2023
Wafuasi wa Mfalme wa Amani
Mei 2023


Wafuasi wa Mfalme wa Amani

Dondoo

Picha
karatasi za kupamba ukkutani

Pakua karatasi ya kupamba ukutani

Kama wafuasi wa Mfalme wa Amani, tumeamriwa kuishi “mioyo ikiwa imefumwa pamoja katika umoja na kwa upendo kila mmoja kwa mwingine” [Mosia 18:21]. …

… Moja ya alama dhahiri kabisa ya kwamba tunasonga karibu na Kristo na kuwa zaidi kama Yeye ni jinsi tunavyowajali wengine kwa upendo, subira na wema, katika hali zozote zile. …

… Haishangazi kwamba moja ya mbinu za adui ni kuchochea uadui na chuki katika mioyo ya watoto wa Mungu. Anashangilia anapowaona watu wakikosoana, kufanyiana dhihaka na kutoleana kashifa. …

Wapendwa kaka zangu na dada zangu, tunapojitahidi kukuza tabia kama za Mwokozi, tunaweza kuwa vyombo vya amani Yake ulimwenguni kulingana na mfumo ambao Yeye mwenyewe ameuweka. Ninawaalika kutafakari njia ambazo sisi wenyewe tunaweza kubadilika na kuwa watu wenye kuinua na kusaidia, watu wenye moyo wa kuelewa na kusamehe, watu wanaoangalia mazuri ya wengine, daima tukikumbuka kwamba “kama kuna kitu chochote kilicho chema, chenye kupendeza, au chenye taarifa njema au chenye kustahili sifa, tunayatafuta mambo haya.” [Makala ya Imani 1:13

Ninawaahidi kwamba tunapotafuta na kukuza tabia hizi, tutakuwa wakunjufu zaidi na zaidi na walio tayari kujali mahitaji ya wanadamu wenzetu na tutapata shangwe, amani na ukuaji wa kiroho.