2021
Kuweka Muziki katika Moyo wa Kuabudu
Machi 2021


Kuweka Muziki katika Moyo wa Kuabudu

Muziki daima umekuwa—na daima utakuwa—katika moyo wa kuabudu kanisani na nyumbani.

Picha
family gathered around piano

Si majuma mengi baada ya Kanisa kuanzishwa, Bwana alimwelekeza Emma Smith “kufanya uchaguzi wa nyimbo takatifu, … zenye kunipendeza Mimi, ili ziwepo katika kanisa langu” (Mafundisho na Maagano 25:11). Watakatifu walihitaji njia za kujifunza ukweli wa injili uliofunuliwa upya na kuunganika katika kumsifu Mungu. Na nyimbo za dini zingekuwa katika moyo wa kuabudu kwao na kujifunza.

Miaka iliyopita, wakati familia yangu ilipojiunga na Kanisa, wazazi wangu walitutia moyo tujifunze muziki wa imani yetu mpya. Nina baadhi ya kumbukumbu za wazi za wakati huo:

  • Kukariri “Prayer Is the Soul’s Sincere Desire” (Wimbo, no. 145) pamoja na familia yangu.

  • Kusikia “O My Father” (Wimbo, no. 292) na kujifunza kwamba nina Baba na Mama wa Mbinguni ambao ninaweza kuwaona tena siku moja.

  • Nikahisi upendo wa Mungu nikiimba “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29)—hata ingawa niliishi jangwani na kamwe nilikuwa sijaona mti wa lilaki!

Tukisonga mbele mkutano wa sakramenti wa Februari 2020. Waumini kadha wa kata yetu walikuwa wanapambana na saratani, na nilihisi faraja wakati kwaya ya kata ikiimba “How Firm a Foundation” (Nyimbo za Kanisa, no. 85). Majuma machache baadaye, misururu ya matukio mazito ilitokea: karantini, mikutano ya kanisa kufutwa, na misururu ya matetemeko na vishindo. Na huo wimbo ulianza kupigwa katika akili yangu tena.

Msiogope, kwani niko nanyi; ni Mungu wenu nitawasaidia. Nitawapa nguvu mpate simama,

Nitawashika na nitawashika na nitawashika na mkono wangu mkuu.

Wakati mwingine inaonekana kama changamoto za ulimwengu wote na za binafsi zinaendelea kukua karibu kila siku. Zaidi kuliko wakati wowote, tunahitaji chakula cha kiroho cha muziki mtakatifu, nyimbo za Msingi na muziki mwingine mtakatifu.

Hakuna Mabadiliko katika Kusudi au Umuhimu

Hata hivyo, tulipobadilisha kwenda kwenye ratiba ya saa mbili kwa ajili ya mikutano ya kanisa, baadhi walishangaa kama nafasi ya muziki itapungua katika kuabudu kwetu. Jibu ni hapana.

  1. Nyimbo takatifu bado ni sehemu ya kila mkutano wa sakramenti, ikijumuisha kusaidia kuandaa mioyo yetu kwa ajili ya ibada za sakramenti. Kuimba kwa kwaya na mkusanyiko na muziki mwingine mtakatifu kunaweza kupangwa ili kustawisha mkutano, kama vile awali. Wakati wa janga la COVID–19, muziki mtakatifu bado ulikuwa ni sehemu muhimu ya mikutano ya sakramenti iliyofupishwa, hata kama ni kwa vyombo pekee.

  2. Watoto hutumia nusu ya muda wao katika Msingi kujifundisha injili kupitia muziki.

  3. Katika saa ya pili, hakuna nyimbo za kufungua au kufunga kwa madarasa ya wazee na vijana. Lakini muziki bado unaweza kutumika katika madarasa ya kufundisha na kuinua.

  4. Ni rahisi kuliko hapo awali kusikiliza muziki mtakatifu kwenye vyombo vya kidijitali, ukitumia programu ya Muziki Mtakatifu wa Kanisa.

Maagizo Kidogo, Dhamira Zaidi

Bado, kutakuwa na kutokuelewana fulani. Jumapili moja ya Pasaka, mwalimu aliomba radhi darasa lake la Mafundisho ya Injili: “Mimi najua hatupaswi kuimba katika Shule ya Jumapili, lakini kwa kweli ningependa tuimbe ‘Najua Mkombozi Wangu Anaishi.’ Mwalimu huyo labda hayupo peke yake katika hii sintofahamu.

Kiuhalisia, muziki bado tu ni muhimu katika kuabudu kwetu kama vile ilivyokuwa. Shuhudia tukio muhimu la kutengeneza upya mkusanyiko wa nyimbo zetu na za watoto. Kama sehemu ya juhudi hizi, waumini wa Kanisa ulimwenguni kote waliwasilisha nyimbo za Kanisa, Nyimbo za Watoto na maandishi 16,000 mapya ya kupendeza.

Lakini tukiwa na muda mchache wa kuimba katika baadhi ya mikutano yetu ya Jumapili, tunahitaji kuwa makini sana na wenye lengo katika kupanga na kutumia muziki.

Picha
group of children singing

Kanuni mbili muhimu zinaweza kutusaidia kuweka muziki katika moyo wa kuabudu kwetu.

1. Muhimu kwa ajili ya Kufundisha

Tunaweza kufikiria juu ya hotuba na mazungumzo kama njia za msingi za kuwasilisha ujumbe wa injili nyumbani na kanisani. Na tunaweza kutumia muda wetu mwingi kwenye mambo haya. Lakini muziki si pambo la ziada. Ni moyo hasa wa ufundishaji wenye nguvu pamoja na Roho.

Kama Mtume Paulo alivyowashauri Watakatifu wa kale, “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu” (Wakolosai 3:16).

Muziki unaweza kumwalika Roho katika somo au mkutano kwa wakati huo huo. Kuchagua wimbo wa kuimba wakati wa darasa la Shule ya Jumapili au majadiliano ya Njoo, Unifuate inahitaji kufikiria kwa makini na kwa maombi kama vile tunavochagua fungu la kusoma au sehemu ya somo tunayoamua kushiriki. Muziki unaochaguliwa kwa maombi unaweza kugusa mioyo, ukiacha misukumo ya kiroho ambayo inadumu maisha yetu yote.

2. “Ni Maombi Kwangu”

Wakati fulani, yawezekana sisi sote kwa nyakati fulani tunajisikia kuvunjika moyo, wakati mwingine njia mbele yetu inakuwa na ukungu. Wakati mwingine inaonekana kwamba tunaendelea kutupa hitaji lile lile mbinguni, bila jibu au suluhisho. Wakati kama huo, inaweza kushawishika kuamua kwamba Mungu hajali au kwamba hatustahili utunzaji Wake. Wakati mwingine tunaweza kuhisi kuacha kuomba.

Kwa muda fulani tunapohisi ukosefu wa muunganiko wa kiroho na mbinguni, hapa kuna ukweli wa kufariji: Muziki mtakatifu unaweza hasa kuwa aina fulani ya maombi. Bwana Mwenyewe alielezea hili alipompatia kazi Emma kutengeneza kitabu cha kwanza cha nyimbo zetu za kidini: “Kwani nafsi yangu hufurahia katika nyimbo za moyoni; ndiyo, wimbo wa mwenye haki ni sala kwangu Mimi” (Mafundisho na Maagano 25:12.; mkazo umeongezwa).

Na tunapotoa wimbo wa dhati wa moyo wetu Kwake, Bwana aliahidi daima kujibu kwa baraka: “Nayo itajibiwa kwa baraka juu ya vichwa vyao. Kwa hiyo, inua moyo wako na ufurahie” (Mafundisho na Maagano 25:12–13).

Wakati mmoja mgumu katika maisha yangu, sikuweza kutambua majibu ya maombi ya moyo wangu kwa muda mrefu. Rafiki yangu mpendwa alikuwa anapitia nyakati zake ngumu yeye mwenyewe. Lakini tulipokuwa tunaomba na kuimba nyimbo za Kanisa na nyimbo za injili kwa pamoja, mara nyingi tulipata hisia za kuzidiwa za faraja na ushuhuda. Mimi sasa ninatambua kwamba Bwana alikuwa anatimiza ahadi Yake. Yeye alikuwa anajibu nyimbo za moyo wangu, tena na tena. Na hilo hasa lilisaidia kuinua moyo wangu na kusonga mbele.

Picha
young woman visiting a cemetery

Photograph by Robert Casey

Katika Jumapili Yoyote Ile

Katika Jumapili yoyote ile, tunaweza kuwa na hakika kwamba wengine katika mikusanyiko yetu, wengine katika madarasa yetu, na wengine katika familia zetu wako ndani ya matatizo makubwa ya mateso binafsi. Wengine watakuwa katika mabonde ya amani yenye kufurika baraka. Wengine bado watakuwa wanajifundisha ukweli wa kimsingi wa injili.

Tunapoweka muziki katika mahali sahihi katika moyo wetu wa kuabudu, tunaweza kuwasaidia wote kupata fursa za kuhisi Roho, kujifunza ukweli wa injili, na kumsifu Bwana kwa wema Wake. Na tunaweza kusaidia wote kuwa na nyimbo za mioyo yao kujibiwa katika njia ambazo tu Baba yetu wa milele, mwenye upendo anaweza kufanya.