2020
Ni nini unasema wakati rafiki zako hawaamini kwamba vitu kama Ono la Kwanza vinaweza kutokea?
Aprili 2020


Maswali na Majibu

Ni nini unasema wakati rafiki zako hawaamini kwamba Ono la Kwanza lilitokea?

Picha
Confused Caucasian girl laying on blanket texting on cell phone - stock photo

Kuza imani

Pamoja na maswali ya kiroho, si tu mantiki pekee tunayohitaji; pia tunahitaji imani ili kujua kwamba Ono la Kwanza lingeweza kwa hakika kutokea. Tunaweza kukuza imani hiyo kupitia kumuomba Baba wa Mbinguni na kumsikiliza Roho.

Julia B., miaka 17, California, Marekani

Jifunze Biblia

Waombe rafiki zako wajifunze Biblia. Kama wataiamini kama neno la Mungu, basi ni sharti waamini kwamba Mungu huzungumza nasi leo kupitia maono kama vile Ono la Kwanza kwa sababu Alifanya hivyo kwa Adamu, Musa, Isaya, na manabii wengine kwa njia tofauti.

Mzee Muanda, miaka 22, Misheni ya Kenya Nairobi

Muombe Mungu

Ukweli kwamba ukengeufu ulidumu kwa muda wa mamia ya miaka haimaanishi kwamba Mungu alisitisha maono Yake. Tunahitaji kuwa na moyo mnyenyekevu na kumuomba Mungu kwa kusudi halisi na moyo wa kweli, jinsi alivyofanya Joseph Smith.

Jeremi E., miaka 19, Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Mwamini Mungu

Ningewauliza rafiki zangu, “Unaamini katika Mungu? Unaamini kwamba aliumba vitu vyote? Unaamini kwamba aliwatokea manabii katika siku za kale? Na kama unaamini, kwa nini huamini kwamba inawezekana hivi sasa? Inawezekana!”

Sarah M., miaka 16, Utah, Marekani

Shiriki Ushuhuda Wako.

Ninashiriki ushuhuda wangu pamoja na rafiki zangu kwamba Baba wa Mbinguni hufunua vitu kwa Watoto Wake wakati wanapomwomba Yeye kwa moyo wa kweli ili kujua ukweli. Joseph Smith alikuwa na tamaa ya kujua ukweli, na alitenda kulingana na imani yake. Unaweza pia kufurahia uzoefu wa ajabu kama utamwomba Baba wa Mbinguni kupitia sala kwa moyo wako wote.

Mara C., miaka 20, Lima, Peru

Picha kutoka Getty Images