2022
Chagua kuwa Makini Kiroho
Septemba 2022


“Chagua Kuwa Makini Kiroho,” Liahona, Sept. 2022.

Chagua kuwa Makini Kiroho

Kuendeleza maendeleo yetu ya kiroho kwenye njia ya injili ni kama kuendesha baiskeli—vyote vinahitaji juhudi za bidii.

Picha
baiskeli

Vielelezo na Dilleen Marsh

Kushughulika na badiliko na ukijua kile cha kufanya katika nyakati za matatizo ni moja ya baraka zisizo za kawaida za kuwa muumini mwaminifu wa kanisa la Bwana. Kipawa cha Roho Mtakatifu ni upendeleo wa kupokea mwongozo na ushawishi endelevu na tunapobakia kuwa waaminifu.

Uzima, Amani, Mwongozo, na Ulinzi

Mtume Paulo Bwana alisema, “kuwa makini kiroho ni uzima na amani” (Warumi 8:6; ona pia mstari wa 5).

Kuchagua kuwa makini kiroho kwa kuishi maisha yenye kustahili ushawishi wa upole wa Roho Mtakatifu utatoa mwongozo katika maamuzi yako na ulinzi kutokana na hatari zote za kimwili na kiroho. Kupitia Roho Mtakatifu , wewe unaweza kupokea karama za Roho kwa faida yako na kwa faida ya wale uwapendao na kuwahudumia. Mawasiliano yake kwenda kwa roho yako yanabeba uhakikisho zaidi kuliko mawasiliano yo yote unayoweza kupokea kupitia njia zako za ufahamu za asili.

Unawezaje kuishi maisha ya kuwa makini kiroho na kupata mwongozo mwingi kutoka kwa Roho Mtakatifu?

1. Uwe msikivu kwa Baba yetu wa Mbinguni na Mwokozi.

Tunapokuwa katika muafaka na Baba wa Mbinguni, tunakuwa na wenzi wa Roho Mtakatifu. Tunapofanya mwafaka huu kuwa kipaumbele katika maisha yetu, tunajisogeza karibu na Yeye na Mwanawe, “Yesu Kristo, ambaye amemtuma kwetu” (Mafundisho na Maagano 132:24).

2. Mpende Mungu.

Kumpenda Baba yetu wa Mbinguni na kupalilia uhusiano na Yeye katika sala kutamweka Yeye katika mawazo na mioyo yetu.

Mtume Yohana, pamoja na ushuhuda wake juu ya upendo wa Mungu kwetu sisi na ushahidi wake binafsi juu ya Yesu Kristo, ulifutilia mbali imani potofu kwamba wokovu unaweza kupatikana kwa njia nyingine kuliko kupitia imani katika Yesu Kristo. Yohana aliwaalika wasomaji wake kuonja shangwe ya kuwa katika maelewano na Baba na Mwana (ona 1 Yohana 1:3). Yeye liongeza:

“Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, upendo wa Baba haumo ndani yake. …

“Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake: bali yeye afanyaye mapenzi ya Baba adumu hata milele” (1 Yohana 2:15, 17).

Katika maisha haya tunaweza kuona upendo wa Mungu kupitia wenza wa Roho Wake. Tunapofanya mapenzi ya Baba yetu wa Mbinguni na kujitahidi kubaki kwenye njia ya agano ambayo hutuongoza sisi kwenda Kwake, Roho Mtakatifu anaweza kutuongoza.1

3. Kumbuka kitu ambacho Mwokozi ametufanyia sisi.

Picha
mvulana akipitisha sakramenti

Baraka zilizoahidiwa katika sala zote za sakramenti ni “kwa wale [watakaopokea] waweze … kuwa na Roho Wake pamoja nao”(Mafundisho na Maagano 20:77). Tunapokea sakramenti kila wiki kwa sababu tunataka kuhifadhi na kukuza mambo yetu ya kiroho.

Rais Dallin H. Oaks, Mshauri wa Kwanza katika Urais wa Kwanza, amefundisha: “Tunapojiondoa mbali zaidi kutoka kwenye mambo ya ulimwengu, tunajisikia kuwa jirani zaidi na Baba wa Mbinguni na kuweza zaidi kuongozwa na Roho Wake. Tunaita ubora huu wa maisha kama hali ya kiroho.” Rais Oaks aliongeza: “Jinsi sisi tunavyo tafsiri uzoefu wetu pia kazi ya kiwango cha hali yetu ya kiroho. … Sisi tulio na ushuhuda juu ya injili ya Yesu Kristo tunapaswa kutafsiri matukio yetu kulingana na uelewa wetu juu ya makusudi ya maisha, misheni ya Mwokozi wetu na hatima ya milele ya watoto wa Mungu.”2

4. Tambua mambo ya kiroho.

Ninathibitisha kwamba hali ya kiroho ni baraka ya juhudi endelevu kwa upande wetu. Tunapotafuta kujifunza na kufuata ushawishi wa Roho, tunaweza kwa urahisi zaidi kutofautisha kati ya mambo ya Mungu kutoka kwenye mambo ya ulimwengu.

Mzee Quentin L. Cook wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alisema, “Kama tu marudio na juhudi endelevu vinavyohitajika ili kupata nguvu kimwili au uwezo wa kiakili, ndivyo ilivyo kweli katika mambo ya kiroho.”3

Kuza Hali Yako ya Kiroho

Shukrani kwa uonaji mbali wa viongozi wa Kanisa, tunazo zana nyingi bora za kutusaidia sisi katika kuimarisha hali zetu kiroho. Fikiria juu ya kuanzishwa kwa app ya Maktaba ya Injili ambayo inaruhusu nguvu ya maandiko na kujifunza injili kuwa ndani ya mfuko wako wakati wote. Fikiria kuhusu mabadiliko yanayohusiana na utumishi ambayo yanahimiza matumizi haya teknolojia tunapowafikia wengine. Fikiria mtazamo wa kujifunza Kanisa kitovu chake kuwa-nyumbani na kusaidiwa na-Kanisa na mtaala wa Njoo, Unifuate ambao unaweza kuinua hali zetu kiroho mahali po pote tulipo.

Hatuhitaji kuwa katika kizuizi cha kiroho tukiwa na nyenzo hizi zote zinazopatikana. Tunaweza kufanya kazi pamoja, tukichagua kila fursa ili kuwa makini kiroho, tukihimiza uzima na amani, na kwa makusudi tukifanya hali ya kiroho kuwa sehemu muhimu ya maisha yetu. Maandiko yanafundisha, “Tunda la Roho ni upendo, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, [na] kiasi” (Wagalatia 5:22–23).

Tengeneza na Kushika Malengo ya Kiroho

Mtu aliye makini kiroho anapenda kuimarisha hali yake ya kiroho na, anapoweka malengo, anajiuliza, “Je, malengo yangu ya kiroho yanatoa uangalifu wa kutosha kwenye mahitaji yangu ya kiroho?”

Mtu aliye makini kiroho anatafuta kujua jinsi ya kufuatilia misukumo ya kiroho na kisha anafanyia kazi misukumo hiyo Kwa hiyo, kuweka malengo kwa ajili ya makuzi ya kiroho ni muhimu.

Annie, mjukuu wetu wa kike mwenye umri wa miaka mitano, aliweka lengo la kujifunza kuendesha baiskeli. Alifanya mazoezi na kufanikiwa haraka sana, hivyo wazazi wake walimchukua na kwenda kuendesha baiskeli kifamilia naye akiendesha yake.

Wakati wakiendesha, mama yake Annie alielezea kustaajabu kwake jinsi Annie alivyoendesha vizuri sana kupanda kilima na kuvuka daraja. Annie alisimulia siri ya mafanikio yake: “Ninashikilia tu, mama, na kuendelea kupiga pedali.”

Ni sharti tufanye vivyo hivyo. Ni kwa kupiga pedali ndipo tunapoweza kutunza uwiano wa magurudumu ya baiskeli. Mambo rahisi, kama, sala ya kila siku, kujifunza maandiko, na kufuata ushauri wa kinabii hufanya hali yetu ya kiroho kusonga mbele licha ya vilima, majanga ya kidunia, na mabadiliko ya maisha.

Picha
familia ikiangalia maandiko pamoja

Rais Russell M. Nelson amesema: “Wakati hamu yako kuu inapokuwa kumwacha Mungu ashinde, kuwa sehemu ya Israeli, maamuzi mengi yanakuwa rahisi. Matatizo mengi yanakuwa si matatizo tena! … Unajua kile unachotaka kutimiza. Unajua ni aina gani ya mtu unataka kuwa.”4.

Unapozingatia kile kilicho muhimu hasa, utaona kwamba mchakato wa kuimarisha hali yako kiroho na kuwa makini kiroho inaweza kuwa rahisi, ingawa inahitaji juhudi na bidii. Kwa hiyo, shikilia na endelea kupiga pedali!

Lisha Liahona yako ya Kiroho

Unapigwa kwa kiwiko, unapigwa kikumbo, na kuvutwa pande nyingi na sauti za ulimwengu huu ambao nyakati zingine unaweza kuhisi kusita kuhusu upande gani unapaswa kwenda. Kumbuka kwamba Liahona yako ya kiroho inafanya kazi vizuri zaidi unapokuwa unatofautisha kati ya sauti ya Roho na sauti za ulimwengu

Roho Mtakatifu ni tulivu, wazi, na yenye kufariji. Inatoa mwongozo dhahiri wa kukuletea amani na matumaini. Inafanya kazi kwa umoja kamili na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo, akitekeleza majukumu mengi ili kukusaidia wewe kuishi kwa haki na kupokea baraka za injili.

“Chanzo kikuu cha nguvu za kiroho ni Mungu Baba yetu,” alisema Rais President Nelson. “Mjumbe wa nguvu hii ni Roho Mtakatifu. Nguvu hii inatofautiana na nguvu ya umeme. Kifaa cha umeme kinanyonya nguvu. Matumizi ya nguvu Yake ya kiroho hujaza tena nguvu yetu. Wakati nguvu ya umeme inaweza kutumika tu kwa vipindi vilivyopimwa vya wakati, nguvu ya kiroho inaweza kutumika kwa wakati huu na kwa milele!”5

Ili kuwa makini kiroho, shikilia, endelea kupiga pedali, na weka malengo ya kiroho. Tumia nyenzo nyingi zinazopatikana ili kuimarisha roho yako.

Ninashuhudia kwamba ili kuwa makini kiroho hakika ni uzima na amani (ona 2 Nefi 9:39), kwamba kiwango cha maisha yetu kinaboreka wakati tunapokuwa katika muafaka na Baba na Mwana, na kwamba Mungu anatupenda sisi na anatujali sisi na mahitaji yetu.

Kutoka katika hotuba ya ibada ndogo, “To Be Spiritually Minded Is Life and Peace,” iliyotolewa huko Chuo Kikuu cha Brigham Young, Februari 9, 2021. Kwa hotuba nzima, nenda speeches.byu.edu.

Mihtasari

  1. Mzee Bruce R. McConkie (1915–85) alifundisha, “To have fellowship with the Lord in this life is to enjoy the companionship of his Holy Spirit” (Doctrinal New Testament Commentary [1973], 3:374).

  2. Dallin H. Oaks, “Spirituality,” Ensign, Nov. 1985, 61.

  3. Quentin L. Cook, “Misingi ya Imani,” Liahona, Mei 2017, 129.

  4. Russell M. Nelson, “Acha Mungu Ashinde,” Liahona, Nov. 2020, 94.

  5. Russell M. Nelson, “Protect the Spiritual Power Line,” Ensign, Nov. 1984, 31.