2013
Wamisionari Wadogo wa Bibi Deny
Aprili 2013


Wamisionari Wadogo wa Bibi Deny

Emília Maria Guimarães Correa anaishi katika Federal District, Brazil.

“Mwanadamu anapozungumza kwa uwezo wa Roho Mtakatifu uwezo wa Roho Mtakatifu huyapeleka katika mioyo ya watoto wa watu.” (2 Nefi 33:1).

Vítor aliishi na mamake na dadake nyumbani mwa Bibi Deny. Bibiye Vítor akawa mgonjwa na hakuweza kuondoka kitandani mwake kwa wiki nyingi. Alikuwa na upweke katika chumba chake peke yake.

Vítor aliamua kwamba angeweza kumkalisha na Bibi Deny. Kila siku, alipofika nyumbani kutoka shule, alichukua nakala ya Liahona ndani ya chumba cha Bibiye na kumsomea hadithi kutoka kwa kurasa za watoto.

Baada ya kusoma nakala zote za Liahona ambazo familia yake ilikuwa nazo, alianza kumsomea Kitabu cha Mormoni na Biblia. Bibi Deny hakuwa mshiriki wa Kanisa, lakini alipenda kumsikiliza Vítor akimsomea. Alikuwa na furaha ya kujifunza injili.

Bibi aliuliza maswali mengi. Kama Vítor hakujua majibu, angemuliza mwalimu wake wa Msingi au angetafuta katika maandiko. Bibi alimuita Vítor mmisionari wake mdogo.

Bibi Deny alimwambia Vítor kwamba alikuwa amejifunza mengi kutoka kwake. Aliahidi kwamba angeweza kuhudhuria kanisa pamoja naye atakapopona. Yale aliyokuwa amejifunza yalimfanya atake kupata nafuu na kujifunza zaidi kuhusu Injili.

Bibi alipopona, aliweka ahadi yake. Alienda kanisani kujifunza zaidi kuhusu yale aliyokuwa amemfundisha. Haikuwa muda mrefu kabla ya Bibi kubatizwa na kuthibitishwa. Vítor alikuwa amemsaidia kujifunza kwamba injili ni kweli.

Vítor alipokua, alikuwa mmisionari wa muda katika Misheni ya Boston Massachusetts. Kabla ya aondoke, alienda hekaluni—na Bibi Deny.

Picha kwa hisani ya Emilia Maria Guimaraes Correa