Muziki
Twashukuru Mungu


45

Twashukuru Mungu

Kwa heshima

1. Twashukuru Mungu

Kwa moyo na sauti,

Miujiza yake

Wanyonge tunakiri;

Tangu tu wachanga

Ametuongoza,

Na baraka zake

Bado anatupa.

2. Ewe Mungu wetu,

Kuwa nasi daima

Tuwe na amani,

Tuwe nayo furaha,

Utupe upendo

Na utuongoze.

Tuepushe dhambi,

Kwa nguvu tulinde.

Maandishi: Martin Rinkhart, 1586–1649; yametafsiriwa na Catherine Winkworth, 1829–1878

Muziki: Johann Crüger, 1598–1662

1 Mambo ya Nyakati 16:8–14

Alma 26:8