2021
Je, Mwokozi Amefanya Nini kwa ajili Yetu Sisi?
Mei 2021


“Je, Mwokozi Amefanya Nini kwa ajili Yetu Sisi?,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Mei 2021.

Kikao cha Ukuhani

Je, Mwokozi Amefanya Nini kwa ajili Yetu Sisi?

Dondoo

Picha
Kaburi tupu la Kristo

Je, Yesu Kristo amefanya nini kwa ajili ya kila mmoja wetu? Yeye amefanya kila kitu ambacho ni muhimu kwa ajili ya safari yetu hapa duniani kuelekea kudura iliyoelezwa katika mpango wa Baba yetu wa Mbinguni. Nitaongelea vipengele vikuu vinne vya mpango huo. …

Ufufuko unatupa mtazamo na nguvu ya kuvumilia changamoto za kidunia zinazomkabili kila mmoja wetu na wale tunao wapenda. Unatupatia namna mpya ya kuyatazama mapungufu ya kimwili, kiakili, au kihisia tuyapatayo wakati wa kuzaliwa au tuyapatayo katika maisha yetu ya duniani. Unatupa nguvu ya kuvumilia huzuni, kushindwa, na kukatishwa tamaa.

Ufufuko pia unatupatia sisi kichocheo chenye nguvu ya kushika amri za Mungu wakati wa maisha yetu ya hapa duniani.

Mwokozi na Mkombozi wetu aliteseka mateso tusiyoweza kuelewa ili awe dhabihu kwa dhambi za wenye mwili wote ambao wangetubu. Dhabihu hii ya kulipia dhambi ilitoa kilicho bora, mwanakondoo asiye na waa, kwa ajili ya kipimo kikuu cha uovu, dhambi za ulimwengu wote. …

… Yesu alitufundisha mpango wa wokovu. Mpango huu unajumuisha Uumbaji, kusudi la maisha, umuhimu wa upinzani, na zawadi ya haki ya kujiamulia. Yeye pia alitufundisha sisi amri na maagano ambayo lazima tuyatii na ibada ambazo lazima tuzipitie ili ziturudishe kwa wazazi wetu wa mbinguni. …

Mwokozi wetu anahisi na anajua majaribu yetu, masumbuko yetu, shida zetu, na kuteseka kwetu, kwani Yeye kwa hiari aliyapitia yote kama sehemu muhimu ya Upatanisho Wake. … Wale wote wanaoteseka kwa aina yoyote ya udhaifu wanapaswa kukumbuka kwamba Mwokozi wetu pia alipitia aina hiyo ya maumivu na kwamba kupitia Upatanisho Wake anampatia kila mmoja wetu nguvu ya kuvumilia.