2020
Kusema Hapana, Kusikia Hapana
Oktoba 2020


Kusema Hapana, Kusikia Hapana

Picha
Saying No, Hearing No

Baba wa Mbinguni anatupenda na anataka sisi tuwe salama! Kusema hapana wakati tunahitaji na kuheshimu wengine wakati wanapotuambia hapana ni njia ambazo tunaweza kujiweka sisi na wengine salama.

Wakati mwingine unahitaji kusema hapana kwa njia nzuri.

“Hapana, asante. Tafadhali naweza kupata maji badala yake?”

Sasa ni zamu yako! Fikiria unahitaji kusema hapana kwa njia nzuri. Ungeweza kusema nini?

Wakati mwingine unahitaji kusema hapana kwa njia yenye nguvu.

“Sitaki kuona hilo! Hatupaswi kuliangalia.”

Sasa ni zamu yako! Fikiria unahitaji kusema hapana kwa njia yenye nguvu. Ungeweza kusema nini?

Wakati mwingine watu wanatuambia hapana ili kutusaidia kubaki salama na wenye afya.

“Samahani, huwezi kwenda. Si salama.”

Sasa ni zamu yako! Fikiria mtu mzima anakwambia hapana na haupendi. Unapaswa kufanya nini?

Wakati mwingine watu wanakuambia hapana wakati wanahisi hawako huru

“Acha! Sipendi mchezo huu.”

Sasa ni zamu yako! Fikiria mtu anakuambia uache kufanya kitu fulani. Unapaswa kufanya nini?

Itakuwaje ikiwa watu hawasikii unaposema hapana? Itakuwaje ikiwa watakuumiza au kufanyia jambo baya?

  • Ondoka kama unaweza.

  • Mwambie mtu mzima unayemwamini kuhusu kilichotokea.

  • Kumbuka kwamba hilo siyo kosa lako.

  • Bila kujali kinachotokea, ujue kuwa Baba yako wa Mbingu na Yesu Kristo wanakupenda kila wakati!