2021
Unapokuwa na Shaka, Fungua Mlango wa Imani
Julai 2021


Vijana Wakubwa

Unapokuwa na Shaka, Fungua Mlango wa Imani

Ingawa wakati mwingine tunaweza kuwa na shaka na uzoefu wetu wa kiroho, uhakika wetu unaweza ukawa wa kufurika.

Picha
woman standing before open door

Kama tulilelewa katika Kanisa au kuongoka baadae maishani, wengi wetu labda tumepata uzoefu wa nyakati za kujiuliza au kuwa na shaka. Tunaweza kuwa tulikuwa na uzoefu wa kiroho wa kushangaza bali sasa tunajikuta wenyewe tukistaajabu: uzoefu huo wa kiroho ulikuwa wa kweli, au niliwaza tu kumhisi Roho? Vipi kama kati ya haya si kweli? Na vipi kuhusu maswali yangu ambayo hayana majibu bado? Nawezaje kukaa katika Kanisa kama sina uhakika kwamba bado ni kweli?

Kwangu mimi, nilishangazwa kwamba maswali haya yalikuja baada ya kuwa nimemaliza kuhudumia misheni yangu! Nilikuwa mimeujua ukweli hadi kuwa na hakikisho la kwamba nilitaka kwenda kuhubiri ukweli huo kwa wengine kwa mwaka mzima na nusu—na sasa nilikuwa na shaka kuhusu vyote nilivyovijua na kufundisha. Ingekuwa ni upotevu kiasi gani kama katika yote hayo hakuna la kweli. Kwa hiyo yalikuwa kweli, yote yale niliyofundisha? Au tu nilikuwa nimetaka yawe ya kweli? Baada ya kuwaona marafiki wakiacha Kanisa na wakati nikikabiliana na mapambano ya imani yangu mwenyewe, nilijiuliza kama nimejidanganya mwenyewe.

Katika kipindi hiki, sikuacha kwenda Kanisani au kutii amri kwa sababu nilikuwa na maswali makubwa. Badala yake, kwa sababu nilikuwa na maswali, nilijaribu kufuata ushauri wa Rais Russell M. Nelson wa “kuongeza uwezo [wangu] wa kiroho ili kupokea ufunuo.”1

Nilijua kwamba “hakuna kinachofungua mbingu kama vile muungano wa usafi uliozidishwa, utiifu mkamilifu, kutafuta kwa bidii, kufurahia kila siku maneno ya Kristo katika Kitabu cha Mormoni, na kutenga muda kwa ajili ya kazi ya hekalu na historia ya familia.”2 Nilihisi ilikuwa muhimu sana kukaa karibu na Mungu. Hata hivyo, Yeye ndiye alikuwa wa pekee ambaye angeweza kuwa na majibu kwa maswali yangu.

Hadithi ya Eunice

Siku moja nilipokuwa nikisoma Watakatifu: Hadithi ya Kanisa la Yesu Kristo katika Siku za Mwisho, nilikutana na hadithi murua kuhusu mwanamke wa Urejesho wa awali. Eunice Franklin alionekana kuwa na maswali na wasiwasi kama wangu.

Eunice alibatizwa New York na mmisionari aliyeitwa Elijah Able. Alikuwa ameongoka kikweli kweli kwenye injili wakati wa ubatizo wake. Kisha, baada ya Elijah kuondoka kwenda Kanada kuhubiri, Eunice alianza kuwa na shaka na injili na kile alichokijua mwanzo kuwa kweli. Alianza kushangaa kama Joseph Smith kwa kweli alikuwa nabii na kama Kitabu cha Mormoni kilikuwa maandiko ya kweli. Alipoteza usingizi mwingi, akifikiri kwamba yawezakuwa amedanganywa.

Bwana alimuonyesha Elijah masumbuko ya Eunice katika ndoto, na mara moja Elijah alirudi New York. Alipogonga mlango wake, Eunice alipigwa na butwaa—alikuwa amepanga kumwambia Elijah kwamba alikuwa haamini tena wakati atakapomwona tena. Badala yake alimkaribisha ndani. Wakati Elijah alipomkaribisha kwenye mahubiri yake jioni ile, alisita na hakutaka kwenda. Lakini hatimaye alikubali na kwenda kusikiliza kile alichotaka kusema.

Kwenye mahubiri yake, Elijah alinukuu 1 Petro 4:12, ambayo inasema “msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu.” Majaribu ya moto ambayo yalitafuta kuharibu imani ya Eunice yasingeweza kufanikiwa—wakati Eunice alipomsikiliza Elijah, shaka yake iliyeyukilia mbali.. Watakatifu inaeleza kwa njia hii: “Uhakika aliokuwa nao mwanzo ulimrudia kwa wingi.”3

Uhakika Unarudi kwa Wingi

Uzoefu wa Eunice ulinishitua, na niliutafakari tena na tena. Kama vile Eunice, nillijifunza kutoka kwa maneno ya kawaida na yenye nguvu ya Elijah. Tunapaswa “kufikiri sio ajabu” kuwa na maswali kuhusu imani yetu. Ni SAWA kabisa. Wakati ukweli hapo awali ulionekana kububujika kutoka mbinguni, kuna uwezekano muda mfupi baadaye tukahisi ukame wa kiroho. Tunaweza kustaajabu kama tuliweza kwa kweli kuhisi mvua. Pamoja na kutokuwa na majibu au uthibitisho kutolewa kwetu, tunaweza kuendelea kusali kwa ajili ya mvua ya ufunuo. Tunaweza kutafuta ushahidi kujua kwamba kile kilichokuwa kweli jana bado ni kweli leo. Mzee Jeffrey R. Holland wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha: “Kama kilikuwa sahihi ulipoomba kukihusu na kuamini na kukiishi, ni sahihi sasa. … Kabiliana na shaka yako. Shinda woga wako.”4

Kwa kufungua mlango tena kwa rafiki yake mmisionari, hata wakati aliposhangaa kwa nini alipaswa kufanya hivyo, Eunice aliufungua upya moyo wake. Bwana angeweza tena kumfikia Eunice na kumsaidia kuhisi uthibitisho wa yote ambayo aliyajua mwanzo. Kwa njia inayofanana, kila mmoja wetu anaweza kufungua mlango wa imani hata wakati tunasumbuliwa na mashaka. Tunaweza kuendelea kufanya kile kilicho sahihi na kutafuta ufunuo—hata wakati hatuna uhakika wa dhati wa kwa nini tunafanya hivyo.

Tunafungua mlango kwa kuendelea kufanya vitu vidogo ambavyo Mungu ametueleza kwamba ni vizuri kwa ajili ya nafsi zetu. Tunaitunza kitakatifu siku ya Sabato na kuhudhuria mikutano yetu. Tunasoma maandiko, hata kama ni mstari mmoja tu nyakati zingine. Tunasikiliza nyimbo au mahubiri ya mkutano mkuu. Tunazungumza na Baba wa Mbinguni kuhusu mashaka na mategemeo yetu na kumwomba Yeye kutusaidia kuujua ukweli. Tunatii amri, kutubu, na kutafuta wenza wa Roho Mtakatifu.

Hata ikiwa hamwezi ila kutamani kuamini tunaweza bado kuendelea kufanya vitu vidogo na kuiacha hamu hiyo kufanya kazi ndani yetu. Tunaweza kuweka nafasi katika mioyo yetu kwa ajili ya kukuza imani zaidi. (Ona Alma 32:27.)

Ninachojua

Picha
man standing before open door

Ingawa wakati mwingine nimeshangaa, na kushangaa, na kuyumbayumba, nimejifunza na kujifunza tena kwa ajili yangu kwamba hili ni Kanisa la Kristo. Ingawa Joseph Smith anaweza kuwa mtu ambaye si mkamilifu, ninajua alikuwa nabii aliyetiwa msukumo na Mungu ambaye alitoa dhabihu kila kitu na kufanya vyema awezavyo. Najua pia kwamba Kitabu cha Mormoni ni kumbukumbu ya kweli ya kale na maandiko matakatifu yaliyohifadhiwa kwa ajili yetu katika wakati wetu. Baba wa Mbinguni anaendelea kuthibitisha kweli hizi kwangu kila siku. Na nina furaha alithibitisha kweli hizi kwa Eunice Franklin pia.

Ninajua kwamba tunapofungua milango na mioyo kwa ajili ya ukweli, Mungu atatusaidia kuhisi kilicho cha kweli na kile kisicho kweli kupitia Roho Mtakatifu. Uzoefu wetu wa kiroho utakuwa usio katalika katika muda mfupi. Na kila muda baada ya uzoefu huo, tunapohisi shaka ikirejea, tunaweza kujikumbusha wenyewe jinsi tulivyohisi. Kama vile ilivyofanya kwa Eunice, uhakika wetu kuhusu kweli za injili zinaweza kurejea kwa wingi.

Hatuhitaji kuishi katika ukame wa shaka kwa muda mrefu sana kama tutashikilia tu kwenye uzoefu wetu wa kiroho. Mzee Neil L. Andersen wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili anasema “kumbatia kumbukumbu zako takatifu. … Amini kwamba zinakuja kwako kutoka kwa Baba yako wa Mbinguni na Mwanawe Mpendwa. Waachie wao wakupe uvumilivu kwenye mashaka yako na uelewa katika magumu yako. Ninakuahidi kwamba kwa hiari unapokubali na kwa umakini kuthamini matukio ya kiroho katika maisha yako, utapokea zaidi na zaidi.”5

Ninajua kwamba kwa wale wanaojitahidi kupata uzoefu mpya wa kiroho na kuonyesha imani katika Kristo, ahadi hii ni ya kweli: “Yeye amwaminiye [Kristo] hataona kiu kamwe” (Yohana 6:35). Majibu tunayohitaji yatakuja. Tunaweza kupita majaribu ya moto ambayo Shetani anayatupa kwenye njia yetu. Na tunaweza kubakia waaminifu kwa Mungu wetu mwenye upendo siku zetu zote.

Muhtasari

  1. Russell M. Nelson, “Ufunuo kwa ajili ya Kanisa, Ufunuo kwa ajili ya Maisha Yetu,” Liahona, Mei 2018, 96.

  2. Russell M. Nelson, “Ufunuo kwa ajili ya Kanisa, Ufunuo kwa ajili ya Maisha Yetu,” 95.

  3. Ona Watatifu: Hadithi ya Kanisa la Yesu Kristo katika Siku za Mwisho, juzuu 1, The Standard of Truth, 1815–1846 (2018), 315-17.

  4. Jeffrey R. Holland, “Cast Not Away Therefore Your Confidence” (Brigham Young University devotional, Mach. 2, 1999), 4 speeches.byu.edu.

  5. Neil L. Andersen, “Spiritually Defining Memories,” Liahona, May 2020, 21–22.