2023
Kuweni Wafuasi wa Amani wa Kristo
Novemba 2023


Kuweni Wafuasi wa Amani wa Kristo

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Kwa wale kati yetu katika Kanisa tunaojitahidi kuwa “wafuasi wa amani wa Kristo,” siku angavu zaidi inatungoja tunapofokasi kwa Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo. Majaribu ni sehemu ya maisha ya duniani na hutokea katika maisha ya kila mtu duniani kote. …

Viongozi wa kanisa huulizwa mara kwa mara, “Kwa nini Mungu mwenye haki anaruhusu mambo mabaya yatokee, hasa kwa watu wazuri?” …

Hatujui majibu yote; hata hivyo, tunajua kanuni muhimu zinazoturuhusu kupitia majaribu, taabu na dhiki kwa imani na uthabiti kwa matumaini ya kesho nzuri inayomngojea kila mmoja wetu. …

Tunatambua kwamba karibu sisi sote tumepitia dhoruba za kimwili na za kiroho maishani mwetu, nyingine zenye kuharibu. Baba wa Mbinguni mwenye upendo na Mwanawe, Yesu Kristo, ambaye ni kichwa cha Kanisa Lake lililorejeshwa, wametupatia maandiko na manabii ili kututayarisha, kutuonya kuhusu hatari, na kutupa mwongozo wa kututayarisha na kutulinda. Maelekezo mengine yanahitaji hatua ya haraka, na mengine hutoa ulinzi kwa miaka mingi katika siku zijazo. …

… Maisha yaliyojaa kusifu, muziki na shukrani yamebarikiwa kipekee. Kuwa na furaha na kutegemea usaidizi wa mbinguni kupitia maombi ni njia yenye nguvu ya kuwa wafuasi wa amani wa Kristo. Kujitahidi kila wakati kuwa na moyo mkunjufu husaidia kuepuka kuwa na huzuni. …

Kama Mtume wa Bwana Yesu Kristo, ninashuhudia kwamba “wafuasi wa amani wa Kristo” watapata amani binafsi katika maisha haya na muunganiko mtukufu wa mbinguni.