2021
Napenda Kuona Hekalu
Mei 2021


“Napenda Kuona Hekalu,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Mei 2021.

Kikao cha Jumamosi Asubuhi

Napenda Kuona Hekalu

Dondoo

Picha
hekalu

Hekalu la Durban Afrika Kusini

Mimi najua kwamba mahekalu ya Bwana ni mahali patakatifu. Kusudi langu leo katika kuzungumza juu ya mahelalu ni kuongeza hamu yenu na yangu ya kuwa wastahiki na tayari kwa ajili ya ongezeko la fursa za uzoefu wa hekaluni ambazo zinakuja kwetu. …

Kama wewe au mimi tutaenda hekaluni tukiwa si wasafi vya kutosha, hatutaweza kuona, kwa nguvu za Roho Mtakatifu, mafundisho ya kiroho kuhusu Mwokozi ambayo tunaweza kuyapokea ndani ya hekalu.

Tunapokuwa wastahiki kupokea mafundisho hayo, kutakuwa na ongezeko kupitia uzoefu wetu wa hekaluni tumaini, furaha, na msimamo wa kutegemea mema kote maishani mwetu. Tumaini hilo, furaha, na msimamo wa kutegemea mema hupatikana tu kwa kukubali ibada zinazofanywa ndani ya mahekalu matakatifu. Ni ndani ya hekalu ambapo tunaweza kupokea hakikisho la muunganiko wa upendo wa familia ambao utandelea baada ya kifo na kudumu milele. …

… Na tunajua kwamba furaha yetu ya milele hutegemea juu ya jithada zetu za kutoa furaha hiyo hiyo ya kudumu kwa wengi wa ukoo wetu kadiri tunavyoweza.

Ninahisi hamu hiyo hiyo ya kufanikiwa katika kuwaalika wanafamilia walio hai kuwa na hamu ya kuwa wastahiki kupokea na kuheshimu ibada za kuunganisha zifanyikazo hekaluni. Hiyo ni sehemu ya kukusanya Israeli kulikoahidiwa katika siku za mwisho pande zote mbili za pazia.