2021
Yesu Kristo: Mtunzaji wa Nafsi Zetu
Mei 2021


“Yesu Kristo: Mtunzaji wa Nafsi Zetu,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Mei 2021.

Kikao cha Jumapili Asubuhi

Yesu Kristo: Mtunzaji wa Nafsi Zetu

Dondoo

Picha
Yesu Kristo akimponya mtu

Moyo wangu unashangilia ninapokumbuka tendo kubwa la kushangaza zaidi, lenye utukufu zaidi, lisilopimika zaidi ambalo limewahi kutokea katika historia yote ya mwanadamu—ile dhabihu ya Bwana, Yesu Kristo ya kulipia dhambi. …

Kristo kwa neema alikamilisha mapenzi ya Baba kupitia dhabihu Yake isiyo na mwisho na yenye rehema. Alishinda uchungu wa kifo cha kimwili na kiroho, alitambulisha kwa ulimwengu kupitia Anguko, akitupatia sisi uwezekano mtukufu wa wokovu wa milele. …

Wakati kupitia dhabihu Yake Mwokozi bila masharti aliondoa athari za kifo cha kimwili, Yeye hakuondosha wajibu wetu binafsi wa kutubu kwa ajili ya dhambi zetu tunazotenda.

Marafiki zangu wapendwa, Ninashuhudia kwenu kwamba tufanyapo toba ya kweli ya dhambi zetu, tunaruhusu dhabihu ya Kristo ya kulipia dhambi kuwa na matokeo makubwa katika maisha yetu. …

Katika nyongeza kwa zawadi hii tukufu ya wokovu, Mwokozi anatupa nafuu na faraja tunapokabiliana na mateso, majaribu, na madhaifu yetu ya maisha katika mwili wenye kufa, pamoja na hali tulizopitia hivi karibuni katika janga la ulimwengu lililopo. …

Tunapomkaribia Yeye zaidi, tukijisalimisha wenyewe kiroho kwenye uangalizi Wake, tutakuwa na uwezo wa kujichukulia juu yetu wenyewe nira Yake, ambayo ni rahisi, na mzigo Wake, ambao ni mwepesi, na hivyo kupata ile faraja na pumziko lililoahidiwa. Zaidi ya hayo, tutapokea nguvu sisi wote tunazohitaji ili kushinda shida, udhaifu, na huzuni za maisha, ambazo ni ngumu zaidi kuvumilia bila msaada na nguvu Zake za uponyaji.