2013
Jinsi ya Kuhudumu Katika Wito za Ukuhani
Aprili 2013


Jinsi ya Kuhudumu Katika Wito WA Ukuhani

Kutoka kwa hotuba ya mkutano mkuu wa Aprili 1987.

Picha
Rais Thomas S. Monson.

Je, umewahi kutafakari thamani ya nafsi ya binadamu? Umewahi kujiuliza kuhusu uwezo ambao upo ndani ya kila mmoja wetu?

Niliwai kuhudhuria mkutano mkuu wa kigingi ambapo rais wa kingingi wangu wa zamani Paul C. Child alifungua Mafundisho na Maagano 18 na kusoma: “Kumbuka thamani ya nafsi ni kubwa mbele za Mungu” (aya ya 10).

Rais Child kisha akauliza, “ni nini thamani ya nafsi ya binadamu?” Aliepuka kuita askofu, rais wa kigingi, au mjumbe wa baraza kuu kutoa jibu. Badala yake, alimchagua rais wa jamii ya wazee.

Mtu aliyegutushwa alibaki kimya kwa kile kilichoonekana kama milele na kisha akasema, “Thamani ya nafsi ni uwezo wake wa kuwa kama Mungu.”

Wote waliokuwa pale walitafakari jibu hilo Rais Child akaendelea na ujumbe wake, lakini nikaendelea kutafakari juu ya jibu hilo lililovutiwa.

Ili kufikia, kufundisha, kugusa nafsi za thamani ambazo Baba yetu ametayarisha kwa ujumbe wake ni kazi kubwa. Mafanikio mara chache ni rahisi. Kwa ujumla unatanguliwa na machozi, majaribio, uaminifu, na ushuhuda.

Watumishi wa Mungu huchukua faraja kutoka uhakikisho la Bwana: “Mimi ni pamoja nanyi siku zote” (Mathayo 28:20). Ahadi hii kubwa inawainua nyinyi ndugu wa Ukuhani wa Haruni ambao mmeitwa kwa nafasi ya uongozi katika jamii ya mashemasi, walimu, na makuhani. Inawahimiza nyinyi katika maandalizi yenu ya kumtumikia katika eneo la misheni. Inawafariji ninyi wakati wa kukata tamaa, ambayo huja kwa wote.

“Kwa hiyo, msichoke kutenda mema,” asema Bwana, kwa kuwa mnajenga msingi wa kazi kubwa. Na kutokana na mambo madogo huja yale yaliyo makuu.

Tazama, Bwana anahitaji moyo na akili yenye kukubali” (M&M 64:33–34). Imani ya kudumu, uaminifu wa daima, na hamu ya dhati daima zimetambulisha wale wanaomtumikia Bwana kwa mioyo yao yote.

Kama ndugu yeyote ndani ya mvumo wa sauti yangu wanajisikia hawajajiandaa, hata hawezi kujibu wito wa kuhudumu, ili kujitolea, kubariki maisha ya wengine, kumbuka ukweli: “Yule ambaye Mungu huita, Mungu humuwezesha”

Picha

Kielelezo cha picha na Cody Bell © IRI