2010–2019
Mungu Atayafuta Machozi Yote
Oktoba 2016


Mungu Atayafuta Machozi Yote

Tunapofanya imani katika Meokozi, Yeye atatuinua na kutubeba kote katika majaribu yetu yote na, hatimaye, atatuokoa katika ufalme wa selestia.

Kama sehemu ya mpango Baba yetu wa Mbinguni, aliruhusu huzuni kufumwa katika uzoefu wetu wa maisha ya sasa.1 Wakati inaonekana kwamba majaribu ya machungu yanatujia kwa njia isiyo sawa, tunaweza kuhakikishiwa kwamba kufikia kiwango fulani au kingine sote tunateseka na kupambana. Ni maombi yangu kwamba Roho Mtakatifu atatuelekeza hadi kuelewa zaidi ni kwa nini hili lazima liwe hivyo.

Wakati tunapotazama matukio magumu ya maisha kupitia lenzi za imani katika Kristo, tunaweza kuona kwamba kunaweza kuwa na sababu ya kiungu katika kuteseka kwetu. Watakatifu wanaweza kuona ukweli wa ushauri wa Petro unaoonekana kujikinza. Aliandika “Kama unateseka kwa ajili ya haki, bahati yako,”2 Tunapojitolea “mioyo yenu[yetu] kwa ufahamu,”3 tunaweza kuongeza uwezo wetu kwa vyote kuvumilia majaribu yetu vizuri na kujifunza kutoka— na kutakaswa—nayo. Ufahamu kama huu unatoa majibu kwa swali hili la kudumu “Ni kwa nini mambo mabaya huwafanyikia watu wazuri?”

Kila mmoja anayesikiliza leo amepata kuona kwa kiasi fulani upweke, kukata tamaa, huzuni, au masikitiko. Bila lile  “jicho la imani”4 na uelewa wa ukweli wa milele, mara nyingi tunapata kwamba huzuni na mateso ambayo tunapitia katika maisha ya duniani yanaweza kutia giza ukweli kuzuia furaha ya milele ya kufahamu kwamba mpango mkuu wa Baba yetu wa Mbinguni kwa kweli ni mpango wa milele wa furaha. Hakuna njia nyingine ya kupokea  utimilifu wa furaha.5

Mungu anatualika kujibu kwa imani mateso yetu ya kipekee ili kwamba tuweze kuvuna baraka na kupokea ufahamu ambao hauwezi kupatikana kwa njia nyingine yeyote. Tumefundishwa kushika amri katika kila hali na mazingira kwani “yule aliye mwaminifu katika taabu, zawadi yake ni kubwa katika ufalme wa mbinguni.”6 Na tunaposoma katika maandiko, “Kama mna huzuni, mlinganeni Bwana Mungu wenu, kwa maombi ya dhati, ili mioyo yenu ipate kufurahi.”7

Mtume Paulo, binafsi sio mgeni kwa mateso, alipata kutoka uzoefu wake mwenyewe kufundisha kwa kina na uzuri taswira ya milele inayokuja tunapovumilia vizuri na kwa subira, Alisema, “Kwa mateso yetu mepesi, ambayo ni bali kwa muda mfupi tu, yanatufanyia kazi kwa mbali mno na uzito wa milele wa utukufu.”8 Kwa maneno mengine, tunajua katika mateso yetu kwamba Mungu ametoa zawadi ya milele ya kulipizia.

Uwezo wa Paulo wa kuzungumza juu ya majaribu, mateso, na huzuni ya maisha yake kama “mateso mepesi” yanatokana na ukali wa mateso yake, ambayo kwake yalimezwa na mtazamo wa milele. Imani  ya Paulo katika Yesu Kristo ilifanya vitu vyote kuvumilika. Alipigwa mara tano kwa mijeledi, mara tatu na fimbo, mara moja na mawe; mara tatu aliteseka na maangamizi ya meli baharini; mara nyingi alikuwa katika janga la kifo kwa kuzama, na wanyang’anyi, na hata na ndugu wa uongo, aliteseka na uchovu na maumivu, njaa na kiu, na alifungwa kwenye baridi na akiwa uchi.9

Wengi wetu tumemsihi Mungu aondoe chanzo cha mateso yetu, na wakati msaada tunaotafuta unakuwa haujafika, tumejaribiwa kufikiria kwamba hatumsikilizi Yeye. Ninashuhudia kwamba, hata katika nyakati hizo, anasikia sala zetu, ana sababu ya kuruhusu mateso yetu kuendelea,10 na atatusaidia kuvumilia.11

Katika kifungu cha moyoni na cha kutafakari, Paulo anatuelezea kuhusu “mwiba” usiojulikana mwilini mwake, ambao ulimsababisha uchungu mwingi na kumwelekeza mara tatu magotini mwake, akimsihi Bwana amuondolee. Katika kujibu sala za Paulo, Bwana hakuuondoa mwiba huo lakini alizungumza amani na kuelewa kwa moyo wake, akisema, “Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu.” Kwa kuelewa tofauti, Paulo aliweza kukubali na kuwa na shukrani kwa mwiba aliopewa. Alisema, “Basi … nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.”12

Tunapopata kuwezeshwa huku, taswira ya milele katika maisha yetu, uwezo wetu wa kuvumilia unakua, tunajifunza jinsi ya kuwasaidia wale wanaohitaji kusaidiwa,13 na tunapata kushukuru na hata kuonyesha shukrani13kwa ajili ya uzoefu Mungu anaoruhuru tuwe nao kama walimu katika njia ya uzima wa maisha.

Wakati tunajikuta tukifanya kazi kupitia dhiki, inaweza kuwa vigumu kuona majaribu yetu kama ishara kwenye njia zetu binafsi za ufuasi. Lakini, hata kama sisi wenyewe tunajikuta wakati mwingine katika bonde la giza la kukata tamaa au kwenye barabara ya juu ya furaha, kujifunza kutokana na kuona huruma kwa mateso ya wengine, kunaweza kuwa baraka.

Wakati wa mkutano mkuu wa hivi majuzi wa kigingi niliopangiwa na kuhudhuria huko Ufilipino, moyo wangu ulivunjika sana niliposikia juu ya uzoefu wa huzuni wa Kaka Daniel Apilado. Kaka Apilado na mke wake walibatizwa mwaka 1974. Walikumbatia injili ya urejesho na walifungwa katika hekalu. Baada ya hapo, walibarikiwa na watoto wazuri watano. Mnamo July 7, 1997, wakati Kaka Apilado akihudumu kama rais wa kigingi, moto ulitokea katika nyumba yao ndogo. Mwana mkubwa wa Kaka Apilado, Michael, alimwokoa baba yake, akamtoa nje kutoka kwenye jengo lililokuwa likiteketea, kisha akarudi ndani katika nyumba kuokoa wengine. Ilikuwa ni mara ya mwisho Kaka Apilado alimwona mwanawe mzima. Walioteketea na moto walikuwa mkewe,  Dominga na kila mmoja wa watoto wao watano.

Ukweli kwamba Kaka Apilado alikuwa anaishi maisha yanayompendeza Mungu wakati mkasa ulipotokea hakuuzuia mkasa wala haukumfanya asiweze kudhurika kutoka majonzi ambayo yalifuata Lakini uaminifu wake katika kuweka maagano yake na kuwa na imani yake katika Kristo kulimpa matumaini katika ahadi ya kwamba ataungana na mkewe na familia yake. Matumaini haya yalikuwa nanga kwa nafsi yake.14

Wakati wa ziara yangu, kaka Apilado, sasa baba mkuu katika kigingi, alinitambulisha kwa mke wake mpya, Simonette, na wana wao wawili, Raphael na Daniel. Kwa kweli, Yesu Kristo anaweza na atafanya hivyo “kuwafunga waliovunjika mioyo.”15

Katika kushiriki hadithi ya Kaka Apilado, ninahofia kwamba uzito wa kupoteza kwake unaweza kuwasababisha wengi kufikiri huzuni wao na mateso ni ya matokeo madogo katika kufananisha. Tafadhali msifananishe, lakini tafuteni kujifunza na kutumia kanuni za milele mnapopitia tanuru la mateso yenu binafsi.

Ikiwa naweza kuzungumza nanyi kibinafsi—“njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo”16—naweza nikapendekeza kwamba mapambano yenu ya kibinafsi—majonzi yenu ya kibinafsi, uchungu, dhiki, na unyonge wa kila aina—yote inajulikana kwake Baba yetu wa Mbinguni na Mwana Wake. Muwe na ujasiri! Muwe na imani! Na muamini katika ahadi za Mungu!

Lengo na kazi ya Yesu Kristo ilijumuisha kwamba “atabeba maumivu na magonjwa ya watu wake,” “atajichukulia unyonge wao,” na “kuwasaidia watu wake kulingana na unyonge wao.”17

Ili kupokea zawadi hizi Mwokozi anapeana bure kikamilifu, sisi wote ni lazima tujifunze kwamba mateso—kwa ajili ya na juu yake—hayatufundishi au hayatupi kitu chochote cha thamani isipokuwa kwa makusudi tujihusishe katika mchakato wa kujifunza kutokana na shida zetu kupitia kufanya imani.

Mzee Neal A. Maxwell alishiriki kile alichojifunza kuhusu mateso yenye maana katika maneno haya:

“Aina fulani ya mateso, yakivumiliwa vyema, yanaweza kwa kweli kuadilisha. …

“… Sehemu ya kuvumilia vyema ni kuwa mnyenyekevu vya kutosha, katikati mateso yetu, kujifunza kutoka kwa uzoefu wetu husika. Badala ya kwa urahisi kupitia mambo haya, sharti yapitie ndani yetu … katika njia ambazo zinatutakasa [sisi].”18

Nimeona katika maisha na mifano ya wengine kwamba kufanya imani ya nguvu na ya kudumu katika Yesu Kristo na ahadi zake huleta matumaini ya kweli ya mema ambayo yatakuja. Matumaini haya ya kweli yanatupa msimamo dhabiti na kuleta nguvu na uwezo tunaohitaji ili kuvumilia.19 Wakati tunaweza kuunganisha mateso yetu na hakikisho la lengo katika maisha ya duniani na hasa kwa zawadi inayotusubiri katika maeneo ya mbinguni, imani yetu katika Kristo inaongezeka na tunapokea faraja kwa nafsi zetu.

Kisha tunaweza kuona nuru mwisho wa upenyo. Mzee Jeffrey R. Holland amefundisha: “Kwa kweli kuna nuru mwisho wa upenyo. Ni Nuru ya Dunia, Nyota Inayong’aa ya Asubuhi, ‘nuru isiyo na mwisho, ambayo haiwezi kuwekwa giza’ [Mosia 16:9]. Ni Mwana wa Mungu Mwenyewe.”20

Tunaweza kuwa na nguvu katika kujua kwamba uzoefu wote mgumu katika maisha haya ni wa muda—hata usiku wa giza nene hupambazuka.

Wakati vyote vitakapomalizika na tumevumilia vitu vyote kwa imani katika Yesu Kristo, tunayo ahadi hii kwamba ”Mungu atafuta kila chozi katika macho [yetu].”21

Mimi nashuhudia kwamba Mungu Baba ywtu na Mwanawe, Yesu Kristo, wanaishi na kwamba Wao no waweka wa ahadi. Ninashuhudia kwamba Mwokozi anatualika sisi wote kuja kushiriki Upatanisho Wake. Tunapofanya imani yetu katika Yeye, atatuinua kutoka kwa majaribu yetu yote, hatimaye atatuokoa katika ufalme wa selestia. Nawaalikeni kuja kwake kwa Kristo, vumilieni vyema katika imani, na mkamilike ndani yake.na muwe na furaha kamili katika Yeye. Katika jina takatifu la Yesu Kristo, amina.