2022
Kuwasaidia Masikini na Wenye Huzuni—Dondoo
Novemba 2022


“Kuwasaidia Masikini na Wenye Huzuni—Dondoo,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Nov. 2022.

Kuwasaidia Masikini na Wenye Huzuni

Dondoo

Picha
Nukuu ya Oaks kwenye bango

Pakua PDF

Ustawi mkubwa na huduma ya kibinadamu kwa wanadamu wenzetu vimefundishwa na kufanyiwa kazi na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho pamoja na sisi kama waumini wake. Kwa mfano, tunafunga kila mwanzo wa mwezi na kuchangia angalau kiasi kinacholingana cha milo ambayo haikuliwa ili kuwasaidia wenye uhitaji katika mikusanyiko yetu. Kanisa pia linatoa michango mikubwa kwa ajili ya huduma za kibinadamu na zinginezo kote ulimwenguni.

Licha ya yote ambayo Kanisa letu linafanya moja kwa moja, huduma nyingi za kibinadamu kwa watoto wa Mungu ulimwenguni kote hufanywa na watu na mashirika yasiyo na muunganiko rasmi na Kanisa letu. …

Kanisa la Yesu Kristo limejikita kwenye kuwahudumia wenye uhitaji na pia limejikita kwenye kushirikiana na wengine katika juhudi hiyo. …

Ufunuo wa siku za leo unafundisha kwamba Mwokozi wetu, Yesu Kristo, ni “nuru ya kweli imwangazayo kila mtu ajaye ulimwenguni.” [Mafundisho na Maagano 93:2]. Kama matokeo, watoto wote wa Mungu huangazwa kumtumikia Yeye na kutumikiana kwa maarifa yao yote na uwezo wao wote. …

… Wengi wetu tunapaswa kutambua mazuri yaliyofanywa na wengine na kuyaunga mkono kwani tuna muda na nyenzo za kufanya hivyo. …

Ninashuhudia juu ya Yesu Kristo, ambaye nuru na Roho wake huwaongoza watoto wote wa Mungu katika kuwasaidia masikini na wenye huzuni kote ulimwenguni.