2020
Ninawezaje kuomba kama alivyo fundisha Mwokozi?
Oktoba 2020


Njoo, Unifuate: Kitabu cha Mormoni

Ninawezaje kuomba kama alivyofundisha Mwokozi?

3 Nefi 17–19

(Septemba 28–Oktoba 11)

Picha
How can I pray as the Savior taught

Wakati Kristo alipowatembelea Wanefi, Yeye aliomba pamoja nao mara 11. Kupitia neno na mfano, Yeye aliwafundisha jinsi wanavyopaswa kuomba. Manabii manabii, waonaji na wafunuzi wa siku za mwisho wanaendelea kufundisha kile ambacho Mwokozi alifundisha kuhusu maombi. Hapa kuna mifano michache:

Kile alichofundisha Mwokozi

Kile walichofundisha manabii, waonaji na wafunuzi wa Siku za Mwisho

Omba kwa ajili ya wengine (ona 3 Nefi 17:14, 17, 21; ona pia 3 Nefi 18:23)

“Kuwaombea wengine kwa nguvu zote za mioyo yetu huongeza uwezo wetu wa kusikia na kutii sauti ya Bwana”1

Mjihadhari na kuomba daima” (3 Nefi 18:15)

“Ni kwa njia ya maombi ya dhati na ya moyo kwamba tunaweza kupokea baraka zinazohitajika na msaada unaohitajika kufanya njia yetu katika safari hii ngumu na yenye changamoto wakati mwingine ambayo tunaiita maisha katika mwili wenye kufa.”2

“Ombeni katika familia zenu” (3 Nefi 18:21; ona pia 3 Nefi 17:3)

“Ikiwa … [utashiriki] katika maombi ya kila siku ya familia, …utapokea baraka zilizoahidiwa za Bwana katika kukuza kizazi kizuri,”3

Usizidishe maneno mengi (ona 3 Nefi 19:24; ona pia 3 Nefi 13:7)

“Maombi yetu yanapaswa kuwa rahisi, ya moja kwa moja, na ya dhati,”4

“Endeleeni kuomba” (3 Nefi 19:26)

“Ombeni kila mara Ombeni katika akili zenu, katika mioyo yenu. Ombeni kwa kupiga magoti. Maombi ni ufunguo wako binafsi wa mbinguni. Kufuli liko upande wako wa pazia.”5

Muhtasari

  1. David A. Bednar, “Ombeni Daima,” Liahona, Nov. 2008, 43.

  2. Thomas S. Monson, “Malengo Matatu ya Kukuongoza,” Liahona, Nov. 2007, 120.

  3. Teachings of Presidents of the Church: Howard W. Hunter (2015), 229.

  4. Dallin H. Oaks, “Lugha ya Maombi,” Ensign, Mei 1993, 17.

  5. Boyd K. Packer, “Asubuhi Angavu ya Msamaha,” Liahona, Nov. 2009. 46