Muziki
Tumsifu Mungu Wetu


34

Tumsifu Mungu Wetu

Kwa shauku

1. Tumsifu Mungu wetu

Aliye mbinguni,

Atawala kwa dhamira,

Mbingu nazo nchi.

[Chorus]

Jina lake liinue;

Sifu utawala!

Msujudu Bwana Mungu,

Mfalme daima.

2. Chini yake, kwa amriye,

Sayari na mbingu

Huonyesha kila saa

Hekima ya Mungu.

[Chorus]

Jina lake liinue;

Sifu utawala!

Msujudu Bwana Mungu,

Mfalme daima.

3. Ua dogo liishilo,

Ndege wa msimu,

Nao pia wanatunzwa;

Kawaumba Mungu.

[Chorus]

Jina lake liinue;

Sifu utawala!

Msujudu Bwana Mungu,

Mfalme daima.

4. Sauti za kuvutia

Nyimbo zimwimbie;

Tumsifu, sala zetu

Azijibu zote.

[Chorus]

Jina lake liinue;

Sifu utawala!

Msujudu Bwana Mungu,

Mfalme daima.

Maandishi: Ada Blenkhorn, 1858–1927

Muziki: Alfred Beirly, 1848–1929

1 Mambo ya Nyakati 16:29

Mathayo 10:29–31