2019
Je, Mungu Ananiongoza?
Aprili 2019


Vijana Wakubwa

Je, Mungu Ananiongoza?

Picha
young adult standing by train

Maisha yetu yamejawa na chaguzi kubwa: kazi ipi ya kufanya, nani wa kufunga naye ndoa, wapi pa kwenda kusoma, n.k. Maisha yetu pia yamejawa na wasiwasi: kuchagua matumizi bora ya muda, kujaribu kuielewa injili, na kutafuta amani katikati ya majaribu. Yote kwa yote, tunahitaji ufunuo binafsi. Lakini wakati mwingine yaweza kuwa vigumu kujua jinsi ya kuupokea na jinsi ya kuutambua pale tunapoupokea. Wakati hatupati au kutambua majibu, tunaweza kujiuliza, “Je, yule alikuwa Roho au mawazo yangu tu?” “Kwa nini nilihisi mwongozo wa kufanya kile na kisha nikashindwa?” “Kwa nini ninahisi kama vile Mungu hajibu sala zangu?”

Kwa bahati nzuri, katika “kufanya Maamuzi: Haki ya Kujiamulia dhidi ya Ufunuo” (ukurasa wa 44), Erin anashiriki hadithi yake kuhusu ufunuo binafsi wakati alipotakiwa kufanya uamuzi wenye kubadilisha maisha. Wakati Mungu anataka kutuongoza, Yeye anataka pia kutusaidia kujifunza kutegemea haki yetu ya kujiamulia kufanya chaguzi nzuri.

Kujifunza jinsi Roho Mtakatifu anavyozungumza na wewe binafsi ni sehemu nyingine ya muhimu ya kupokea na kutambua ufunuo. Inaweza kuwa vigumu kwa kila mmoja wetu. Katika ukurasa wa 48, vijana wakubwa wengi wanashiriki jinsi wanavyopokea ufunuo.

Katika makala ya kidijitali pekee, Aspen anaelezea kwamba ufunuo binafsi huitaji “Kufanyia Mazoezi Misuli Yako ya Kiroho.”

Kufikiria kuhusu wakati ujao kunaweza kuwa kwa kuchosha, hata kuogopesha. Hasa kama kijana mkubwa. Lakini ninapokumbuka jinsi Mungu alivyoyaongoza maisha yangu katika siku za nyuma, inanipa ujasiri wa kusonga mbele na kutenda, nikiamini kwamba Yeye ataendelea kunipa mwongozo ninaohitaji nikiwa njiani.

Kwa moyo wa dhati,

Katie Sue Embley