Muziki
Bwana, Pokea Uliko


124

Bwana, Pokea Uliko

Kwa kushangilia

1. Bwana, pokea uliko

Kila anayetubu,

Azaliwaye kwa maji

Na roho wako, Mungu.

Wafariji na ongoza

Maisha ya vijana;

Na neno lako tukufu

Liwape maarifa.

2. Hamjui ndiye Mungu?

Na akawa shahidi,

Kwamba njia ni nyembamba

Irudiyo mbinguni.

Sikia habari njema;

“Njoo, unifuate

Katika ufalme wangu,

Na uishi milele.”

3. Ukweli umerejeshwa:

Ibada takatifu,

Kwa agano ziokoe

Milele wanadamu!

Watu wote mfurahi!

Watu wote muimbe!

Waliokufa wasifu

Mungu wetu Mfalme!

Maandishi: Mabel Jones Gabbott, 1910–2004. © 1948 IRI

Muziki: Alexander Schreiner, 1901–1987. © 1948 IRI

2 Nefi 31:5–13

Mafundisho na Maagano 128:12, 22