2020
“Je, Mnacho Kitabu cha Bluu chenye Herufi za Dhahabu?”
Oktoba 2020


“Je, Mna Kitabu cha Samawati chenye Herufi za Dhahabu?”

Wakati fulani baada ya kukitupa kitabu, nilikuwa na hamu ya kujua kile kilichoandikwa ndani yake.

Picha
seaag with Book of Mormon inside

Kielezo na Greg Newbold

Miaka kadhaa iliyopita, nilipokea kitabu cha rangi ya samawati chenye herufi za dhahabu juu ya jalada kutoka kwa wamisionari wanao hudumu kwenye kambi ya jeshi ambapo nilikuwa nikipata mafunzo ya kazi yangu katika Jeshi la Wanamaji la Marekani.

Nilipoanza kusoma kitabu, mtu mmoja aliniambia kuwa ni cha uongo kwa sababu kimenakiliwa kutoka kwenye Biblia. Hii ilinifanya niwe na shaka na uhalisi wa kitabu hiki, lakini nilikishikilia. Nilikisoma kidogo, nikakiweka chini ya begi langu la baharini, na kisha nikakisahau.

Zaidi ya mwaka baadaye, niliamua kusafisha begi langu la baharini. Nilikiona kile kitabu lakini sikuwa na shauku nacho tena, kwa hivyo nikakitupa. Lakini wakati fulani baadaye, nilikua na hamu ya kujua kile kilichokuwa kwenye kile kitabu cha rangi ya samawati na herufi za dhahabu. Sasa ninaamini kwamba hisia hii ilikuja kutoka kwa Roho, “ambaye huongoza kufanya mema” (Mafundisho na Maagano 11:12).

Mwaka 2005, rafiki yangu mpya alinialika niwasikilize wamisionari. Mwanzoni, nilikuwa na maswali na mashaka juu ya yale wanayofundisha, lakini wamisionari walijiamini na walinipa majibu ambayo yalinifanya nielewe.

Wakati nilipogundua kuwa hawa wamisionari walikuwa kama wale ambao nilikuwa nimekutana nao miaka kadhaa iliyopita, niliwauliza kwa shauku, “Je, nyinyi mna kitabu cha samawati chenye herufi za dhahabu?”

“Ndio, tunacho!” mmoja wao alijibu. “Kinaitwa Kitabu cha Mormoni!”

Nilifurahi kupata tena Kitabu cha Mormoni. Kwa kweli, nilikuwa na furaha sana hata kwamba nilikisoma zaidi ya mara moja kwa muda wa chini ya wiki mbili! Niliposoma na kuomba, nikaja kujua kwamba ni neno la Mungu.

lMzee Rubén V. Alliaud wa Sabini aliongea kitu fulani kwenye mkutano mkuu ambacho kinawiana na uzoefu wangu wa Kitabu cha Mormoni: “Msomaji yeyote anayeweka msimamo wa kukisoma kwa dhati [Kitabu cha Mormoni], kwa roho ya maombi, si tu atajifunza kuhusu Kristo bali atajifunza kutoka kwa Kristo—hasa ikiwa wanafanya uamuzi wa ‘kujaribu matokeo ya neno’ [Alma 32:5] na kutolikataa katika hatua ya mwanzo kutokana na madhara ya kutoamini kwenye kile wengine walichosema kuhusu vitu ambavyo hawajawahi kamwe kuvisoma.”1

Kwa kusoma Kitabu cha Mormoni, kuomba, na kumwamini Roho, nimeona mambo makubwa yakitokea katika maisha yangu.

Muhtasari

  1. Rubén V. Alliaud, “Kupatikana kupitia Nguvu ya Kitabu cha Mormoni” Liahona, Nov. 2019, 37.