2022
Ninachagua Kumsikiliza Yeye
Machi 2022


“Ninachagua Kumsikiliza Yeye,” Liahona, Machi./Aprili 2022

Sauti za Watakatifu wa Siku za Mwisho: Wanawake wa Imani

Ninachagua Kumsikiliza Yeye

Wakati dada alipotaja keki kwenye ushuhuda wake, niliangalia juu na kuanza kuweka umakini.

Picha
seti ya funguo mezani, na mwanamke akiomba upande wa nyuma

Nilizaliwa Kanisani, kwa hivyo nilihudhuria shughuli za Msingi na vijana. Nilifurahia Msingi kwa sababu ya nyimbo na masomo yake.

Kama kijana, hata hivyo, nilianza kupoteza matamanio ya kuwa mwaminifu baada ya kuhamia kata mpya. Nilihudhuria shughuli za vijana kwa wiki nyingi, lakini nilijiweka kando na sikushiriki sana. Sikufurahia kanisa siku ya Jumapili, lakini nilihudhuria siku moja moja. Niligundua kuwa sikuwa nimeongoka kweli kwenye injili na mafundisho yake. Sikuwa na ushuhuda wa kwangu mwenyewe.

Kama kawaida wakati wa mkutano mmoja wa mfungo na ushuhuda, akili yangu ilitangatanga. Sikuwa nikisikiliza hasa wakati waumini wa kata wakitoa shuhuda zao, lakini nilisema amina mwishoni mwa kila mmoja. Kisha dada mmoja alipanda kwenye mimbari na kuanza kutoa ushuhuda wake. Alipotaja keki, niliangalia juu na kuanza kuweka umakini.

“Daima huwa ninazungumza na Baba wa Mbinguni, hata wakati ninapooka keki,” alisema. “Ninasema sala fupi kwamba keki iumuke na kutoka vizuri. Ninajua Yeye anajibu maombi yetu.”

Sikufikiria sana juu ya ushuhuda huo mpaka pale gari letu lilipoacha kuwaka wakati tulipohitaji kwenda dukani kununua chakula. Wakati huo nilikumbuka maneno ya yule dada. Kwa hivyo, nilirudi chumbani kwangu kuomba Mungu atusaidie ili gari liwake. Nilipiga magoti na kusali. Nilipomaliza, nilichukua funguo za gari na kuziweka mahali pake na kuwasha. Na kisha jibu la sala yangu lilikuja—sauti ya gari ikiwaka.

Kwa sababu ya jibu hilo kwa sala rahisi, niliondoka kutoka kwenye kukaribia kupoteza matamanio ya kuwa mwaminifu na kurejea kwenye njia ambayo imenisaidia kupata ushuhuda binafsi na kuwa mwongofu kamili kwenye injili. Maneno ya wimbo niupendao wa Msingi, “Ninahisi Upendo wa Mwokozi Wangu,” 1 yakawa zaidi ya maneno ya wimbo tu. Yakawa hisia ambazo ninazo kweli.

Ninaomba kuhusu kila kitu sasa. Na ingawa jibu au muda siyo daima kile ninachotamani, lakini bado ninachagua kumsikiliza Yeye wakati ninapokumbuka maneno ya Nefi: “Lakini tazama, ninawaambia kwamba lazima msali kila wakati, na msife moyo” (2 Nefi 32:9).

Muhtasari

  1. Ona “I Feel My Savior’s Love,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto,, 74–75.