2021
Amani ya Kristo Huondoa Uadui
Novemba 2021


“Amani ya Kristo Huondoa Uadui,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Nov. 2022.

Kikao cha Jumapili Asubuhi

Amani ya Kristo Huondoa Uadui

Dondoo

Picha
wafanyakazi wa kupiga makasia

Yesu Kristo alieleza kwamba fundisho Lake halikuwa “kuchochea mioyo ya watu kwa hasira, mtu na mwenzake; bali mafundisho [yake] ni kwamba mambo kama hayo yaondoke” [3 Nefi 11:28–30]. …

Baada ya Mwokozi kutembelea Amerika, watu waliungana. … Tofauti zao zilionekana kuwa ndogo kuliko upendo wao wa pamoja wa Mwokozi, na waliungana kama “warithi wa ufalme wa Mungu” [4 Nefi 1:17]. Matokeo yalikuwa kwamba “hakungekuwa na watu wenye furaha zaidi ambao walikuwa wameumbwa kwa mkono wa Mungu” [4 Nefi 1:16].

Umoja unahitaji juhudi. Umoja unakua pale tunapokuza upendo wa Mungu ndani ya mioyo yetu na tunazingatia hatima yetu ya milele. Tunaunganishwa kwa utambulisho wetu wa msingi wa pamoja kama watoto wa Mungu na dhamira yetu kwenye ukweli wa injili ya urejesho. Upendo wetu kwa Mungu na ufuasi wetu kwa Yesu Kristo huleta kujali wengine kwa dhati. …

Pale upendo wa Kristo unapojaza maisha yetu, tutatatua kutokukubaliana kwa upole, uvumilivu na wema. Tuna wasiwasi kidogo kuhusu hisia zetu wenyewe na zaidi kuhusu jirani zetu. Tunatafuta kuweka mambo sawa na kuunganisha. Hatujihusishi katika “mabishano yasiyo na manufaa,” kuwahukumu wale tusiokubaliana nao, au kujaribu kuwafanya wakosee. Badala yake, tunachukulia kwamba wale ambao hatukubaliani nao wanafanya kadiri wawezavyo kwa uzoefu wa maisha waliyonayo. …

… Mwaliko wangu ni tuwe majasiri kwa kuweka upendo wetu kwa Mungu na ufuasi kwa Mwokozi juu ya matamanio mengine yote. Tuimarishe agano tulilonalo katika ufuasi wetu—agano la kuwa wamoja.