2020
Ni jinsi gani Joseph Smith alitafsiri Kitabu cha Mormoni?
Aprili 2020


Ni kwa jinsi gani Joseph Smith alitafsiri Kitabu cha Mormoni?

Picha
Restoration Project: 213 Translation begins. (Joseph and Oliver working on translation).

Kabla ya kuficha bamba za dhahabu, Moroni, nabii wa mwisho katika Kitabu cha Mormoni, aliandika kwenye ukurasa wa jina wa kitabu kwamba kitabu kingetafsiriwa “kupitia karama na uwezo wa Mungu.” Haya yanabakia kuwa maelezo bora zaidi ya tafsiri ya Kitabu cha Mormoni.

Joseph smith alisoma kwa sauti maneno ya tafsiri kwa waandishi, hasa Oliver Cowdery. Kwa sababu Joseph alikuwa akitafsiri lugha isiyojulikana kabisa, alihitaji msaada wa Bwana. Njia moja ambayo Bwana alitoa msaada ilikuwa kutoa vifaa kumsaidia Joseph katika kutafsiri. Mashahidi walisema kwamba Joseph aliangalia kwa kutumia vifaa na kwamba maneno yalionekana kwake kwa Kingereza. Vifaa vya kutafsiri vilijumuisha “vikalimani” au “Urimu na Thumimu”—mawe mawili masafi ambayo yalikuwa yamewekwa katika pinde ili Joseph aweze kutazama ndani yake. Hivi vilikuwa vimekabidhiwa kwa Joseph Smith pamoja na mabamba. Kifaa kingine ambacho Joseph alitumia kilikuwa “jiwe la mwonaji” ambalo angeangalia kupitia hilo, kawaida kwa kuliweka ndani ya kofia. Joseph alikuwa amelipata jiwe hili awali na akawa amelitumia kupata vitu vilivyofichika au vilivyopotea. Alitumia vyote viwili vikalimani na jiwe la mwonaji wakati akitafsiri, siku zote akitegemea msukumo kutoka mbinguni.

Kutafsiri Kitabu cha Mormoni ilikuwa kwa kweli muujiza na kulifanyika “kwa karama na uwezo wa Mungu.”