2023
Kutafuta Kusudi la Kiungu katika Familia Yetu “Yenye Mapungufu”
Januari 2023


Kutafuta Kusudi la Kiungu katika Familia Yetu “Yenye Mapungufu” Liahona, Jan. 2023.

Vijana Wakubwa

Kutafuta Kusudi la Kiungu katika Familia Yetu “Yenye Mapungufu”

Kuwa na familia “yenye mapungufu” katika maisha ya hapa duniani kunaweza kuhuzunisha, lakini tunaweza kutumia uhalisia wetu ili kukaribia zaidi kwa Mwokozi.

Picha
msichana mkubwa mwenye wazo la puto la familia

Vielelezo na David Green

Hakuna kitu kinacholeta hisia za kina zenye maana, shangwe, majuto na maumivu kuliko mahusiano ambayo kitovu chake ni uzoefu tuupatao katika maisha ya hapa duniani—mahusiano yetu ya kifamilia. Na kwa sababu mahusiano haya yana maana sana, viongozi wetu wa Kanisa walipata mwongozo wa kiungu na kutengeneza “Famila: Tangazo kwa Ulimwengu.”1 Ukweli wake unatoa ushahidi juu ya Baba mwenye upendo ambaye anatamani sana kwa sisi kujua mipangilio mitukufu ambayo inaongoza kwenye furaha ya milele katika maisha ya kifamilia.

Rais Henry B. Eyring, Mshauri wa Pili katika Urais wa Kwanza, alifundisha: “Kwa sababu Baba yetu anawapenda watoto wake, hatatuacha tukisie kuhusu kipi ni muhimu zaidi katika maisha haya kuhusu wapi usikivu wetu utaweza kuleta shangwe au tofauti zetu zitaweza kuleta huzuni.”2 Hii inajumuisha idadi kubwa mno ya majukumu matakatifu ya kifamilia tunayoweza kuwa nayo katika maisha haya: binti au mwana, dada au kaka, mama au baba, shangazi au mjomba, bibi au babu.

Kweli katika tangazo la familia zinaangaza njia kuelekea “ukamilifu wa milele” ambao wengi wetu tunautamani sana—mahusiano imara ya familia, yenye furaha ya milele. Tatizo ni kwamba tunaishi katika “maisha halisi ya mwili wenye kufa.” Na ufa ule kati ya “halisi” na “kamilifu” unaweza kuwa wenye maumivu. Wakati mwingine, badala ya kuiona kama nuru ya kutuongoza, tunaweza hata kupata uzoefu wa tangazo la familia kama ukumbusho mchungu wa wapi “tumeshindwa” katika kuufikia “ukamilifu.”

  • Yawezekana tukatamani kuwa na ndoa lakini tusiione kama kitu kinachowezekana.

  • Yawezekana tukawa tumefunga ndoa na kupitia uzoefu wa maumivu ya talaka.

  • Yawezekana tukatamani watoto ambao hatuwezi kuwazaa.

  • Yawezekana tumepitia unyanyasaji katika mahusiano ya familia tuliyoiamini.

  • Yawezekana tumepitia uzoefu wa maumivu ya kipekee kwa sababu ya chaguzi za wanafamilia tunaowapenda.

  • Yawezekana tukahisi tumegawanyika licha ya juhudi zetu kubwa za kuleta umoja miongoni mwa wapendwa wetu.

  • Yawezekana hata tukahisi kukata tamaa kwa matamanio na ahadi zisizotimia.

Katika uhalisia, sisi sote tutajua changamoto, maumivu na huzuni katika maisha ya kifamilia—baadhi zaidi ya wengine. Kwa kiwango fulani, sisi sote tutaanguka nje ya mipangilio mikamilifu iliyobainishwa katika tangazo la familia.

Yawezekana kitu tusichoweza kutambua ni kusudi la kiungu katika uhalisia huo.

Kutafuta na Kujiweka chini ya Mwokozi

Kama mwanamke mseja niliyetamani ndoa na watoto kwa miaka mingi, nilitamani na kuamini kwamba kusudi la msingi la maisha yangu lilikuwa kufanikisha ukamilifu wa maisha ya familia kama yalivyoainishwa katika tangazo la familia. Bado licha ya juhudi zangu za dhati, sikuweza kuyafanya yatokee jinsi nilivyoamini nilipaswa kufanya yatokee. Juhudi ile ilikuwa ya maumivu.

Kwa wakati ule, sikuweza kuona kazi ya kimiujiza ambayo Bwana alikuwa anaileta katika moyo wangu kupitia juhudi ile.

Nikiangalia nyuma, matamanio yangu ambayo hayakutimia yalileta jukumu takatifu katika kuinamisha moyo wangu kwa Mkombozi wangu ili kutafuta amani na mwelekeo ambao ni Yeye pekee angeweza kunipa na kuongeza matumaini yangu katika upendo Wake mkamilifu na nguvu Yake ya kuwezesha. Maombi ya kila siku na kujifunza maandiko na hususan maneno ya mkutano mkuu, ikawa tegemeo kuu la tumaini na mwongozo. Nilihisi msukumo kugeukia maneno ya baraka zangu za patriaki—na baraka zingine za ukuhani—ili kutafuta upendo na mwongozo ambavyo vilikuwa binafsi kwangu kutoka kwa Baba yangu wa Milele.

Nilipoumimina moyo wangu wote kwa Bwana, hata wakati nilipokuwa nikijaribiwa kugeukia mbali katika uchungu, misukumo mitakatifu ilikuja kwenye akili na moyo wangu ambayo ilinihakikishia kwamba Yeye alijua wapi nilipokuwa, kwamba maisha yangu yalikuwa na mpango mzuri na kwamba nilipaswa kumtumaini Yeye. Kuwa wa agano3 kwa Mkombozi wangu kukawa mfereji wa amani kubwa na furaha ipitayo chanzo kingine chochote cha kuridhika au furaha.

Nilikuja kuona kwamba ingawa niliamini kusudi la maisha yangu lilikuwa kufanikisha ndoto zangu za familia kamilifu, Bwana alikuwa anafanya iwezekane kile Mzee Jeffrey R. Holland wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alichokiita kusudi la msingi la maisha ya duniani. Akimnukuu Mfalme Benjamini, alifafanua “pengine kusudi la msingi … ni kuwa ‘mtakatifu kupitia upatanisho wa Kristo Bwana,’ ambayo itatutaka sisi kuwa ‘kama mtoto, mtiifu, mpole, mnyenyekevu, mwenye subira, aliyejaa upendo, aliye tayari kukubali vitu vyote ambavyo Bwana anaona vinafaa kuviweka juu yake, hata kama mtoto anavyojiweka chini ya baba yake.’”4

Hitaji langu kwa ajili ya msaada na nguvu ya Mwokozi lilinipeleka kutafuta na kupata uzoefu wa moyo Wake wa utii, upole, unyenyekevu, subira na upendo. Katika mchakato huo nilibadilishwa kwa nguvu Yake ya kuwezesha. Na katika ukweli, hilo ndio nililokuwa nalitaka kwa kina hasa. Kile kilichoonekana “chenye mapungufu”kwa kweli kilikuwa kimeandaa njia kwa ajili ya “ukamilifu” mzuri zaidi.

Rafiki yangu na mshirika Ty Mansfield alieleza ukweli kama huo. Kama mwanamume aliyepata uzoefu wa mvuto wa jinsia moja, Ty alishuhudia ukuaji wa kiroho ambao unaweza kuchukua nafasi wakati tunapoyatia nanga maisha yetu kwa Yesu Kristo na kwa hiari kuachia mioyo yetu yote kwake, tukimruhusu kuweka wakfu magumu yote tunayopitia kwa ajili ya faida yetu. Kwa Ty, hiyo ilianza pale Roho alipomfundisha “kwamba ikitokea nikaoa, nilikuwa ninapendwa na kukubalika kwa Mungu. Jukumu langu lilikuwa kuendelea kuishi siku moja baada ya nyingine huku nikitafuta na kufuata mwongozo wa Roho.”5 Na hatimaye, kumtumaini Mungu kulimwongoza Ty kuingia katika ndoa yenye furaha, nzuri, ya milele kwa mke wake.

Kukuza Mahusiano ya Kina Zaidi na Mwokozi

Mimi pia hatimaye niliolewa baada kujiuliza kama ningeweza kuolewa. Lakini haja ya kutia nanga kwa kina katika Yesu Kristo imeendelea tu, kama si kuongezeka, katika miaka tangu nilipounganishwa kwa mume wangu. Nilianza tena kumtafuta kwa ajili ya amani wakati nilipokuwa nahangaika kwa ugumba. Sikujua jinsi gani ningeweza kwa wakati wowote kuwa na furaha niliyoitumainia katika maisha ya familia bila watoto. Lakini hata baada ya mume wangu na mimi kubarikiwa kwa watoto wawili, mara kwa mara nilifokasi juu ya udhaifu wangu kama mama. Ingawa hatimaye nilipata kile ambacho siku zote nilikuwa nakitaka, katika baadhi ya njia ufa kati ya “ukamilifu” na “uhalisia” ulionekana kukua.

Hali hizi zilinialika kufikiria upya kusudi la maisha ya duniani na michakato ya kiungu iliyowekwa ambayo kupitia hiyo sisi tunakua. Labda kusudi la maisha si hasa kupata familia iliyo kamilifu. Labda ukamilifu haupo kabisa katika maisha ya duniani. Labda familia, badala yake, ni fursa kwa ajili ya maendeleo.

Kwa kweli, labda uhalisia ambao una uchungu “wenye mapungufu kidogo” unatimiza hasa kusudi takatifu la kualika ukuaji tunaouhitaji kwa hakika ili kuishi mahusiano “yaliyo makamilifu.” Labda nguvu ipo katika ukweli kwamba ufa mkubwa kati ya uhalisia na ukamilifu unatualika kwenye mahusiano ya kina na Yesu Kristo ambapo Yeye anaponya na kutakasa kile kinachohisiwa kuvunjika, akijenga hekima, nguvu na upendo katika mchakato. Kimuujiza, ni kupitia neema na ukombozi, na Yake peke yake, kwamba tunaweza kuwa aina ya watu katika aina za mahusiano ambayo tunatafuta kuwa nayo mbinguni.

Nimekuja kuamini kwamba “ukamilifu” kwa kweli hauwezekani katika mahusiano ya kifamilia, kwa yoyote yule—angalau katika maisha haya. Lakini uaminifu, uadilifu na ukaribu wa kweli vinawezekana. Kwa kweli, kujifanya au kutegemea ukamilifu kutaingilia kati ule ukaribu wa kweli na Mungu, familia zetu na wengine. Badala yake, kama tunamruhusu Kristo, familia zetu pamoja na wengine watuone jinsi tulivyo hasa, ikijumuisha katika vyote ambavyo ni “chini ya ukamilifu,” tunaweza kualika nguvu Yake ya utakaso ndani ya maisha yetu. Tunaweza kupata uzoefu wa nguvu Yake ya kimuujiza ili kusuluhisha kile ambacho bado hakijasuluhishwa, kutujaza kwa upendo Wake na kutubadilisha kuwa viumbe ambao tuna mahusiano ya kina na Yeye pamoja na wapendwa wetu.

Pengine kusudi takatifu zaidi la tangazo la familia ni kutuhakikishia kwamba kwa sababu ya Yesu Kristo, familia “yenye ukamilifu” inaweza kuwa majaliwa ya milele kwa kila mmoja wetu.

Kama wana na mabinti wapendwa wa wazazi wa mbinguni, sisi sote ni wa familia ya milele. Uzoefu wetu wa kipekee katika maisha ya duniani ni sehemu muhimu ya mpango wa Baba yetu ili kutusaidia sisi tuendelee na “hatimaye tutambue majaliwa [yetu] ya kiungu kama warithi wa uzima wa milele”6—maisha yale yale mazuri ya familia ambayo Yeye anayapitia, hata kama ni tofauti na ukamilifu ambao familia yetu inapitia kwa sasa. Kama Mzee D. Todd Christofferson wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alivyotamka: “Upatanisho wa Yesu Kristo umetarajia na, mwishoni, utafidia unyang’anyi na upotevu wote kwa wale wanaomgeukia Yeye. Hakuna aliyepangiwa mapema kupokea kidogo kwenye vyote ambavyo Baba anavyo kwa ajili ya watoto Wake.”7

Kama vile Bwana alivyomwahidi Yakobo katikati ya changamoto za familia yake “yenye mapungufu,” uhusiano Wake wa agano pamoja nasi unatuhakikishia, “Mimi nipo pamoja nanyi na nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka [nyumbani]; kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia” (Mwanzo 28:15). Tunapomfuata Yeye, bila kujali uhalisia wa mapungufu yetu unaonekana vipi, Yeye “hatatuacha tupotee,” mpaka tuwe tumeweza kuwa vyote tunavyotamani kuwa, tumeungana katika mahusiano ya kifamilia yenye shangwe tukufu ya milele.

Muhtasari

  1. Ona “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu,” ChurchofJesusChrist.org.

  2. Henry B. Eyring, “Familia,” Liahona, Okt 1998, 10.

  3. Ona Gerrit W. Gong, “Kuwa wa Agano,” Liahona,, Mei 2019, 80–83.

  4. Jeffrey R. Holland, “Mfakatifu kupitia Upatanisho wa Kristo Bwana” (Brigham Young University, Devotional address, Jan. 18 2022), 1 speeces.byu.

  5. Ty Mansfield, Voices of Hope (2011), 5.

  6. “Familia: Tangazo kwa Ulimwengu.”

  7. D. Todd Christofferson, “Kwa Nini Ndoa, Kwa Nini Familia,” Liahona, Mei 2015, 52.