2023
Kushiriki Injili ya Yesu Kristo
Julai 2023


“Kushiriki Injili ya Yesu Kristo,” Liahona, Julai 2023.

Misingi ya Injili

Kushiriki Injili ya Yesu Kristo

Picha
msichana akiwa na maandiko yamefuniliwa juu ya paja

Tunapotafakari kuhusu baraka tunazopokea kwa sababu tu waumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, tunataka kushiriki injili na wale tuwapendao. Tunaweza kushiriki shuhuda zetu za ukweli kupitia maneno yetu na mifano. Tunaweza kuomba kwa ajili ya mwongozo ili kujua mtu wa kushiriki naye na cha kusema.

Picha
Yesu akimsaidia mtu aliyepooza

Wapende Wengine

Sehemu muhimu ya kushiriki injili ni kuwapenda wengine. Tunapoonyesha upendo wetu kwa wengine kupitia matendo kama ya Kristo, tunashiriki injili ya Yesu kristo—wakati mwingine pasipo kusema neno lolote. Na wakati wengine wanapotambua kwamba tunawajali kwa dhati, wanaweza kuwa radhi zaidi kusikiliza mawazo yetu kuhusu injili. (Ona Gary E. Stevenson, “Penda, Shiriki, Alika,” Liahona, Mei 2022, 84–87.)

Shiriki katika Njia za Kawaida na Asilia

Tunaweza kushiriki kile tukipendacho kuhusu injili. Tunapofanya hili kama sehemu ya maisha yetu ya kila siku, haitakuwa jambo baya au lisilofaa. Kwa mfano, tunaweza kuongea na familia na marafiki zetu kuhusu kile tukifanyacho Jumapili. Au tunaweza kuwaambia kuhusu furaha tunayohisi tuwatumikiapo wengine. (Ona Dieter F. Uchtdorf, “Kazi ya Umisionari: Kushiriki Yaliyo Moyoni Mwako,” Liahona, Mei 2019, 15–18.)

Waalike Wengine Kuungana Nasi

Tunaweza kuwaalika wengine kujifunza zaidi kuhusu injili. Kwa mfano, tunaweza kuwaalika wahudhurie mkutano au shughuli ya Kanisa, kusoma Kitabu cha Mormoni, kuangalia video ya Kanisa au kutembelea pamoja na wamisionari. Uzoefu huu unaweza kuwasaidia kumhisi Roho na kutaka kujifunza zaidi.

Picha
wanawake wawili wazee wamekaa wakiongea

Uliza kuhusu Uzoefu Wao

Baada ya marafiki na wanafamilia kuja kanisani au kufundishwa na wamisionari, tunaweza kuwauliza kuhusu uzoefu wao. Baadhi ya mafundisho ya injili yanaweza kuwa mapya kwao, hivyo tunaweza kujibu maswali waliyonayo. Tunaweza kuonyesha upendo na msaada kwa juhudi zao za kusonga kwa Kristo.

Ongezea kwenye Imani Zao

Tunathamini na kuheshimu imani za wengine na tunajaribu kuongeza kwenye imani waliyonayo tayari. Kwa mfano, rafiki ambaye amepata faraja katika maandiko ya Biblia anaweza pia kupata faraja katika mafundisho tunayoshiriki kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni.

Picha
wasichana wakimsaidia mwanamke mzee kuvuka barabara.

Wasaidie Waumini Wapya wa Kanisa

Wakati watu wanapojiunga na Kanisa, tunaweza kusaidia kuimarisha imani zao. Tunaweza kuwa rafiki yao, kujibu maswali yao na kuwasaidia pale wanapopokea wito. Tunawahimiza kuendelea kumfuata Yesu Kristo na kujifunza kuhusu injili Yake.

Picha
wazee wamisionari wawili na mwanaume wakiangalia simu kwa pamoja

Tumikia Misheni

Kwa kuongezea kwenye kushiriki injili katika maisha yetu ya kila siku, waumini wa Kanisa wanaweza kuitwa kama wamisionari. Kama wamejiandaa, wavulana wanaweza kutumikia pale wafikapo miaka 18. Wasichana na watu wazima pia wanaweza kutumikia. Unaweza kupata taarifa zaidi kwenye ChurchofJesusChrist.org/callings/missionary.