2020
Simama juu ya Mwamba wa Ufunuo
Oktoba 2020


Simama juu ya Mwamba wa Ufunuo

Kutoka kwenye hotuba ya mkutano wa ibada, “Simama Milele,” iliyotolewa katika Chuo Kikuu cha Brigham Young mnamo Januari 22, 2019.

Kwa kuwekwa juu ya mwamba wa ufunuo, tunaweza kupata majibu ya maswali muhimu zaidi.

Picha
man standing on mountain surrounded by people yelling

Vielelezo na Michal Dziekan

Kama sehemu ya jukumu nililokuwa nalo kama Kiongozi mwenye Mamlaka miaka michache iliyopita, nilisoma habari nyingi zinazopingana na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, Nabii Joseph Smith, Kitabu cha Mormoni, na matukio ya Urejesho. Toka majukumu hayo yalipobadilika, sijarudi tena kugaagaa katika shida ile.

Kusoma nyenzo hiyo kila wakati kuliniacha na hisia za gizani, na siku moja hisia hiyo ya giza ilinichochea kuandika majibu kadhaa kwenye sehemu ya madai hayo yote ya kupinga. Ningependa kushiriki nanyi baadhi ya mawazo niliyoandika siku hiyo, na ingawa kile nilichoandika kilikuwa kwa faida yangu, natumaini kitakusaidia wewe pia.

Je, Tutasimama Milele?

Nabii Danieli alisema kwamba katika siku za mwisho “Mungu wa Mbinguni angeweka ufalme, ambao kamwe hautaharibiwa: na ufalme huo hautaachwa kwa watu wengine, bali utavunjika katika vipande vipande na kuteketeza falme zote zingine, na utasimama milele” (Danieli 2:44).

Ufalme wa Mungu ni Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. “Litasimama milele.” Swali ni kwamba, Wewe na mimi tutasimama au “[sisi] pia tutaondoka?“ (Yohana 6:67). Na kama tutaondoka, tutakwenda wapi?

Picha
wolf in sheeps clothing

Udanganyifu Ni Ishara ya Wakati Wetu

Wakati Bwana alipoelezea ishara za kuja Kwake na mwisho wa ulimwengu, Alitaja mambo mengi, pamoja na vita na uvumi wa vita, mataifa yakiibuka dhidi ya mataifa, njaa, tauni, matetemeko ya ardhi, na ishara zingine nyingi, pamoja na hii: “Kwani katika siku hizo [leo] kutatokea Makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu, ili mradi, kwamba, kama ikiwezekana, wapate kuwadanganya hata wale walio wateule, ambao ni wateule kulingana na agano” (Joseph Smith—Mathayo 1:22; ona pia Mathayo 24:24).

Sina uhakika wa yote ambayo yanamaanishwa na sifa “kama inawezekana, watawadanganya wateule,” lakini nadhani inamaanisha, angalau, kwamba kila mtu atapata changamoto katika siku yetu.

Kuna wengi ambao wanadanganya, na wigo wa udanganyifu ni mpana. Mwisho mmoja tunakutana na wale wanaoshambulia Urejesho, Nabii Joseph Smith, na Kitabu cha Mormoni. Baadaye tunawaona wale ambao wanaamini katika Urejesho lakini wanadai kwamba Kanisa lina mapungufu na limepotea. Wengine wanadai wanaamini katika Urejesho lakini wamekatishwa tamaa na mafundisho ambayo yanapingana na mitazamo ya siku yetu. Baadhi wasio na mamlaka wanadai kupokea maono, ndoto, na kutembelewa ili kuisahihisha meli, kutuongoza sisi kwenye njia ya juu, au kuliandaa Kanisa kwa ajili ya mwisho wa ulimwengu. Wengine wanadanganywa na roho wa uongo.

Kwenye mwisho mwingine wa wigo tunakuja kwenye ulimwengu mzima wa fadhaa. hakujawahi kuwa na habari zaidi, taarifa potofu, na habari potofu; bidhaa zaidi, vidude, na michezo; na chaguzi zaidi, mahali pa kwenda, na vitu vya kuona na kufanya ili kuchukua muda na usikivu mbali na yale yaliyo muhimu zaidi. Hayo yote na mengi zaidi husambazwa kwa wakati mmoja ulimwenguni kote na vyombo vya habari vya kielektroniki. Hii ni siku ya udanganyifu.

Maarifa Ni Muhimu

Ukweli unatusaidia sisi kuona vizuri zaidi kwa sababu ni “maarifa ya mambo kama yalivyo, na kama yalivyokuwa, na kama yatakavyokuwa” (Mafundisho na Maagano 93:24). Maarifa ni muhimu ili kuepuka udanganyifu, ili kutambua kati ya ukweli na makosa, na kuona wazi na kuchora ramani ya uelekeo kupitia hatari za siku yetu.

Nabii Joseph Smith alisema: “Maarifa ni muhimu kwa uhai na uchamungu. … Maarifa ni ufunuo. Sikia… ufunguo huu mkuu: maarifa ni nguvu ya Mungu kwa wokovu.”1

Watu wanasema, “Unapaswa kuwa mkweli kwa imani zako.” Wakati hiyo ni kweli, huwezi kuwa bora kuliko kile unachokijua. Wengi wetu tunachukua hatua kulingana na imani zetu, haswa tunachoamini kuwa ni kwa faida yetu. Shida ni kwamba, wakati mwingine tunakosea.

Watu wengine wanaweza kumwamini Mungu na kwamba ponografia sio sahihi na bado unabonyeza kwenye tovuti ya ponografia, kwa kuamini vibaya kwamba watakuwa na furaha zaidi ikiwa watafanya au hawawezi kujizuia bali kubofya au kwamba hawamuumizi mtu mwingine yeyote. Wanakosea kabisa.

Wengine wanaweza kuamini sio sawa kudanganya na bado wanadanganya kwa nyakati fulani, kimakosa wakiamini kuwa watakuwa bora zaidi ikiwa ukweli haujafahamika. Wanakosea kabisa.

Mtu anaweza kuamini na hata kujua kwamba Yesu ndiye Kristo na bado anamkataa sio mara moja lakini mara tatu kwa sababu ya imani potofu kwamba angekuwa bora kwa kuuridhisha umati. Petro hakuwa muovu. Na hata siamini kama alikuwa dhaifu. Alikuwa amekosea tu. (Ona Mathayo 26:34, 73-75.)

Tunapotenda vibaya, tunaweza kujifikiria kuwa sisi ni wabaya, wakati ukweli ni kwamba tumekosea tu. Changamoto sio kupunguza sana pengo kati ya matendo yetu na imani zetu; badala yake, changamoto ni kupunguza pengo kati ya imani zetu na ukweli.

Je, tunapunguzaje pengo hilo? Je, tunaepukaje udanganyifu?

Picha
man walking up steps

Maswali ya Msingi na Maswali ya Upili

Kuna maswali ya msingi na kuna maswali ya upili. Anza kwa kujibu maswali ya msingi kwanza. Maswali ya msingi ndiyo ya muhimu zaidi. Kuna maswali machache tu ya msingi. Ninayataja manne:

  1. Je, kuna Mungu ambaye ni Baba yetu?

  2. Je, Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, Mwokozi wa Ulimwengu?

  3. Je, Joseph Smith alikuwa nabii?

  4. Je, Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni ufalme wa Mungu duniani?

Kwa upande mwingine, maswali ya upili hayana mwisho. Ni pamoja na maswali juu ya historia ya Kanisa, ndoa ya mitala, watu wa asili ya Kiafrika na ukuhani, wanawake na ukuhani, tafsiri ya Kitabu cha Mormoni, Lulu ya Thamani Kuu, DNA na Kitabu cha Mormoni, ndoa za mashoga, maelezo tofauti juu ya Ono la Kwanza, na kuendelea.

Ikiwa unajibu maswali ya msingi, maswali ya upili hujibiwa pia, au yanapauka maana. Jibu maswali ya msingi, na unaweza kushughulika na vitu unavyoelewa na vitu ambavyo hauvielewi na vitu unavyovikubali na vitu usivyovikubali bila ya kurukia meli.

Njia ya Kiungu ya Kujifunza

Kuna njia tofauti za kujifunza, ikiwemo njia za kisayansi, uchambuzi, kitaaluma, na njia za kimungu. Njia zote nne ni muhimu ili kujua ukweli. Zote zinaanza kwa njia ile ile: na swali. Maswali ni muhimu, hususani maswali ya msingi.

Njia ya kiungu ya kujifunza inajumuisha elementi za mbinu zingine lakini mwishowe hupiga baragumu kwenye kila kitu kingine kwa kugonga kwenye nguvu za mbinguni. Mwishowe mambo ya Mungu yanafahamika kwa njia ya Roho wa Mungu, ambayo kwa kawaida ni sauti ndogo, tulivu. Bwana alisema, “Mungu atakupa maarifa kwa njia ya Roho wake Mtakatifu, ndiyo, kwa kipawa chake cha ajabu cha Roho Mtakatifu” (Mafundisho na Maagano 121:26).

Mtume Paulo alifundisha kwamba hatuwezi kujua mambo ya Mungu isipokuwa kwa njia ya Roho wa Mungu (ona 1 Wakorintho 2:9-11; ona pia Joseph Smith, Tafsiri ya, 1 Wakorintho 2:11). Alisema, “Mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuuzi.” Tunaona hayo kila siku. Paulo aliendelea, “Wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya roho” (1 Wakorintho 2:14).

Shida zote unazokutana nazo katika maisha, moja inakuwa juu ya nyingine zote na haieleweki zaidi. Mbaya zaidi ya hali zote za mwanadamu sio umaskini, magonjwa, upweke, unyanyasaji, au vita—ni mbaya kama hali hizo zilivyo. Hali mbaya zaidi ya zote ya mwanadamu ya kawaida zaidi: ni kufa kiroho. Ni kutengwa na uwepo wa Mungu, na katika maisha haya, uwepo Wake ni Roho au nguvu Yake.

Kinyume chake, hali bora zaidi ya zote ya wanadamu sio utajiri, umaarufu, ufahari, afya njema, heshima ya wanadamu, usalama, au alama nzuri. Hali bora zaidi ya zote ya mwanadamu ni kujaliwa maarifa ya nguvu za mbinguni. Ni kuzaliwa tena, kuwa na kipawa na wenza wa Roho Mtakatifu, ambaye ni chanzo cha maarifa, ufunuo, nguvu, uwazi, upendo, shangwe, amani, matumaini, kujiamini, imani, na karibia kila kitu kingine kizuri.

Yesu alisema, “Mfariji, ambaye ni Roho Mtakatifu, … atawafundisha mambo yote” (Yohana 14:26). Ni uwezo ambao kwa huo “tunajua ukweli wa vitu vyote.” (Moroni 10:–5). “Atatuonyesha … [sisi] vitu vyote … [tunavyo] stahili kutenda” (2 Nefi 32:5). Ni chemchemi ya “maji yaliyo hai” ambayo hutoka kwenye uzima wa milele (Yohana 7:38; ona pia mstari wa 37).

Lipa bei yoyote ambayo lazima ulipe, beba mzigo wowote ambao lazima ubebe, na utoe dhabihu yoyote unayolazimika kufanya ili kuipata na kuitunza katika maisha yako roho na nguvu ya Roho Mtakatifu. Kila kitu kizuri hutegemea kuipata na kuitunza nguvu ya Roho Mtakatifu katika maisha yako.

Picha
man surrounded by question marks

“Kile Kisichojenga”

Kwa hivyo, ile huzuni niliyoisikia miaka kadhaa iliyopita wakati wa kusoma taarifa za adui ilikuwa ni kitu gani? Wengine wangesema kuwa huzuni ile ni matokeo ya imani ya upendeleo, ambayo ni sawia ya kuchukua na kuchagua vitu ambavyo vinakubaliana na mawazo na imani zetu. Wazo la kwamba kila kitu ambacho mtu amekiamini na kufundishwa kinaweza kuwa si sahihi, hasa bila kitu bora kuchukua nafasi yake, ni wazo dhaifu na la kutatanisha hakika.

Lakini huzuni niliyoipitia wakati nikiwa naisikiliza kwaya ya giza ya sauti zilizopazwa dhidi ya Nabii Joseph Smith na Urejesho wa Kanisa la Yesu Kristo ni tofauti. Huzuni hiyo sio imani ya upendeleo, na sio hofu ya kuwa katika makosa. Ni kutokuwepo kwa Roho wa Mungu. Ni hali ya mwanadamu wakati akiwa “ameachwa peke yake” (Mafundisho na Maagano 121: 38). Ni huzuni ya giza na “mzubao wa mawazo” (Mafundisho na Maagano 9:9; ona pia mstari wa 8).

Bwana alisema:

Na kile kisichojenga siyo cha Mungu, nacho ni giza.

Kile kilicho cha Mungu ni nuru; na yule ambaye huipokea nuru, na kukaa ndani ya Mungu, hupokea nuru zaidi; na nuru hiyo huzidi kung’ara hata mchana mkamilifu” (Mafundisho na Maagano 50:23–24).

Ufunuo kutoka kwa Roho wa Mungu unachukua nafasi ya imani ya upendeleo kwa sababu haujapatikana kwa ushahidi tu. Nimetumia maisha yote kutafuta kusikia neno la Bwana na kujifunza kutambua na kumfuata Roho wa Mungu. Roho inayohusishwa na sauti za giza zinazomshambulia Nabii Joseph Smith, Kitabu cha Mormoni, na Urejesho sio roho ya nuru, akili na ukweli. Sijui mengi, lakini naijua sauti ya Bwana, na sauti Yake haiko katika kwaya hiyo ya giza.

Kinyume kabisa na huzuni na mzubao wa kudhoofisha wa mawazo ambao unaeneza maji ya shaka ni roho ya nuru, akili, amani na ukweli unaosherehekea matukio na mafundisho matukufu ya Urejesho, hasa maandiko yaliyofunuliwa kwa ulimwengu kupitia Nabii Joseph Smith. Yasome tu na ujiulize mwenyewe na Mungu ikiwa hayo ni maneno ya uwongo, ulaghai, na udanganyifu au ikiwa ni ya kweli.

Huwezi Kujifunza Ukweli kwa Kuondoa

Wengine ambao wanaogopa kwamba Kanisa linaweza kuwa sio la kweli hutumia muda wao na umakini wakitembea kwa bidii kwenye njia ya maswali ya upili. Kwa makosa wanajaribu kujifunza ukweli kwa mchakato wa kuondoa, kwa kujaribu kuondoa kila shaka. Hilo daima ni wazo baya. haliwezi kufanya kazi kamwe.

Kuna madai na maoni yasiyo na mwisho yaliyotolewa kinyume na ukweli. Kila wakati unapopata jibu la dai moja la kupinga na kuangalia juu, jingine linakuangalia usoni. Sisemi kwamba unapaswa kuweka kichwa chako kwenye mchanga, lakini ninasema unaweza kutumia maisha yako yote ukifuatilia jibu la kila dai lililotolewa dhidi ya Kanisa na kamwe usifikie maarifa ya ukweli muhimu zaidi.

Majibu ya maswali ya msingi hayaji kwa kujibu maswali ya pili. Kuna majibu kwa maswali ya upili, lakini huwezi kuthibitisha mazuri kwa kuondoa kila hasi. Hauwezi kuthibitisha Kanisa ni la kweli kwa kutokubali kila madai yaliyotolewa dhidi yake. Ni mkakati ulio na makosa. Mwishowe lazima kuwe na uthibitisho wa kukubalika, na kwa mambo ya Mungu, uthibitisho wa kukubalika hatimaye na hakika unakuja kwa ufunuo kupitia roho na nguvu ya Roho Mtakatifu.

Kwa wanafunzi Wake, Yesu aliuliza:

“Ninyi mnasema mimi ni nani?

“Naye Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

“Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Baryona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.

“… Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; na milango ya kuzimu haitalishinda” (Mathayo 16:15–18; ona pia mstari wa 13–14).

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho limejengwa juu ya msingi wa ufunuo, na wala milango ya kuzimu haitalishinda. Wewe na mimi ni Kanisa. Lazima tujengwe juu ya mwamba wa ufunuo, na ingawa labda hatujui jibu la kila swali, lazima tujue majibu ya maswali ya msingi. Ikiwa tutafanya hivyo, milango ya kuzimu haitatushinda na tutasimama milele.

Picha
man holding up candle

Simama juu ya Mwamba wa Ufunuo

Kuna Mungu mbinguni ambaye ni Baba yetu wa Milele. Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, Mkombozi wa ulimwengu. Joseph Smith alikuwa nabii wa Mungu aliyeweka msingi kwa ajili ya Urejesho wa ufalme wa Mungu. Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ni ufalme wa Mungu duniani. Ninajua hili kwa uzoefu wangu—wote. Ninajua hili kwa ushahidi, na ushahidi ni mkubwa. Mimi najua hili kwa kujifunza. Na, hakika zaidi, ninajua hili kwa njia ya roho na nguvu ya Roho Mtakatifu.

Na kwa hiyo, ninajua kila kitu ninachohitaji kujua ili kusimama milele. Naomba tusimame juu ya mwamba wa ufunuo, hasa kuhusiana na maswali ya msingi. Ikiwa tutafanya hivyo, tutasimama milele na hatutaondoka kamwe.

Muhtasari

  1. Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith (2007), 265.