2021
Yenye Kupendeza kwa Urahisi—Yenye Urahisi wa Kupendeza
Novemba 2021


“Yenye Kupendeza kwa Urahisi—Yenye Urahisi wa Kupendeza,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Nov. 2022.

Kikao cha Jumamosi Alasiri

Yenye Kupendeza kwa Urahisi—Yenye Urahisi wa Kupendeza

Dondoo

Picha
Yesu Kristo katika Gethsemane

Ili kupokea uzima wa milele, ni lazima sisi “tuje kwa Kristo, na kukamilishwa ndani Yake” [Moroni 10:32]. Tunapokuja kwa Kristo na kuwasaidia wengine kufanya vivyo hivyo, tunashiriki katika kazi ya Mungu ya wokovu na kuinuliwa, ambayo inafokasi juu ya majukumu matakatifu yaliyoainishwa. Majukumu haya matakatifu yanafungamana na funguo za ukuhani zilizorejeshwa na Musa, Elia na Eliya, kama ilivyoandikwa katika sehemu ya 110 ya Mafundisho na Maagano,3 na amri kuu ya pili iliyotolewa kwetu na Yesu Kristo ya kuwapenda jirani zetu kama tunavyojipenda wenyewe. Yanapatikana katika kurasa mbili za mwanzo za Kitabu cha Mwongozo, kilichofanyiwa maboresho kinachopatikana kwa waumini wote. …

  1. Kuishi Injili ya Yesu Kristo

  2. Kuwajali wale wenye mahitaji

  3. Kuwaalika watu wote waipokee injili

  4. Kuunganisha familia milele

Unaweza kuyatazama jinsi mimi ninavyoyatazama: kama ramani ya njia ya kurudi kwa Baba yetu wa Mbinguni mwenye upendo. …

Imesemwa kwamba injili ya Yesu Kristo “inapendeza kwa Urahisi na ina urahisi wa kupendeza.” Ulimwengu hauko hivyo. Una changamoto, usioeleweka na umejawa dhoruba na migogoro. Tunabarikiwa pale tunapokuwa makini kutoruhusu ugumu, ambao ni wa kawaida ulimwenguni, kuingilia njia ambayo kwayo tunapokea na kufanyia kazi injili.

… Sote tunapaswa kujitahidi kuifanya injili iwe rahisi—katika maisha yetu, katika familia zetu, katika madarasa na akidi zetu na katika kata na vigingi vyetu.