2023
Wamoja katika Kristo
Mei 2023


Wamoja katika Kristo

Dondoo

Picha
karatasi za kupamba ukkutani

Pakua karatasi ya kupamba ukutani

Ni katika Yesu Kristo pekee sisi tunaweza kwa uhakika kuwa wamoja.

Kuwa wamoja katika Kristo huanza kwa mtu mmoja mmoja—sote tunaanza na sisi wenyewe. Sisi ni wanadamu wenye mwili na roho na wakati mwingine tupo katika vita ya nafsi zetu wenyewe. …

Yesu pia alikuwa mwanadamu mwenye mwili na roho. Alijaribiwa; Anaelewa; Anaweza kutusaidia tufikie umoja ndani yetu. …

… Kwa “kumvaa Kristo” hakika hujumuisha kufanya “amri Yake iliyo kuu na ya kwanza” [ona Mathayo 22:37–38] kuwa dhamira yetu ya kwanza na kuu, na kama tunampenda Mungu, tutashika amri Zake.

Umoja pamoja na kaka na dada zetu katika mwili wa Kristo hukua tunapotii amri ya pili—isiyoweza kutenganishwa na ya kwanza—ya kuwapenda wengine kama tunavyojipenda wenyewe. …

“Tunapomvaa Kristo,” inawezekana ama kutatua au kuweka kando tofauti, kutoelewana na migogoro. …

Umoja hauhitaji usawa, lakini unahitaji mapatano. Tunaweza kuwa na mioyo yetu ikiwa imefumwa pamoja katika upendo, tukawa wamoja katika imani na mafundisho na bado tukashangilia timu tofauti, tusikubaliane kwenye masuala mbalimbali ya kisiasa, tukawa na mijadala kuhusu malengo na njia sahihi ya kuyafanikisha na mambo mengine mengi kama hayo. Lakini kamwe hatuwezi kutofautiana au kubishana kwa hasira au kudharauliana. …

Narudia tena kwamba ni katika na kupitia uaminifu wetu binafsi na upendo kwa Yesu Kristo kwamba tunaweza kutumaini kuwa wamoja—wamoja ndani yetu, wamoja nyumbani, wamoja Kanisani, hatimaye wamoja katika Sayuni, na zaidi ya yote, wamoja pamoja na Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.