2021
Baba Yetu wa Mbinguni Anatutaka Tuwe na Furaha
Julai 2021


Misingi ya Injili

Baba Yetu wa Mbinguni Anatutaka Tuwe na Furaha

Tunapokumbuka mpango wa Mungu wa furaha, tunaweza kupata furaha hata wakati maisha yanapokuwa magumu.

Picha
family looking at tree

Kazi zote za sanaa, isipokuwa ya mbali kulia, na J. Kirk Richards

Kabla hatujazaliwa duniani, sisi sote tuliishi pamoja na Baba wa Mbinguni kama watoto Wake wa kiroho. Alitoa mpango wa kuwasaidia watoto Wake kujifunza na kukua. Kupitia mpango Wake, tunaweza kuwa zaidi kama Yeye na kustahili kufurahia maisha ya milele. Mpango huu unawezekana kwa sababu Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, alikuja duniani kuteseka kwa ajili ya dhambi zetu, dhabihu inayoitwa Upatanisho.

Mpango wa Baba wa Mbinguni unaitwa mpango wa

Kama haya na maandiko mengine yanavyoonesha, Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kuwa kama Yeye, kurudi Kwake, na kuwa wenye furaha ya kweli (ona Musa 1:39).

Tunakuja Duniani Kujifunza na Kukua

Picha
globe

Mungu alituleta duniani, ambako tutakuwa na mwili wa nyama na mifupa (ona Mwanzo 1:26–27). Tulihitaji miili ili kutusaidia kupata uzoefu wa maisha hapa duniani.

Mungu alijua kwamba tusingeweza kuhisi furaha wakati wote. Tunapitia kukata tamaa, maumivu, na hata kifo. Bali kupitia changamoto za maisha, Baba wa Mbinguni anatusaidia kujifunza na kukua.

Mungu pia alitupa uhuru wa kuchagua, uwezo wa kuchagua kati ya mema na uovu. Anatuacha tujichagulie wenyewe kile tunachofikiri na kufanya. Ametupatia maandiko na manabii wanaoishi ili kutusaidia kujifunza kuchagua kilicho sahihi (ona Ibrahimu 3:25).

Jaribu Kuwa Kama Yesu Kristo

Mungu hakutuleta duniani bila mfano wa kufuata (ona Yohana 13:15). Alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo, kutuonyesha njia. Ili kujifunza jinsi ya kumfuata Yeye, tunaweza kusoma maandiko kujifunza Yeye ni nani na alifanya nini wakati wa maisha Yake duniani. Tunaweza pia kufanya kwa uwezo wetu wote kuwa kama Kristo kwa kumtii Mungu na kuwapenda wengine.

Tunapofanya makosa, tunaomba msamaha na kutegemea nguvu za Upatanisho wa Yesu Kristo kutusaidia sisi kubadilika. Tunaweza kuwa na furaha tunapojaribu kila siku kuwa zaidi kama Yeye.

Kifo sio Mwisho

Picha
Mary Magdalene and Jesus

Tunapokufa roho zetu huenda kwenye ulimwengu wa roho. Huko tunaendelea kujifunza tunapojiandaa kwa ajili ya ufufuko.

Wakati wa Ufufuko, miili yetu na roho vitaungana. Miili yetu itakuwa mikamilifu, na kamwe hatutasumbuliwa na kifo au maradhi. (Ona Alma 11:44–45.) Kama vile Yesu Kristo alivyokufa na kuishi tena, sisi sote tutaishi tena.

Wakati Mungu anapotuhukumu, Anaangalia matendo na matamanio yetu. Kama tumejaribu kutii amri na ahadi tulizofanya kwa Baba wa Mbinguni, tunaweza kuishi pamoja Naye tena.

Maisha pamoja na Mungu na Familia zetu Mbinguni

Katika ufalme wa selestia, tutaishi na Mungu na Yesu Kristo. Vilevile tutaweza kuishi huko pamoja na familia zetu milele na milele kama tumeunganishwa nao. Tutapata amani, furaha, na pumziko (ona Mosia 2:41).

Maisha yetu duniani yanaweza kuwa magumu nyakati zingine, bali kama tutamfuata Yesu Kristo, tunaweza kupata furaha katika maisha haya na shangwe ya milele katika maisha yajayo.

Maandiko Yanasema Nini kuhusu Mpango wa Furaha?

Picha
woman reading scriptures

Jinsi tunavyoishi maisha yetu ni muhimu. Mungu atatuhukumu na kutuzawadia kulingana na mawazo na matendo yetu. (Ona Alma 41:3)

Shetani ni adui kwa furaha yetu. Anatujaribu tutumie vibaya maisha yetu hapa duniani na kutenda dhambi. Yeye anataka sisi tuwe wenye taabu kama yeye. (Ona 2 Nefi 2:27).

Tunapokuwa na imani katika mpango wa Mungu kwa ajili yetu, tunaweza kuwa na amani bila kujali majaribu tunayokumbana nayo. Tunaweza kutegemea kuishi milele na Mungu. (Ona Mafundisho na Maagano 59:23.)