2019
Onyesho Kuu la Upendo wa Mungu
Aprili 2019


Neno la Mwisho

Onyesho Kuu la Upendo wa Mungu

Kutoka katika hotuba ya mkutano mkuu wa Aprili 1988.

Mungu huonyesha upendo wake kwetu kwa kutoa mwongozo tunaohitaji ili kuendelea na kufikia uwezekano wetu. Yeye anayejua mengi kutuhusu sisi, na uwezekano wetu wa milele ametupatia ushauri mtakatifu na amri katika vitabu Vyake vya mwongozo—maandiko matakatifu. Tunapoelewa na kufuata maelekezo haya, maisha yetu yana lengo na maana. Tunajifunza kwamba Muumba wetu anatupenda na anataka sana furaha yetu. Katika onyesho lisiloweza kufananishwa la upendo huu mtakatifu kwetu, Yeye alimtuma Mwana Wake wa Pekee, Yesu Kristo.

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanaye wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

“Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye” (Yohana —173:16).

Yesu alizaliwa katika ulimwengu. Aliishi maisha makamilifu na, kwa kufanya hivyo, alitengeneza njia kwa ajili yetu kufuata. Yeye aliwafundisha wanafunzi Wake: “Mimi ni nuru ya ulimwengu: yule ambaye ananifuata mimi hatatembea gizani, bali atapata nuru ya uzima” (Yohana 8:12).

Tunaweza kuanza kuelewa kina cha upendo wa Kristo kwetu tunapofikiria kwamba Yeye alikuwa tayari kufanya upatanisho na kuteseka kwa maumivu ya dhambi zetu, “Mateso ambayo yaliyosababisha [yeye], hata Mungu, mkuu kuliko wote, kutetemeka kwa sababu ya maumivu, na kutoka damu kwenye kila kinyweleo, na kuteseka mwili na roho” (Mafundisho na Maagano 19:18).

Pasaka hii, acha tutoe shukrani za kipekee kwa Mungu kwa ajili ya Upatanisho na Ufufuko wa Mwanaye mpendwa, Yesu Kristo. Kwani ndani Yake, Kwake, na kupitia Kwake, hali hii ya muda ya maisha ya kufa inaweza kufanywa ya kudumu, uwepo mkamilifu, ambao maneno hayawezi kuelezea shangwe yetu.

Maajabu yote ya asili ni tazamo la mara moja la nguvu Yake takatifu na onyesho la upendo Wake. Bado muujiza mkuu wa miujiza yote unatusubiri. Utatokea wakati, kwa nguvu Yake, tutatoka kwenye kifo na kaburi kwenda kwenye ulimwengu mpya ambao hautapita, ambapo, ikiwa tutastahili, tutakuwa Naye na baba Yetu wa Mbinguni milele na milele.

Picha
infographic about President Ballard