Muziki
Ee Baba wa Milele


94

Ee Baba wa Milele

Kwa unyenyekevu

1. Ee Baba wa milele,

Uliye mbinguni,

Katika jina Lake,

Takasa, bariki—

Ikiwa tu wasafi—

Mkate, divai,

Ili tuikumbuke

Damu nao mwili.

2. Dhabihu takatifu

Tusiyoelewa,

Kusamehewa dhambi,

Na kumkumbuka,

Ili tushuhudie

Kuteswa kwa Kristo,

Tuwe na Roho wake,

Na upatanisho.

3. Na Yesu, Mteule,

Akashuka chini

Kujitoa dhabihu

Kuokoa nafsi—

Asiye na mvuto,

Wa kutamaniwa—

Mwokozi wa ahadi

Akatutakasa.

4. Ile hekima kuu,

Mpango kamili

Ulifanya wokovu,

Neno kuwa mwili,

Kushuka duniani

Awe mwanadamu,

Afe, japo Mfalme,

Kutuweka huru.

Maandishi: William W. Phelps, 1792–1872. Yalijumuishwa katika kitabu cha kwanza cha nyimbo za Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, 1835.

Muziki: Felix Mendelssohn, 1809–1847

Mafundisho na Maagano 20:77, 79

Isaya 53:2–5