2023
Ni kwa Jinsi Gani Mungu Huniongoza Kutenda Kazi Yake?
Julai 2023


“Ni kwa Jinsi Gani Mungu Huniongoza Kutenda Kazi Yake?,” Liahona, Julai 2023.

Njoo, Unifuate

Matendo ya Mitume 9

Ni kwa Jinsi Gani Mungu Huniongoza Kutenda Kazi Yake?

Picha
Paulo, akiwa kipofu, amekaa chini

Njiani Kwenda Dameski, Lifeway Collection / licensed from Goodsalt.com

Tunaposoma hadithi ya kuongoka kwa Sauli, tunatiwa moyo na kauli yake kwa Mwokozi: “Bwana, unataka nifanye nini?” (Matendo ya Mitume 9:6). Kama mfuasi wa Yesu kristo, mara kwa mara tumeuliza swali sawa na hilo pale tunapotafuta kushiriki katika kazi ya Bwana.

Lakini nini hufuatia baada ya kuuliza swali? Ni kwa jinsi gani tunapokea mwongozo kujua mapenzi ya Mungu kwa ajili ya kazi zetu?

Utayari wa Kutenda

Katika kumjibu Sauli kuhusu anachopaswa kufanya, Bwana mara moja akajibu kwa maelekezo ya yeye kwenda Dameski. Wakati mwingine tunatumainia kwamba Bwana atatupatia mwongozo mahsusi sawa na huo. Lakini hatupaswi kusubiri kwa ajili ya maelekezo ya hatua kwa hatua kabla ya kushiriki katika kazi ya Mungu.

Mzee Dieter F. Uchtdorf wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha, “Mara nyingi, jibu la ombi letu haliji wakati tumepiga magoti kusali lakini wakati tuwapo katika kumtumikia Bwana na kuwatumikia wale wanaotuzunguka” (“Kungojea katika Barabara ya Kwenda Dameski,” Liahona, Mei 2011, 76).

Tafakari jinsi Bwana alivyowaongoza watu hawa wawili katika fursa za kutumikia kwa sababu walikuwa tayari kutenda: