2023
Mtegemee Mungu kwa ajili ya Dhumuni na Mwongozo
Septemba 2023


“Mtegemee Mungu kwa ajili ya Dhumuni na Mwongozo,” Liahona, Sept. 2023.

Kwa ajili ya Wazazi

Mtegemee Mungu kwa ajili ya Dhumuni na Mwongozo

Picha
familia ikisali

Wapendwa Wazazi,

Baba yetu wa Mbinguni hakututuma ulimwenguni bila mwongozo. Kupitia vipawa vya kiungu vya maandiko, sala, manabii walio hai, mmoja na mwingine, na vingine zaidi, tunaweza kumtegemea Mungu kwa ajili ya dhumuni na Mwongozo. Mnaposoma toleo hili la Liahona, tafakarini nyenzo ambazo Yeye ametupatia ili zitusaidie kupata maana katika maisha haya na kurudi Kwake katika maisha yajayo.

Mijadala ya Injili

Wajibu Wetu wa Pamoja katika Mpango wa Mungu

Kama familia, tungeweza kusoma 1 Wakorintho 11:11 na kujadili kile inachomaanisha. Shirikini kauli kutoka kwenye makala ya Mzee Gerrit W. Gong (ukarasa wa 4), ambazo zinaeleza wajibu wa pamoja wanaume na wanawake walionao katika mpango wa wokovu. Je, ni kwa jinsi gani tofauti zetu zinatuunganisha badala ya kutugawanya?

Nguvu ya Uponyaji ya Imani

Someni Mathayo 15:21–28 pamoja, ambayo inazungumza kuhusu mwanamke wa Kanaani. Kwa nini mnadhani imani yake iliongoza kwenye uponyaji wa binti yake? Someni vifungu vya maneno kutoka kwenye makala ya Rais Camille N. Johnson kwenye ukurasa wa 8 ili kuelewa vyema wajibu wa upole na imani katika kufikia nguvu za Bwana.

Ukumbusho wa Kila Siku wa Yesu Kristo

Kama familia, Je, ni kwa jinsi gani mtamkumbuka Mwokozi katika maisha yenu? Soma sehemu muhimu kutoka kwenye makala hii kwenye ukurasa wa 38 kuhusu umuhimu wa kukumbuka. Fikiria kuonesha katika nyumba yenu picha au nukuu ambayo inawakumbusha juu ya Kristo.

Njoo, Unifuate Burudani ya Familia

Kumbukeni Baraka za Kristo Kila Siku.

1 Wakorintho 15

Paulo alifundisha huko Korintho: “kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu … na kwamba alizikwa, na kwamba alifufuka tena siku ya tatu” (1 Wakorintho 15:3–4). Aliwahimiza “wayashike sana maneno” (1 Wakorintho 15:2) injili aliyowahubiria. Ialike familia yako icheze mchezo huu wa kumbukumbu:

  1. Mpe kila mmoja muda wa kuandika jibu fupi la swali lifuatalo: Ni baraka ipi ya injili unaifurahia kwa sababu ya Upatanisho wa Mwokozi? (Kwa baadhi ya mawazo, ona 1 Wakorintho 15:19–29.)

  2. Fanyeni zamu kushiriki kile mlichoandika na kurudia kwa kumbukumbu kile ambacho mtu kabla yako alikiandika.

Mjadala: Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kukumbuka vyema baraka ambazo Kristo ametupatia? Fikiria kufanya mpango wa familia ili kufikiria njia moja kila siku ambayo kupitia hiyo Kristo amebariki maisha yenu.