2022
Kuwasaidia Mababu Kupata Ibada Takatifu
Machi 2022


NJIA YANGU YA AGANO

Kuwasaidia Mababu Kupata Ibada Takatifu

Historia ya familia huleta baraka kwa wanafamilia wote.

Baba yetu wa Mbinguni anawapenda watoto Wake wote na ameandaa njia kwa ajili ya wanafamilia wetu waliofariki kupokea baraka za injili. Kata na matawi mengi yana madarasa ya historia ya familia ambayo huwafunza waumini jinsi ya kukusanya majina na taarifa za wanafamilia.

Dada Dolly Nyandei, kutoka kata ya Dobsonville Kigingi cha Soweto, anapenda historia ya familia na anaelezea jinsi alivyoanza. “Nilihudhuria darasa la historia ya familia kanisani na nilijifunza zaidi kuhusu kujaza chati ya vizazi na vipengele vingine muhimu kuhusu familia yangu.”

“Kwa kufunga na sala, Roho Mtakatifu aliniongoza kujua mambo mengine kama vile majina na tarehe zilizokuwa zinahitajika kwa ajili ya mababu zangu. Pia, mikusanyiko ya familia ilinisaidia kupata taarifa zaidi.”

“Nilipata utambuzi zaidi katika Malaki 4 mstari wa 5 na 6. Nabii Eliya alifundisha kuhusu kuigeuza mioyo ya watoto kuwaelekea baba zao na ya baba kuwaelekea watoto wao, kabla ya kuja kwa siku ya kuogofya ya Bwana. Hiyo ilinipa utambuzi kwenye muunganiko na upendo tulionao pamoja na mababu zetu. Wao wako pamoja nasi kiroho.”

Kuna rasilimali nyingi ndani ya kanisa za kukusaidia wewe katika kuanza kukusanya majina ya familia yako. Kijitabu cha ‘Familia Yangu’ na FamilySearch.org ni njia mbili za kuanzia. Tafuta rafiki au mwanafamilia wa kukusaidia kujaza majina ya wanafamilia yako. Kisha unaweza kupanga tarehe ya kuhudhuria hekaluni pamoja na familia na marafiki na kufanya ubatizo kwa niaba ya wanafamilia yako waliofariki.

Rais Russell M. Nelson alisema, “Wakati hekalu na kazi ya historia ya familia ina nguvu ya kuwabariki wale walio upande wa pili wa pazia, ina nguvu sawa ya kuwabariki pia wale walio hai.  Ina ushawishi wa utakaso kwa wale wanaojihusisha nayo. Kiuhalisia wanasaidia kuziinua familia zao.”1

Unapotafakari kwa sala ni mababu gani wa familia wa kuwapeleka hekaluni, utapokea Roho wa kukuongoza kadiri unavyowahudumia.

“Wakati nikifanya ibada muhimu hekaluni,” Dada Dolly anasimulia, “Nilihisi uwepo wa Baba wa Mbinguni, shangwe Yake na upendo Wake kwani nilikuwa nimeunganishwa na mababu zangu katika roho. Tutabarikiwa kwa wingi na wao pia watakuwa na ile shangwe ya kuachiliwa kutoka kifungoni kwani sisi si kitu bila wao kadhalika na wao bila sisi.”

Nabii wetu ametuambia: “Bwana anaharakisha kazi Yake ya kukusanya Israeli.  Kukusanya huko ni jambo muhimu sana linalotokea duniani hivi leo . . . ikiwa utachagua, ikiwa unataka, unaweza kuwa sehemu kubwa ya jambo hili. Unaweza kuwa sehemu kubwa ya jambo kubwa, jambo la kustaajabisha sana, jambo adhimu!”2

Acha tufuate ushauri wa Rais Nelson na kuwa sehemu ya jambo kubwa, la kustaajabisha sana na adhimu kwa kufanya historia ya familia yetu.

Muhtasari

  1. Russell M. Nelson, “Vizazi Vilivyounganishwa kwa Upendo”, Mkutano Mkuu, Aprili 2010.

  2. Russell M. Nelson, “Tumaini la Israeli”, Ibada ya Vijana Ulimwenguni kot, Juni 2018.