kujaribu kweli” kuna maana kutenda kadiri ya uwezo wetu, kutambua pale tunapohitaji kuimarika, na kisha kujaribu tena. Kwa kurudia kufanya hivi, tunakuwa karibu zaidi na Bwana; tunahisi Roho Wake zaidi na zaidi;4 na tunapokea neema Yake, na msaada Wake.5

Wakati mwingine, nafikiri, hatutambui ni jinsi gani Bwana anataka kutusaidia. Ninayapenda maneno ya Mzee David A. Bednar, aliyesema:

“Wengi wetu tunaelewa vizuri kwamba Upatanisho ni kwa ajili ya wenye dhambi. Sina uhakika, hata hivyo, kwamba tunajua na kuelewa kwamba Upatanisho pia ni kwa ajili ya watakatifu. …

“… Upatanisho unaleta msaada kwetu wa kushinda na kuepuka mabaya na kutenda na kuwa wazuri. …

“‘… Ni … kwa neema ya Bwana kwamba watu binafsi … hupata nguvu na kusaidia kutenda kazi nzuri ambazo uenda wasingeweza [kuzifanya]. … Neema hii ni uwezo unaowezesha …’ [Kamusi ya Biblia, “Neema”; mkazo umeongezewa]… au msaada wa mbinguni kila mmoja wetu huhitaji sana ili kufuzu kwa ajili ya ufalme wa selestia.”6

Tunachotakiwa kufanya ili kupata msaada huu wa mbinguni ni kuuomba na kisha kutenda juu ya msukumo wa haki tuanopokea.

Habari njema ni kwamba kama tumetubu kwa dhati, dhambi zetu za awali hazitatufanya tushindwe kutukuka. Moroni anatusimulia kuhusu watenda dhambi katika siku zake. Lakini mara walipotubu na kuomba msamaha, kwa kusudi halisi, walisamehewa.7

Na Bwana Mwenyewe alisema kuhusu mtenda dhambi:

“Kama ataungama dhambi zake mbele yako na mimi, na atubu kwa moyo wake kwa kweli, utamsamehe, na pia nitamsamehe.

“Ndio, na kila mara watu wangu watatubu nitawasamehe makosa yao dhidi yangu.”8

Kama tutatubu kwa dhati, hakika Mungu atatusamehe, hata kama tumetenda dhambi hiyo tena na tena. Kama vile Mzee Jeffrey R. Holland alivyosema: “Hata hivyo ikawa umekosea mara ngapi, hata makosa mangapi unaweza kuhisi umetenda … , nashuhudia kwamba unaweza kuwa haujasafiri mbali kupita uwezo wa kufikia wa upendo wa Mungu. Haiwezekani wewe kuzama chini zaidi ya kule nuru isiyokoma ya Upatanisho wa Kristo inang’aa.”9

Hii haimaanishi kwa namna yoyote ile kwamba dhambi ni Sawa. Dhambi daima ina matokeo. Dhambi wakati wote huleta madhara na inaumiza wote mtenda dhambi na wale waliodhurika na dhambi zake. Na toba ya kweli haijawa rahisi.10 Hata hivyo, tafadhali elewa kwamba ijapokuwa Mungu huondoa hatia na madoa ya dhambi pale tunapotubu kwa dhati. Huenda asiondoe mara moja matokeo ya dhambi zetu. Wakati mwingine hubaki nasi katika maisha yetu yote. Na aina mbaya zaidi ya dhambi iliyopangwa ambapo mtu anasema, “Mimi naweza kutenda dhambi sasa na kutubu baadaye.” Ninaamini kwamba hii ni kejeli makini ya dhabihu na mateso ya Yesu Kristo.

Bwana mwenyewe alisema, “Kwani mimi Bwana siwezi kuiangalia dhambi na kuivumilia hata kidogo.”11

Na Alma alitangaza, “Tazama, nakwambia, uovu haujapata kuwa furaha.”12

Mojawapo ya sababu ambayo kauli ya Alma ni kweli ni kwamba kuendelea kutenda dhambi, tunajiweka mbali wenyewe na Roho wa Bwana, tunakata tamaa, na kisha kuacha kutubu. Lakini narudia, kwa sababu ya Upatanisho wa Mwokozi, tunaweza kutubu na kusamehewa kabisa, iwapo tu toba yetu ni ya kweli.

Kile ambacho hatuwezi kufanya ni kurazini badala ya kutubu. Haitawezekana kujitetea wenyewe katika dhambi zetu kwa kusema, “Mungu anajua ni vigumu mno kwangu, hivyo ananikubali mimi kama nilivyo.” “Kujaribu kweli” kuna maana kuendelea kujitahidi hadi tutakapofikia kikamilifu kiwango cha Bwana, ambacho kimeelezwa vizuri katika maswali tunayoulizwa ili kupata kibali cha hekalu.

Kitu kingine ambacho kitatufanya tusiende mbinguni na kututenganisha na msaada tunaouhitaji sasa ni uasi. Kutoka katika kitabu cha Musa, tunajifunza kwamba Shetani alifukuzwa kutoka mbinguni kwa sababu ya uasi.13 Tunakuwa katika uasi kila wakati tunaposema katika mioyo yetu, “Simhitaji Mungu, na sihitaji kutubu.”

Kama daktari wa watoto wa wagonjwa mahutihuti, ninajua kwamba kama mtu isivyo sahihi akikataa tiba ya kuoka maisha, inaweza kupelekea kifo cha kimwili. Vilevile, tunapoasi dhidi ya Mungu, tunaukataa msaada na tumaini pekee, ambao ni Yesu Kristo, ambao hupelekea kifo cha kiroho. Hakuna kati yetu anayeweza kufanya haya kwa uwezo wake mwenyewe. Ukweli ni kwamba hakuna hata mmoja wetu atakaye kuwa “mzuri wa kutosha,” isipokuwa kwa ustahili na neema ya Yesu Kristo,14 lakini kwa sababu Mungu anauheshimu uhuru wetu, nasi pia hatuwezi kuokolewa bila ya kujaribu. Hivyo ndivyo mizani kati ya neema na vitendo hufanya kazi. Tunatumaini hili katika Kristo kwa sababu Yeye anataka kutusaidia na kutubadilisha. Hakika, tayari Yeye anatusaidia sisi. Tulia kidogo na tafakari na tambua msaada Wake katika maisha yako.

Ninashuhudia kwako kama utajaribu hasa sana na hautarazini au hutaasi—ukitubu kila mara na kuomba neema, au msaada, wa Kristo, hakika utakuwa “mzuri vya kutosha,” ambayo ni kupokelewa mbele za Bwana; utaweza kufika kwenye ufalme wa Mungu ukiwa mkamilifu kwa Kristo; na utapokea baraka na utukufu na furaha ambayo Mungu ameiweka kwa kila watoto Wake—wakiwemo hususani wewe na mimi. Mimi nashuhudia kwamba Mungu yu hai na anatutaka twende nyumbani. Mimi nahuhudia kwamba Yesu yu hai, Katika jina takatifu la Yesu Kristo, amina.