2022
Anguko Lilikuwa Sehemu ya Mpango wa Mungu
Januari/Februari 2022


Misingi ya Injili

Anguko lilikuwa sehemu ya mpango wa Mungu

Kwa sababu ya Anguko, tunapata kuja duniani na tunaweza siku moja kurudi kuishi na Baba yetu wa Mbinguni.

Picha
Adam and Eve holding their infant child

Adamu na Hawa katika Bustani ya Edeni, na Robert T. Barrett; Adamu na Hawa Wanafukuzwa Kutoka Bustani ya Edeni, na Gary L. Kapp, haiwezi kunakiliwa; Adamu na Hawa, na Jay Bryant Ward; Ufufuo, na Harry Anderson

Katika Bustani ya Edeni, Mungu aliwaamuru Adamu na Hawa wasile tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Kisha Aliwaambia, “Wewe waweza kujichagulia mwenyewe, … lakini, kumbuka kwamba nimekataza” (Musa 3:17). Shetani alimjaribu Hawa kula tunda la mti. Alimwambia Hawa, “Mtakuwa kama miungu, mkijua mema na maovu” (Musa 4:11). Hawa alikula tunda na kisha kumshirikisha Adamu. Mungu aliwafukuza kutoka kwenye Bustani ya Edeni.

Anguko

Picha
Adam and Eve leaving the Garden of Eden

Wakati Adamu na Hawa walipoondoka kwenye Bustani ya Edeni, hawakuwa tena kwenye uwepo wa Mungu. Utengano huu kutoka kwa Mungu huitwa kifo cha kiroho. Kuondoka bustanini pia kulimaanisha Adamu na Hawa walikuwa wenye mwili wa kufa na hivyo waliweza kufa. Japokuwa Adamu na Hawa hawakuwa tena pamoja na Mungu na walikuwa sasa wenye miili ya kuweza kufa, walikuwa na furaha na wenye matumaini wakati walipoona kuwa wangeweza kuendelea (ona Musa 5:10–11). “Adamu alianguka ili wanadamu wawe; na wanadamu wapo, ili waweze kuwa na shangwe” (2 Nefi 2:25).

Wakati wa Majaribio

Wakati tunapozaliwa, tunaishi mbali na Mungu, kama vile Adamu na Hawa walivyofanya baada ya Anguko. Shetani hutujaribu ili tufanye chaguzi mbaya. Majaribu haya huturuhusu sisi kupimwa na kuchagua kati ya mema na mabaya (ona Alma 12:24). Kila mara tunapotenda dhambi na hatutubu, tunakuwa mbali sana kutoka kwa Baba wa Mbinguni. Lakini ikiwa tunatubu, tunakuwa karibu zaidi na Baba yetu wa Mbinguni.

Kifo cha Mwili

Dunia iliumbwa kwa ajili yetu (ona 1 Nefi 17:36). Anguko lilifanya iwezekane kwa Adamu na Hawa kutimiza amri ya Mungu ya kuwa na watoto, likiruhusu sisi tuje duniani katika mwili wa nyama na mifupa. Miili yetu siku moja itakufa, lakini roho zetu zitaendelea kuwa hai. Miili na roho zetu vitaungana tena wakati tutakapofufuka.

Kuokolewa na Yesu Kristo

Picha
The resurrected Jesus Christ appearing to Mary Magdalene at the empty tomb

Kupitia nguvu ya upatanisho ya Yesu Kristo, tunaweza kushinda kifo cha mwili na roho. Kwa sababu Kristo alifufuka, kila mmoja ambaye alizaliwa katika dunia hii atafufuka na kuishi milele. Na kwa sababu Kristo aliteseka kwa ajili ya dhambi zetu, tunaweza kutubu na kusamehewa ili kwamba tuweze kuishi tena na Baba yetu wa Mbinguni.