2021
Upendo wa Mungu: Furaha Zaidi kwa Nafsi
Novemba 2021


“Upendo wa Mungu: Furaha Zaidi kwa Nafsi,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Nov. 2022.

Kikao cha Jumamosi Alasiri

Upendo wa Mungu: Furaha Zaidi kwa Nafsi

Dondoo

Picha
maandiko

Tunaweza kuuelezea upendo wa Mungu kama nuru inayosambaa kutoka kwenye mti wa uzima, ikijieneza kila mahala juu ya dunia yote mpaka ndani ya mioyo ya watoto wa watu. Nuru ya Mungu na upendo vinasambaa kwa viumbe Vyake vyote.

Wakati mwingine kimakosa tunadhani kwamba tunaweza tu kuhisi upendo wa Mungu baada ya kufuata fimbo ya chuma na kula tunda. Upendo wa Mungu, hata hivyo haupokelewi tu na wale wanaokuja kwenye mti bali ni nguvu hasa ambayo inatusababisha sisi tuutafute ule mti. …

Upendo wa Mungu haupatikani katika hali za maisha yetu, bali katika uwepo Wake ndani ya maisha yetu. Tunafahamu kuhusu upendo Wake wakati tunapopokea nguvu zaidi ya zetu wenyewe na wakati Roho Wake anapoleta amani, faraja na mwongozo. Nyakati zingine inaweza kuwa vigumu kuhisi upendo Wake. Tunaweza kuomba kuwa na macho yetu yakiwa yamefunguliwa ili kuuona mkono Wake katika maisha yetu na kuuona upendo Wake katika uzuri wa uumbaji Wake.

Tunapoyatafakari maisha ya Mwokozi na dhabihu yake isiyo na mwisho, tunaanza kuelewa upendo Wake kwa ajili yetu.

Ninashuhudia kwamba Bwana wetu na Mwokozi hakika alikufa kwa ajili ya kila mmoja wetu. … Lilikuwa ni onesho la upendo Wake usio na mwisho kwetu na kwa Baba Yake. …

Na tufungue mioyo yetu ili kupokea upendo msafi ambao Mungu anao kwa ajili yetu na kisha kuumimina upendo huo katika yote tunayofanya na yale tuliyo.