2018
Muujiza Katika Nyumba ya Bwana Huko Kyiv
Oktoba 2018


Muujiza Katika Nyumba ya Bwana Huko Kyiv

Doru Vasile

Bucharest, Romania

Picha
President Monson greeting members in the temple

Kielelezo na Allen Garns

Mimi na familia yangu tulikuwa na shauku ya kusafiri kwa gari kutoka Romania kwenda Kyiv, Ukraine, kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa hekalu mnamo Agosti 2010. Kwa kujua kwamba hili litakuwa hekalu kwa Watakatifu huko Misheni ya Romania/Moldova, tulisafiri kwa takriban saa14 ili tu kuwa pale. Tulipofika, tulikutana na kundi lingine ambalo pia lilisafiri kutoka Romania. Wote tulikuwa na furaha kuwa Kyiv kwa ajili ya tukio hili takatifu.

Katika siku ya kuweka wakfu, kundi letu kutoka Romania lilipewa jukumu la kuangalia uwekaji wakfu kupitia matangazo katika chumba cha chini cha hekalu. Baadhi walianza kuelezea kuvunjika moyo kwao. Walikuwa wametegemea kushiriki katika uwekwaji wakfu pamoja na nabii katika chumba cha selestia. Baadhi hata walisema wangeweza kubaki tu nyumbani na kuangalia matangazo katika nyumba zao za ibada huko Romania.

Nilianza kusali katika moyo wangu, “Baba wa Mbinguni, ni kwa namna gani tunaweza kuwasaidia waumini hawa kutoka Romania kuwa na uzoefu usiosahaulika katika nyumba Yako?”

Bado sikupokea jibu wakati kipindi cha uwekaji wakfu kilipoanza. Punde tuligundua kwamba nabii, Rais Thomas S. Monson (1927–2018), atakuja kwenye chumba cha chini na kuweka jiwe la msingi. Labda hili lingekuwa jibu letu! Nilisali kwa ajili ya uwezekano ili Nabii aje na kuwasalimu Watakatifu wa Romania.

“Siombi jambo hili kwa ajili yangu mwenyewe,” nilisali, “Lakini kwa ajili ya kaka na dada zangu.”

Baada ya sherehe ya uwekaji jiwe la msingi, Rais Monson alitembea kupita chumba chetu akielekea chumba cha selestia. Ghafla, nilihisi katika moyo wangu kwamba lazima nisimame na kumwalika kuja kwenye chumba chetu.

Nilisimama na kusema, “Nabii wetu! Njoo na utuone. Sisi tunatokea Romania.”

Alionekana kutonisikia. Kisha muda mfupi baadae, alirudi. “Romania!” alisema na kuingia chumbani

Alitusalimia kila mmoja wetu na akasema anatupenda sana. Moyo wangu ulijaa wakati nilipoziangalia nyuso za shangwe za waumini wetu wapendwa. “Asante, Baba mpendwa,” Nilisali, “kwa muujiza huu katika nyumba Yako.”

Wakati nabii alipotoka chumbani, hakuna aliyekuwa na huzuni tena. Nilihisi kwamba tulikuwa kwenye chumba kilichobarikiwa zaidi katika hekalu. Ulikuwa ni uzoefu ambao sitausahau.