Misaada ya Kujifunza
Sanduku la Agano


Sanduku la Agano

Pia hujulikana kama Sanduku la Yehova na Sanduku la Ushuhuda, Sanduku la Agano lilikuwa kasha la mstatili au sanduku lililotengenezwa kwa mbao zilizofunikwa kwa dhahabu. Lilikuwa ni alama iliyokuwa ya zamani na takatifu zaidi katika dini ya Waisraeli. Kiti cha Rehema ambacho kilitengeneza maficho yake kiliheshimiwa kama mahali akaapo Yehova hapa duniani (Ku. 25:22). Wakati hekalu lilipokamilika, sanduku liliwekwa katika Patakatifu pa Patakatifu, mahali patakatifu zaidi kuliko pengine katika jengo lile (1 Fal. 8:1–8).