2021
Tumaini Tena
Novemba 2021


“Amini Tena,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Nov. 2022.

Kikao cha Jumapili Alasiri

Tumaini Tena

Dondoo

Picha
mwana mpotevu

Wana Wapotevu Wawili, na Jorge Cocco

Je, umewahi kuhisi kama unatoroka nyumbani? Mara nyingi, kukimbia kutoka nyumbani kunamaanisha kwamba tumaini limeharibika au limevunjika—tumaini baina yetu wenyewe, sisi kwa sisi, pamoja na Mungu. Wakati tumaini linapopitia changamoto, tunastaajabu ni jinsi gani ya kutumaini tena.

Ujumbe wangu leo ni kwamba, kama tunakuja nyumbani au tunakwenda nyumbani, Mungu anakuja kukutana nasi. Katika Yeye tunaweza kupata imani na ujasiri, hekima na utambuzi, kuwa na tumaini tena. Vivyo hivyo, anatuomba tuweke nuru kwa kila mmoja wetu, tuwe wenye kusamehe zaidi na wenye kujihukumu kidogo sisi wenyewe na wenzetu, ili Kanisa Lake liwe mahali ambapo tunahisi kuwa nyumbani, iwe tunakuja kwa mara ya kwanza au kurejea tena.

Tumaini ni tendo la imani. …

Tunajua kwamba furaha kwenye njia ya agano la Bwana, na wito wa kutumikia katika Kanisa Lake ni mwaliko wa kuhisi tumaini la Mungu na upendo kwetu na kwa kila mmoja. …

Tumaini linakuwa halisi wakati tunapofanya mambo magumu kwa imani. Huduma na dhabihu huongeza uwezo na kusafisha mioyo. …

Wakati hali zetu binafsi ni za kipekee, tunaweza kupata msaada toka kwenye kanuni za injili na Roho mtakatifu kujua ikiwa, jinsi gani, na wakati gani wa kuwatumainia wengine tena. …

Mtumaini Mungu na miujiza Yake. Sisi na mahusiano yetu yanaweza kubadilika. …

Safari zetu za maisha ni za mtu binafsi, lakini tunaweza kurudi tena kwa Mungu Baba yetu na Mwanawe Mpendwa kupitia kuweka tumaini kwa Mungu, kwa kila mmoja wetu na sisi wenyewe.